Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
NYUMBA YA OMARI SELEMANI KAGOBE NA MNARA WA NYERERE KIGOMA UJIJI
Mbele ya nyumba ya marehemu Omari Selemani Kagobe umejengwa mnara unaojulikana kama Mnara wa Nyerere.
Mnara huu ni kumbukumbu yake Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere safari yake ya kwanza kufika Kigoma wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.
Katika safari hii Mwalimu Julius Nyerere alifikia nyumbani kwa Omari Selemani Kagobe.
Bahati mbaya mzalendo Omari Selemani Kagobe na wapigania uhuru wenzake hawafahamiki na historia hii haijapewa umuhimu unaostahili halikadhalika kumbukumbuku hii ya nyumba na mnara wake.
Ni suala la muda tu nyumba itatoweka na mnara sawia.
Kitakachobaki ni simulizi kuwa hapo ilikuwapo nyumba ya Omari Selemani Kagobe nyumba aliyolala Mwalimu Nyerere wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.
Mbele ya nyumba ya marehemu Omari Selemani Kagobe umejengwa mnara unaojulikana kama Mnara wa Nyerere.
Mnara huu ni kumbukumbu yake Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere safari yake ya kwanza kufika Kigoma wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.
Katika safari hii Mwalimu Julius Nyerere alifikia nyumbani kwa Omari Selemani Kagobe.
Bahati mbaya mzalendo Omari Selemani Kagobe na wapigania uhuru wenzake hawafahamiki na historia hii haijapewa umuhimu unaostahili halikadhalika kumbukumbuku hii ya nyumba na mnara wake.
Ni suala la muda tu nyumba itatoweka na mnara sawia.
Kitakachobaki ni simulizi kuwa hapo ilikuwapo nyumba ya Omari Selemani Kagobe nyumba aliyolala Mwalimu Nyerere wakati wa kupigania uhuru wa Tanganyika.