Nyumba na. 81 Aggrey street Dar es salaam 1955

Nyumba na. 81 Aggrey street Dar es salaam 1955

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074


  1. R1yGBRkdmOsT18Riz-DWbDa6mw3WCuIhE40YFxhzq1OyBTuUnGnDm_1WecbXIcTjbn38scAjFe4=w1366-h768-rw-no

    Mzee Said na familia yake nje ya nyumba yake na. 81 Mtaa wa Aggrey
    Picha hii imepigwa 1955

    Picha hii kaniletea rafiki yangu toka utoto Juma Khube. Kaniambia kuwa huyo aliyesimama ni Mzee Said na mkewe (kulia) na katikati ni Shaban Sudi ambae alikuwa mfanyakazi wa bandari na amestaafu kazi mwaka 2015 na kulia kwake ni binti yake. Hapo ilipokuwa nyumba hii hivi sasa kuna ofisi ya CCM. Mimi na Juma sote tulipozaliwa hatukuikuta nyumba hii iliyokuwa Mtaa wa Aggrey. Jirani ya nyumba hii sisi tumekuta nyumba bora zaidi ya Mzee Maleta, nyumba ya Mzee Kleist na nyumba nyingine zilizokuwa katika hali nzuri kupita hii. Nyumba ya Mzee Khube ilikuwa hapo Aggrey na ilikuwa nyumba nzuri. Nyumba hii hivi sasa ni gorofa ndefu na inakabiliana na Msikiti wa Kiblatein moja ya misikiti maarufu ya Dar es Salaam. Waasisi wawili wa TANU Abdulwahid Sykes na Tewa Said Tewa walikuwa wanaishi mtaa huo majirani na si mbali na nyumba hii. Jirani na nyumba hii kwenye kona ya Mtaa wa Aggrey na Sikukuu sisi tulipozaliwa tulikuta jengo zuri la fahari kwa nyakati zile ambalo baadae ikajakuwa ofisi ya Tanganyika Federation of Labour (TFL). Ikitazamana na nyumba hii kwa pembeni kidogo ilikuwa nyumba ya mmoja wa bibi zangu Bi. Debora. Hii nyumba ipo hadi leo lakini imejengwa upya.

  2. aIE5dIOIkuor1LNM_HYsE8YFPSN2hY3BwHnjMbpbqyrBNT3ksijjx4EOEaU4AIO_BG3huVagp1lbCL3d0-Plrmga3X3hgD0jBhhcrF0TKaaWQO0Mn3uKh2WvjK7YC3Ymp8IKmGBvP10MGyCbUbo2X0QogdtRfnYy-mJEIHSrQhpk1g-9wu7L7P1SoumjyLJ6pbyLXF_I94R49Fbx3XbMD2PJ2HvhxvDj9JpDda5HjivRHDKG6vAfS1keU8x1jh31gLKf8E8CRPWEKAsmYHj8RFhPdmuHlczTbtInosBADP8AT4xl4FqX-W-H73cc6oVYX2unjI_LzP99DFv0fmhM_ADrN1RaWL80Fej7vKSj9r82JwSLuzFmG_mzwxMVhm-0BQdgxRgyieU8Uz-ZezwJhz6subkuHx-oT5Ak5GLyQPUhfS8oipcH4wm4VBsSNg7TbVBh189ZXawwGi9G3YUcnUc400alOcrt10faYzMYTP_brUEz8Jbt-Nh-GdkhcNmN4utiFhURFTTgZ328Z_qyd7GwrRpKlpQMoTEZ8V2UhSzMAISbULFZU_C6rfg3Feb8pyd-L7mJp_VqVzMjrYDXdZEYmYGpfwR8FI4XfKw6KwRDAJTO=w876-h657-no

    Mtaa wa Aggrey kama ulivyo hivi sasa angalia ghorofa zinazojengwa Kariakoo
    Picha imepigwa 2014

  3. R1yGBRkdmOsT18Riz-DWbDa6mw3WCuIhE40YFxhzq1OyBTuUnGnDm_1WecbXIcTjbn38scAjFe4=w1366-h768-rw-no


  4. Posted 11 minutes ago by Mohamed Said
    Labels: makala
Loading
 


  1. R1yGBRkdmOsT18Riz-DWbDa6mw3WCuIhE40YFxhzq1OyBTuUnGnDm_1WecbXIcTjbn38scAjFe4=w1366-h768-rw-no

    Mzee Said na familia yake nje ya nyumba yake na. 81 Mtaa wa Aggrey
    Picha hii imepigwa 1955

    Picha hii kaniletea rafiki yangu toka utoto Juma Khube. Kaniambia kuwa huyo aliyesimama ni Mzee Said na mkewe (kulia) na katikati ni Shaban Sudi ambae alikuwa mfanyakazi wa bandari na amestaafu kazi mwaka 2015 na kulia kwake ni binti yake. ....
Loading
Mzee acha kuongopa uzeeni. Haiwezekani huyo mtoto mwaka 1955 akawa na chini ya mwaka mmoja.
 
Kampelewele,
Hapana haja ya kunitusi.

Ikiwa umeona kuna kitu hakijaa sawa adabu ni kunifahamisha
kuwa,''Mbona Mzee hili halijakaa sawa na ukanieleza.''
Mheshimiwa unatakiwa ujue tofauti ya kutusi=kudanganya na neno la kiungwana kuongopa. hatujuani humu ndani, mimi kukuita mzee si kwamba mimi ni kijana.
 


  1. R1yGBRkdmOsT18Riz-DWbDa6mw3WCuIhE40YFxhzq1OyBTuUnGnDm_1WecbXIcTjbn38scAjFe4=w1366-h768-rw-no

    Mzee Said na familia yake nje ya nyumba yake na. 81 Mtaa wa Aggrey
    Picha hii imepigwa 1955

    Picha hii kaniletea rafiki yangu toka utoto Juma Khube. Kaniambia kuwa huyo aliyesimama ni Mzee Said na mkewe (kulia) na katikati ni Shaban Sudi ambae alikuwa mfanyakazi wa bandari na amestaafu kazi mwaka 2015 na kulia kwake ni binti yake. Hapo ilipokuwa nyumba hii hivi sasa kuna ofisi ya CCM. Mimi na Juma sote tulipozaliwa hatukuikuta nyumba hii iliyokuwa Mtaa wa Aggrey. Jirani ya nyumba hii sisi tumekuta nyumba bora zaidi ya Mzee Maleta, nyumba ya Mzee Kleist na nyumba nyingine zilizokuwa katika hali nzuri kupita hii. Nyumba ya Mzee Khube ilikuwa hapo Aggrey na ilikuwa nyumba nzuri. Nyumba hii hivi sasa ni gorofa ndefu na inakabiliana na Msikiti wa Kiblatein moja ya misikiti maarufu ya Dar es Salaam. Waasisi wawili wa TANU Abdulwahid Sykes na Tewa Said Tewa walikuwa wanaishi mtaa huo majirani na si mbali na nyumba hii. Jirani na nyumba hii kwenye kona ya Mtaa wa Aggrey na Sikukuu sisi tulipozaliwa tulikuta jengo zuri la fahari kwa nyakati zile ambalo baadae ikajakuwa ofisi ya Tanganyika Federation of Labour (TFL). Ikitazamana na nyumba hii kwa pembeni kidogo ilikuwa nyumba ya mmoja wa bibi zangu Bi. Debora. Hii nyumba ipo hadi leo lakini imejengwa upya.

  2. aIE5dIOIkuor1LNM_HYsE8YFPSN2hY3BwHnjMbpbqyrBNT3ksijjx4EOEaU4AIO_BG3huVagp1lbCL3d0-Plrmga3X3hgD0jBhhcrF0TKaaWQO0Mn3uKh2WvjK7YC3Ymp8IKmGBvP10MGyCbUbo2X0QogdtRfnYy-mJEIHSrQhpk1g-9wu7L7P1SoumjyLJ6pbyLXF_I94R49Fbx3XbMD2PJ2HvhxvDj9JpDda5HjivRHDKG6vAfS1keU8x1jh31gLKf8E8CRPWEKAsmYHj8RFhPdmuHlczTbtInosBADP8AT4xl4FqX-W-H73cc6oVYX2unjI_LzP99DFv0fmhM_ADrN1RaWL80Fej7vKSj9r82JwSLuzFmG_mzwxMVhm-0BQdgxRgyieU8Uz-ZezwJhz6subkuHx-oT5Ak5GLyQPUhfS8oipcH4wm4VBsSNg7TbVBh189ZXawwGi9G3YUcnUc400alOcrt10faYzMYTP_brUEz8Jbt-Nh-GdkhcNmN4utiFhURFTTgZ328Z_qyd7GwrRpKlpQMoTEZ8V2UhSzMAISbULFZU_C6rfg3Feb8pyd-L7mJp_VqVzMjrYDXdZEYmYGpfwR8FI4XfKw6KwRDAJTO=w876-h657-no

    Mtaa wa Aggrey kama ulivyo hivi sasa angalia ghorofa zinazojengwa Kariakoo
    Picha imepigwa 2014

  3. R1yGBRkdmOsT18Riz-DWbDa6mw3WCuIhE40YFxhzq1OyBTuUnGnDm_1WecbXIcTjbn38scAjFe4=w1366-h768-rw-no


  4. Posted 11 minutes ago by Mohamed Said
    Labels: makala
Loading
Sheikh Saidi umepunguza ladha kidogo kwa kuuita huo mtaa Aggrey. Haukuwa unaitwa Stanley????
 
Sheikh Saidi umepunguza ladha kidogo kwa kuuita huo mtaa Aggrey. Haukuwa unaitwa Stanley????
Abunuwasi,
Ahsante sana kwa kunizindua lakini kabla ya wewe kuniamsha hilo
nililigundua na nikafanya masahihisho.

Ingia upya utaona nimesahihisha.

Hakika ni Stanley Street na kulikuwa na Kirk Street ambao sasa ni
Mtaa wa Lindi.
 
Kampelewele,
Hapana haja ya kunitusi.

Ikiwa umeona kuna kitu hakijaa sawa adabu ni kunifahamisha
kuwa,''Mbona Mzee hili halijakaa sawa na ukanieleza.''
Achana naye huyo,katika kamusi yake neno.... MZEE,halipo,utajipa stress bure,ushindwe kusimama usiku kufanya ibada.
 
Achana naye huyo,katika kamusi yake neno.... MZEE,halipo,utajipa stress bure,ushindwe kusimama usiku kufanya ibada.
Isambe,
Ahsante ndugu yangu.

Nimeshangazwa na ile chuki katika kauli zake.
Nimejiuliza kipi kimemghadhibisha huyu ndugu yangu?

Yawezekana katika ile ''post,'' lipo kosa nami sikuliona.

Ikiwa hivyo ndivyo ilikuwa yeye kunielekeza basi nami
nitoe jibu.

Lakini anakuja na ghadhabu na matusi pasi na sababu.
 
Hongera sana bwana Mohamed Said,Wallah historia inamanufaa mno,nikiona habari kama hizi natamani ningekua ndo kijana wa miaka hiyo enzi Dar es salaam ilivyokua mahala pa ustaarabu.
Othiambo,
Hakika nyakati zile wazee wakituhimiza sana kuhusu adabu.
Walikuwa na neno lao wakituasa,''Usitutukanishe.''

Maana ikiwa mtoto atakosa adabu watu watajua mama yake
hakumfunza adabu na hili kwao lilikuwa tusi kubwa.

Ustaarabu bado ungalipo ni wajibu wetu kuwafunza wanetu
na hata hapa barzani ikiwa unahisi mtu hakupata malezi kwao
kwa njia ya utaratibu unamuelekeza kuwa huenda huko kwenu
si vibaya lakini haifai kufanya kadha wa kadha kwenye kadamnasi.
 
Shukrani. Nimepitia.
Slim5,
Ahsante sana.

Kulikuwa na somo yako hapa Dar anaitwa Slim.
Alikuwa mtu wa mikasa kweli kweli.

In Shaallah iko siku nitaleta visa vyake hapa barzani.

Kama Dar ya 1970 kulikuwa na wajanja 10 na yeye
namba yake imo humo tena nafasi za matawini.
 
Asante sana kwa Historia iliyotukuka Mzee wetu. Tunaomba uendelee kuiweka humu kwa manufaa ya vizazi vijavyo. Asante sana.
 
Back
Top Bottom