Nywele zinavyohusishwa na roho na mapepo

Nywele zinavyohusishwa na roho na mapepo

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
301,577
Reaction score
754,412
Kuna mambo ya kushangaza ambayo kwasababu ileile ya kimapokeo na mazoea huwa hatuyahoji au hatuna muda wa kufuatilia na pengine tunaridhika tu na hivyo yalivyo.

Nywele hizi zetu za kichwani zinabeba siri kubwa ambayo ina mawasiliano ya moja kwa moja na kuzimu au na roho zinazotangatanga.

Hebu tujihoji haya;

- Kwanini baadhi ya imani ni marufuku na hairuhusiwi kwa mwanamke kuonyesha nywele zake hadharani?
- Kwanini mchawi/mwanga anapokamatwa hukatwa nywele zote ili kummaliza nguvu zake?
- Kwanini chizi kichaa au mwendawazimu hunyolewa nywele kama sehemu ya tiba?
- Kwanini wachawi na waganga wengi hutumia nywele kama sehemu ya uchawi/ulozi wao?

Historia ya nywele kuhusiana na roho na nguvu za kiza inaanzia mbali sana miaka elfu nyingi iliyopita kwenye habari za Biblia takatifu kisa cha Samsoni na Delilah pale Mwenyezi Mungu alipoweka nguvu isiyomithilika kwenye nywele za Samsoni lakini shetani kupitia Delilah alimrubuni Samsoni na Samsoni akatoa siri ya nguvu zake.

Ni kutoka hapo ile nguvu ya kimungu iliyowekwa kwenye nywele za Samsoni iligeuka na kuwa nguvu ya kishetani na kufanya maangamizi makubwa, tangu hapo nywele imekuwa ni kitu kinachohusishwa na roho chafu na mapepo.

 
Sasa naanza kufikiria ,maana kuna ibada moja ya wahindi na baadhi ya sehem nyingi za Asia. Hunyoa nywele kama sadaka kwa Miungu yao. Hebu tuendeleee mshana jr then nitatoa mchango wangu juu ya hili……

Chuo nilichosoma mimi hatukuruhusiwa kufuga nywele na tulikuwa tunanyoa kwa mwezi mara mbili na ilikuwa imo kwenye ratiba ya chuo na haikuwezekana usinyoe unaweza hata kufukuzwa chuo ukikaidi
 
Last edited by a moderator:
Chuo nilichosoma mimi hatukuruhusiwa kufuga nywele na tulikuwa tunanyoa kwa mwezi mara mbili na ilikuwa imo kwenye ratiba ya chuo na haikuwezekana usinyoe unaweza hata kufukuzwa chuo ukikaidi

Kuna hatari gani unazoweza kutana nazo unapoa tupa ovyo nyewele zako, au kunyolewa salun na kuziach…?
 
Huyu mshana jr ana tatizo........basi itabidi tunyoe nywele zote maana atakuja na story ya Brazilian wigs na weaves zina majini...................
Preta kuvaa hayo madude ni kukosoa Muumba wako, kwa macho ya kawaida ni urembo lakini ndani yake ni kichaka cha mapepo, yani ni sawa na kutengeneza makazi ya hayo madudu bila kujijua
 
Last edited by a moderator:
Ndomaana nivizuri baada ya kunyoa nywele uzichimbie na kuzifukia, ila kabla unatakiwa uangalie kushoto na kulia kama kuna anaye kuona. Kama hayupo fukia kisha sepa!!

Kuna hatari gani unazoweza kutana nazo unapoa tupa ovyo nyewele zako, au kunyolewa salun na kuziach…?

Kama unashika dini hakuna shida lakini ukiwa na hizi imani zetu ni rahisi mno wachawi na wanga kuzibeba kama malighafi ya kufanya mambo yao
 
Preta kuvaa hayo madude ni kukosoa Muumba wako, kwa macho ya kawaida ni urembo lakini ndani yake ni kichaka cha mapepo, yani ni sawa na kutengeneza makazi ya hayo madudu bila kujijua

Sasa nifanyeje......?......maana nikinyoa nitafanana na shemeji yako halafu tutakukomfyuzi........twende kilioni nilisuka praimare..........inatosha..........
 
Chuo nilichosoma mimi hatukuruhusiwa kufuga nywele na tulikuwa tunanyoa kwa mwezi mara mbili na ilikuwa imo kwenye ratiba ya chuo na haikuwezekana usinyoe unaweza hata kufukuzwa chuo ukikaidi

Hiyo inategemeana na Chuo kinahusiana na nini?,mfano tulipokuwa sekondari walitukataza kufuga nywele na ndevu,sasa je nako ni ushirikina?,Ukienda Polisi na majeshi mengine nywele hairuhusiwi kufuga je nako ni ushirikina?,Ipo cku mtawahusisha watu wanaopenda kunyoa nywele zao mara kwa mara na ushirikina wakati ndiyo ustaarabu wao uko hivyo.
 
Back
Top Bottom