Nyumba au Biashara

nyabaheta

JF-Expert Member
Joined
Dec 4, 2012
Posts
247
Reaction score
82
Habari wadau,nilipita eneo flani hapa dar nikasikia vijana wakibishana,upande mmoja ulikua unasema ukipata pesa afadhali ufanye biashara kwanza ndo baadae biashara ije ikupe makazi,yaani ujenge nyumba yako ya kuishi na upande wa pili ulikua unasema bora nyumba kwanza halafu ndo uje ufanye biashara sasa wewe mwenye ndoto za kuwa mjasiriamali siku moja unadhani kipi ni bora?

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 


Mimi naona Kwanza unatakiwa Ufanye Biashara, nyumba mara nyingi kama ni ya Kuishi haina return so huwezi kuila hiyo nyumba, ila ukiwa Mjasirimali na ukafanikiwa kujenga ni simple sana tena sio kujenga unanunua gheto likiwa na kila kitu wewe ni kwenda na Nguo zako tu kuanza maisha,
 

Kweli kabisa mkuu chasha,ile kuambiana kwamba ukipata pesa jenga kwanza haina nguvu asilimia mia kwa mtu anayesaka uhuru.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Kweli kabisa mkuu chasha,ile kuambiana kwamba ukipata pesa jenga kwanza haina nguvu asilimia mia kwa mtu anayesaka uhuru.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Ni kweli haa Mambo ya Kujenga yapo tu na ni pesa yako, siku hizi watu kwanza hawataki kujihangaisha na mafundi, mtu anafika na kununua kitu ikiwa tiyali,

Ujue katika maswala ya Kiuchumi kujenga Nyumba kwa pesa yako mwenyewe ni makosa sana, ila Ndo kama hivyo na mara nyingi nyumba za kuishi inatakiwa zijengw kwa mikopo ya Muda Mrefu kwa sababu haina return kabisa
 
fanya biashara kwanza ila cha muhimu kama unataka kujenga uanze kurecord mapato yako uweze kukopa mkopo wa muda mrefu ujenge nyumba au ununue nyumba , ni rahisi kusema lakini kibongo bongo kuwa na deni la mil 200 unalilipa taratibu kwa miaka 20 si kitu ambacho wafanyabiashara wengi wanakipenda ....
 
Inategemea, kama muajiriwa jenga kwanza pale ulipo. Ukihama waweza uza nyumba na kupata mtaji. Kumbuka ulijenga kwa pesa za kudunduliza, ukaishi kwenye hiyo nyumba na ukiuza unapata pesa ya pamoja ambayo yaweza kuwa mtaji wa biashara.
 
Inategemea, kama muajiriwa jenga kwanza pale ulipo. Ukihama waweza uza nyumba na kupata mtaji. Kumbuka ulijenga kwa pesa za kudunduliza, ukaishi kwenye hiyo nyumba na ukiuza unapata pesa ya pamoja ambayo yaweza kuwa mtaji wa biashara.

Hakuna kitu wabongo tunaogopa kama kuuza nyumba,na isitoshe unayo hiyo moja tu.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Jenga nyumba halafu chukulia mkopo ufanyie biashara ukiona mtaji unataka kuzama unafunga biashara unarudisha mkopo fasta unabaki na nyumba yako. Kesho ukipata biashara poa zaidi unachukua tena mkopo nyumba iko palepale. Mambo ya kusema usijenge ufanyie biashara uwezekano wa mtaji kudidimia na biashara kufa ni mkubwa kwa kuwa hakuna mabiashara yenye uhakika wa kuleta faida wakati wote na kama yapo yalishakamatwa na wajanja kitambo sana.
 
Mkuu watu wanatofautiana malengo na mataji wa biashara maana hapa mtoa mada hajazungumzia mtaji wa kiasi au nyumba ya sh ngapi, kuna mtu mwingine anaweza jenga ili apate sifa ya kuwa hadhi ya kupata hela nyingi hata kwenye mabenki ili afanye biashara kubwa hii inatokana na kipato chake cha awali kuwa kidogo kidogo alishindwa kufanya biashara.Maisha hayana kanuni
 
Mkuu sijajua unazungumzia nyumba ya thamani gani na wapi maana ukiwa na uwezo wa kununua nyumba nzuri kwa cash sidhani hata mjadala huu unakuhusu kwa maana nyingine mambo safi hasa kwa maisha ya wa TZ wengi
 

Pessmistic.....unavyosema hakuna hata kama ipo umeshaufunga ubongo wako kuona fulsa....tatzo la umaskin sio fulsa wala mtaji ni the way maskini anavyofikili,ndo maana matajili ni wa chache cz n wa2 wachache waliokubali kuwaza tofauti...
 
Pessmistic.....unavyosema hakuna hata kama ipo umeshaufunga ubongo wako kuona fulsa....tatzo la umaskin sio fulsa wala mtaji ni the way maskini anavyofikili,ndo maana matajili ni wa chache cz n wa2 wachache waliokubali kuwaza tofauti...

Wewe ni tajiri? kiingereza kibovu, kiswahili kibovu utaelewekaje? si bora unyamaze au ongea basi kikwenu. Kwa ubongo wako wewe unaouona supa kila anayeanzisha biashara anapata faida na kutajirika? Unajua kitu trial and error? kwanini vyuoni wanafundisha probability? acha kuongea pumba kwanza hueleweki
 

usiwake kaka..kubali changamoto ya kubadilika,ni kweli co mzuri kwenye both kiingereza na kiswahili lakin tofauti ni the way 2navyofikili 2....nafasi zipo ni kufikili kwako 2,nakuacha na this two quotes utafakali kwa makini kabla hujawaka tena cz i know ua a gr8t thinker ndo maana upo humu ndani...1.As a man thinketh in his heart, so is he.... 2.Whether you think you can, or you think you can't--
you're right .
 

Hayo nimeyaeleza kwa kirefu katika kitabu changu 'Philosophy of Healing'. It is not automatic as day follows night that whatever occupies your mind will find a manifestation as condition in life. There exists a myriad of thoughts in the mind of an individual at any one time T and what really gains the day is the resultant thought of the said sample space. The individual components forming the myriad are vectorial in nature and the resultant is a summation of those individual components. Based on these facts it is not automatic that the idea picking your choice of business in which to engage is necessarily the resultant and when the resultant plays sway you are likely to crash land. Please find my book in this website Home
 
Depends.., majibu yote yanaweza yakawa sawa kulingana na opportunity cost (kwahio bila kujua value ya hio nyumba au biashara itakayofanywa ni vigumu kutoa jibu sahihi) pila inategemea na muda wa kumaliza the said project...

Kumbuka pia kwamba hata hiyo nyumba inaweza ikawa ni biashara au collateral
 
hahaha, umenikumbusha mbaali sana,
unakuta mtu/mfanyakazi anakopa pesa ananunua kiwanja, anaulipa kwa taabu sana kwenye makato ya mshahara wake,
anakuja tena anakopa anainua msingi, tena anailipa kwa suluba manake njia pekee ya kuulipa huo mkopo ni kukatwa mshahara wake, anakuja jenga nyumba na kukamilika lakini kwa muda mrefu sana na kwa suluba,

hapa bora angekopa akaanza na biashara, halafu biashara ndio ilipe mkopo , pia biashara ndiyo ijenge nyumba!

tatizo ni nini ? watu wengine waoga sana kujaribu biashara anafikiria nianze biashara halafu pesa/mtaji ukakata itakuwaje? unakuta hapa mtu hajawahi hata kugusa biashara ya aina yoyote au uwoga unamtawala. kwahiyo anaona bora akope anunue kiwanja, apandishe msingi, hadi kuezeka!

kwa mtu kama mimi ninayejiamini bora kwanza biashara, biashara ndiyo itanipa vyote, kama ni kuulipa mkopo ikiwa nimekopa, na itanipa nyumba pia.
 
hapo juu nimemzungumzia mtu anayepata pesa kidogo kidogo au mfano mfanyanyakazi,
lakini vilevile kama ni kwa mtu aliyepata pesa nyingi kwa mara moja, kama zinatosha anunue kiwanja cha bei chee na nyingine apeleke kwenye biashara, lakini kama hazitoshi kuzigawanya au wazo lake la biashara linahitaji pesa zote ni sawa tu aanze na biashara akipata zaidi atanunua tu kiwanja na kujenga nyumba.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…