Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
NYUMBA ZILIZOKUWAKO DAR ES SALAAM YA 1950s
Hapo chini ni mfano wa nyumba nyingi zilizokuwapo Dar-es-Salaam miaka ya 1950.
Nyumba hizi zilikuwa na vyumba sita vyumba vitatu kila upande vikiangaliana na katikati kulikuwa na ukumbi mrefu.
Uani kulikuwa na mabanda madogo jiko, vyoo na bafu.
Nyumba nyingi zilikuwa na karo ambalo lilitumika kama mahali pa kuoshea vyombo au kufua nguo.
Nyingi ya nyumba hizi zilikuwa za kupangisha kwa hiyo utakuta nyumba moja ikikaliwa na familia tofauti.
Baadhi ya nyumba zilikuwa na baraza mbele kwa ajili ya wakazi kukaa na kupumzika hasa wanaume mfano wa hiyo nyumba picha ya pili.
Wanawake kwa kawaida wao wakipumzika uani au ukumbini.
Nyumba hizi zimetoweka Kariakoo lakini nimebahatika kuziona nyumba hizi Magomeni Mapipa.
Hapo chini ni mfano wa nyumba nyingi zilizokuwapo Dar-es-Salaam miaka ya 1950.
Nyumba hizi zilikuwa na vyumba sita vyumba vitatu kila upande vikiangaliana na katikati kulikuwa na ukumbi mrefu.
Uani kulikuwa na mabanda madogo jiko, vyoo na bafu.
Nyumba nyingi zilikuwa na karo ambalo lilitumika kama mahali pa kuoshea vyombo au kufua nguo.
Nyingi ya nyumba hizi zilikuwa za kupangisha kwa hiyo utakuta nyumba moja ikikaliwa na familia tofauti.
Baadhi ya nyumba zilikuwa na baraza mbele kwa ajili ya wakazi kukaa na kupumzika hasa wanaume mfano wa hiyo nyumba picha ya pili.
Wanawake kwa kawaida wao wakipumzika uani au ukumbini.
Nyumba hizi zimetoweka Kariakoo lakini nimebahatika kuziona nyumba hizi Magomeni Mapipa.