Nyuma ya Mtaala wa Elimu Tanzania

Nyuma ya Mtaala wa Elimu Tanzania

Victor Mlaki

JF-Expert Member
Joined
May 1, 2016
Posts
4,151
Reaction score
4,277
NYUMA YA MTAALA WA ELIMU WA TANZANIA

Naomba nianze na ile salamu yetu ya " Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kazi iendelee".

Leo tarehe 6/4/2021 nimefarijika sana baada ya kusikia kauli muhimu " tendo uneni" kutoka kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ndg. Samia Suluhu Hassan ikihitaji mtaala wetu kuangaliwa kwa jicho pevu.

Kauli hii muhimu katika mustakabali wa elimu Nchini imelenga kusukuma tathmini ya elimu ili kupata elimu bora itakayonmsaidia Mtanzania kuliko hali ilivyo sasa. Hali hii inaonesha kuna tatizo kubwa katika elimu yetu. Sharti tujiulize huu mtaala uliopo kwa nini upo ulivyo na kwa nini unazalisha wasomi wa aina tunayoiona Nchini.

Serikali mekuwa ikitatua kero nyingi zinazohusiana na elimu mara kadhaa kwa kuuangalia mtaala wa elimu na kuacha suala linaloutawala mtaala wa elimu yaani "Falsafa ya Taifa". Huu ndiyo wakati muhimu wa kuiangalia falsafa yetu kwa makini zaidi kama tunataka kufanya kuhakikisha elimu itasaidia kila Mtanzania.

Kabla ya kuangalia Mtaala sharti tufahamu kwa dhati kabisa "TUNATAKA KUJENGA TAIFA LA NAMNA GANI?.Kama hatufahamu aina ya Taifa tunalolitaka ni vigumu sana kupata suluhu ya kudumu ya changamoto na matatizo ya elimu yetu.

Tukifahamu barabara aina ya Taifa tunalotaka kilijenga ndipo tutakapoweza kuweka mipango ya elimu yenye kufikisha kwenye shabana hiyo (Nyerere, 1968). Ipo kila sababu ya shabana na nguzo za Taifa kuwekwa wazi na kueleweka kwa kila mtu. Kwa mfano falsafa ya ujamaa kama ilivyoasisiwa na Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius. Kambarage Nyerere ilitamka wazi nguzo tatu ambazo ni;
(i) Usawa na heshima za ubinadamu
(ii)Kushirikiana mali inayotokana na juhudi zetu
(iii)Kazi kwa kila mtu na kufuta unyonuaji.Mambo haya matatu yalielekezwa kuwa ni Kanuni za Taifa. Tunapoona shida kwenye elimu yetu tunapaswa kuangalia Kanuni zetu zinasemaje?.. Je tunazifahamu kwa dhati kanuni za Taifa letu?.

Elimu yetu imekuwa ikisukumwa sana na kumbo la wakati na mahitaji yake kuliko mahitaji halisi ya jamii yetu " SHABAHA YETU". Utandawazi umesababisha mabadiliko makubwa kwenye mtaala wetu wa elimu kuliko namna ambavyo mtaala wetu ulipaswa kuendana na shabaha yetu "AINA YA TAIFA TUNAOLIHITAJI".

Watanzania hatuna budi kukubali hali ya elimu ndani na nje ya Nchi yetu ilivyo sasa lakini "TUNALO JUKUMU LA KUHAKIKSHA HALI HIYO INAENDANA NA SHABAHA YETU. Kwa maana nyingine ni kwamba, pamoja na kupokea mabadiliko makubwa kutokana na maendeleo ya sayansi na teknolojia yanaosukumwa nautandawazi bado tunapaswa kuangalia shabaha yetu " AINA YA TAIFA TUNALOLITAKA"

Tunaweza tukaingia katika utandawazi ila badala kuiga kila kitu tukachanganya "glocalization" bila kutoka kwenye shabaha. Nchi kama Japan inaonekana kufanya vizuri kwenye teknolojia na pia elimu kwa kutokana na tabia ya kuchukua na kuchanganganya na utamaduni wake. Hali hii inalifanya Taifa kulinda shabaha yake.

Mambo haya yote yanahitaji zaidi ya matamko ila yanajikita zaidi katika utendaji wa ila siku imani ya jamii. Tunapaswa kufikia mahali ambapo kila Mtanzania anakuwa siyo tu sehemu ya utekelezaji ila utekelezaji wenyewe wa shabaha ya Taifa hili.
 
Professor Mkuu amesikia by the way lile someone la Historia ya Tanzania ndio litazalisha wasomi wa kupambana na ukosefu wa ajira?
 
Professor Mkuu amesikia by the way lile someone la Historia ya Tanzania ndio litazalisha wasomi wa kupambana na ukosefu wa ajira?
Sualani falsafa ya Taifa ambayo ndiyo msingi Mkuu wa shabaha na imani ya Taifa
 
Ondoa wasiwasi mkuu.kama kweli wewe ni mdau wa elimu unafaa kujua mtaala uliopo umekaa vizuri. Kinachohitajika ni usimamizi na uwezeshwaji ili utekelezwe prof anajielewa sana sema swala la somo la historia linahitaji mjadala mpana.
 
Ondoa wasiwasi mkuu.kama kweli wewe ni mdau wa elimu unafaa kujua mtaala uliopo umekaa vizuri...kinachohitajika ni usimamizo na uwezeshwaji ili utekelezwe....prof anajielewa sana sema swala la somo la historia linahitaji mjadala mpana...
Wekeni motivation kwa hao walimu. Vinginevyo Ni kazi ya kulalama tu
 
Ondoa wasiwasi mkuu.kama kweli wewe ni mdau wa elimu unafaa kujua mtaala uliopo umekaa vizuri...kinachohitajika ni usimamizo na uwezeshwaji ili utekelezwe....prof anajielewa sana sema swala la somo la historia linahitaji mjadala mpana...
Mkuu wasiwasi wangu ni huu
tafuta mwanafunzi yeyote wa tena wa kidato cha nne au sita muuleze " Falsafa a Taifa lako unasemaje?" .
Ukipata jibu linaloelweka njoo.
 
Mkuu wasiwasi wangu ni huu
tafuta mwanafunzi yeyote wa tena wa kidato cha nne au sita muuleze " Falsafa a Taifa lako unasemaje?" .
Ukipata jibu linaloelweka njoo.
Mkuu victor, Mtaala ulioboreshwa umefikia darasa la saba tu tangu ulipoanza kutekelezwa.Ukifanya utafiti utagundua kuwa elimu wanayoipata watoto wetu walioko shule za msingi unawapa umahiri zaidi ya mfumo wa elimu tuliyokuwanayo hapo mbeleni.tutafika tu...
 
Hali sio shwari kwa waliopo maana ni zao la mtaala wa zamani...ni vyema tukajua mchango wa wazazi na wadau wengine kama wizara husika kwenye malezi na utekelezaji wa mtaala respectively.
Mkuu wasiwasi wangu ni huu
tafuta mwanafunzi yeyote wa tena wa kidato cha nne au sita muuleze " Falsafa a Taifa lako unasemaje?" .
Ukipata jibu linaloelweka njoo.
 
Mkuu hujanijibu swali langu, Je watu wanaoelewa shabaha ya Taifa?..angalia hata Sisi Walimu je tunaielewa vizuri falsafa ya Taifa letu na kuirithisha kwa jamii pana?
Hali sio shwari kwa waliopo maana ni zao la mtaala wa zamani...ni vyema tukajua mchango wa wazazi na wadau wengine kama wizara husika kwenye malezi na utekelezaji wa mtaala respectively.
 
Elimu bure, si Elimu Bora.
Wazazi waliambiwa wafyatue.
Kuna haja ya mtaala kuwa decentralised, ila wenye usimamizi wa kina kwelikweli.
Elimu ya Ujamaa na Kujitegenea ilikuwa sahihi zama za Nyerere, kwa sasa ELIMU YA KUJITEGEMEA inapaswa kupewa kipaumbele.
Watu wasome kadiri ya mahitaji ya jamii husika na taifa.
 
Elimu bure, si Elimu Bora.
Wazazi waliambiwa wafyatue.
Kuna haja ya mtaala kuwa decentralised, ila wenye usimamizi wa kina kwelikweli.
Elimu ya Ujamaa na Kujitegenea ilikuwa sahihi zama za Nyerere, kwa sasa ELIMU YA KUJITEGEMEA inapaswa kupewa kipaumbele.
Watu wasome kadiri ya mahitaji ya jamii husika na taifa.
Garbage in Garbage Out (GIGO)
Unachokiingiza ndicho unachokitoa, Unavuna ulichopanda, "Quid pro quo".

Kutaka elimu ya Tanzania kuwa bora na kumuacha Mwalimu ni sawa na kusaga wa mahindi na kutegemea kupata unga wa mihogo "UDAGA".

Uthibiti unapaswa kuanza na kuthibiti ubora wa Walimu kabla ya ubora wa elimu. Mifumo ya uthibiti inapaswa kuwa na mawanda mapana na changamani " diverse and holistic" kuliko ilivyo sasa.

Uthibiti uangalie kila kinachoingia katika mfumo wa elimu (input), Mchakato wake (process), Matokeo (Output) na mawanda mapana zaidi ya matokeo kwa jamii (outcome).

Uangalizi (control)ili kutawala matokeo ni muhimu katika kila hatua ya mchakato mzima wa elimu kuanzia ( Input-Process-Output- Otcome).

Sharti pawepo na mianya ya mrejesho au mshindo nyuma (feedback loops) katika kila hatua ili kujenga utamaduni endelevu wa kuthibiti kuliko hali ilivyo sasa ambapo kwa kiasi kikubwa tunaangalia zaidi mchakato na matokeo tunaacha mawanda mapana ya matokeo na raslimali zinazoingia kwenye mfumo bila uangalizi wa kutosha.

Ikumbukwe "Ujinga ni Adui".
 
Ondoa wasiwasi mkuu.kama kweli wewe ni mdau wa elimu unafaa kujua mtaala uliopo umekaa vizuri...kinachohitajika ni usimamizi na uwezeshwaji ili utekelezwe....prof anajielewa sana sema swala la somo la historia linahitaji mjadala mpana...
Umekaa vizuri kwenye vitu gani kwa mfano?
 
Back
Top Bottom