Nyuzi kuachia au kutokushonwa vizuri

Nyuzi kuachia au kutokushonwa vizuri

MadamG

Senior Member
Joined
Feb 1, 2013
Posts
125
Reaction score
47
NESI ALIENIANGALIA ANASEMA SIJASHONWA VIZURI KWA NDANI NA NJE

Nimejifungua kwa njia ya kawaida na niliongezewa njia mtoto wa kwanza.

je ni tatizo kubwa sana la kupelekwa thieter na kupigwa nusu kaputi?, maana naogopa sana je hawatanishona kama mara ya kwanza nilivyoshonwa nilivojifungua?

Nimejifungulia hosp kubwa ya serikali Iringa naogopa sana au kuna njia nyingine ya sehemu za siri kurudi katika hali yake yaani sehemu ambayo haikushonwa kujifunga?
 
swali langu ninaweza kushonwa kama nilivyoshonwa baada ya kujifungua? na nitaweza kurudi hali yangu kama ya zamani wakati sijajifungua?
maana wananiogopesha kuwa naenda kufanyiwa oparesheni
 
Yangu ni pole tu, mengine wasubiri madaktari wa hapa
 
Nnavojua mie utashonwa km mwanzo, lkn ukubali maumivu makali mana ngozi itakua ishafaya ugumu so kuvutika inakua shughuli tofauti na pale mwanzo ambapo bado inakua laini.

Ila vovote itavokua bora ufanye hio repair mapema ili usije pata matatizo makubwa zaidi.

Pole sana, hope utarudi kwenye hali yako ya uzima kama kawaida
 
swali langu ninaweza kushonwa kama nilivyoshonwa baada ya kujifungua? na nitaweza kurudi hali yangu kama ya zamani wakati sijajifungua?
maana wananiogopesha kuwa naenda kufanyiwa oparesheni

Nimekuelewa, kwahiyo ulipojifunguwa walikuongezea njia kidogo na wakakushona tena ila hukushonwa vizuri hivyo bilashaka una kidonda. Nenda hospitali kubwa watakushona vizuri tena na lazima watakuchoma sindano ya ganzi hawawezi kukushona hivi hivi utalia sana, sasa ni nusu kaputi au ganzi ya kawaida tu watakuambia hapo hapo hospitali kutegemea na watakavyokuona. Kupona hivi hivi bila kushonwa tena inawezekana pia kutegemea kidonda chenyewe kilivyo.
 
Back
Top Bottom