OCD Gairo amempatia Shabiby walinzi katika zoezi la kugawa rushwa

OCD Gairo amempatia Shabiby walinzi katika zoezi la kugawa rushwa

T2020

Senior Member
Joined
Jul 15, 2020
Posts
158
Reaction score
361
Wakati wajumbe wakianza kuingia mjini Gairo kwa ajili ya kupiga kura ya maoni kwa waliojaza na kurudisha fomu, mbunge aliyemaliza muda wake Mhe. Shabiby anakabiliwa na wagombea wengine zaidi ya 20. Juzi baada ya kikao cha wagombea wake, amesambaza pesa kupitia kwa wagombea udiwani waliomaliza muda wake wanaoomba tena muhula huu wa pili.

Jana tarehe 18/07/2020 mpambe wàke akiwa na askari walikuwa wakiita wajumbe ili kugawa pesa. Amelazimika kushirikiana na polisi ili kukwepa madiwani hao kukamatwa na polisi. Pili, ni uhakika wa wagawa pesa hao kufikisha pesa kwa wapiga kura. Shabiby ambaye ana mahusiano mabaya na watumishi wa Gairo hasa DC wa hapa amekuwa akikodi wahuni kumtukana DC Huyo na kisha kutoroka.

Mmoja wa wahuni hao ni kaka yake ajulikanae kwa jina la Salehe ambaye kwa sasa ametoroka na kila akitaka kukamatwa OCD amekuwa akimsaidia kutoroka. Katika kikao cha juzi cha wagombea wrote mmoja wa wagombe niliyepata jina moja tu la Omary alilazimika kutolewa nje ya kikao baada ya kumtuhumu mwenyekiti ya wilaya hiyo wa CCM kuwa amekuwa akimpendelea na kumfanyia Shabiby kampeni kama sehemu ya kulipa fadhila baada ya kununuliwa gari aina ya Verossa na mfanyabiashara huyu maarufu wa mabasi, vituo vya mafuta na nyumba za kisasa za kulala wageni.
 
Kwani Rushwa ipo hadi CCM ya JPM?

watatumbuliwa wote aisee kama ni kweli
 
Hivi ndugu kwanini usipige simu TAKUKURU hapo hapo kabla ya kuchukua muda mrefu kuandika huu uzi hapa??
 
Safari hii ameshindwa kupandikiza wagombea wake ili baadaye wajitoe. Nasikia kuna dogo aliyeenda shule mhadhiri wa UDOM miaka ya nyuma alikuwa ananunuliwa ili asigombee. Dogo safari hii kakomaa amekataa kujitoa. Wakazi wa Gairo wanapasha iwe jua iwe mvua Shabiby chali asubuhi tu kesho.
 
Unajua maana ya jamii forum na kazi yake? Kwa comment yako naona wewe hapa ulipotea njia
Hivi ndugu kwanini usipige simu TAKUKURU hapo hapo kabla ya kuchukua muda mrefu kuandika huu uzi hapa??
 
Safari hii ameshindwa kupandikiza wagombea wake ili baadaye wajitoe. Nasikia kuna dogo aliyeenda shule mhadhiri wa UDOM miaka ya nyuma alikuwa ananunuliwa ili asigombee. Dogo safari hii kakomaa amekataa kujitoa. Wakazi wa Gairo wanapasha iwe jua iwe mvua Shabiby chali asubuhi tu kesho.
Huyo Shabiby yupo karibu sana na Madelu hivyo anajiamini sana
 
Safari hii ameshindwa kupandikiza wagombea wake ili baadaye wajitoe. Nasikia kuna dogo aliyeenda shule mhadhiri wa UDOM miaka ya nyuma alikuwa ananunuliwa ili asigombee. Dogo safari hii kakomaa amekataa kujitoa. Wakazi wa Gairo wanapasha iwe jua iwe mvua Shabiby chali asubuhi tu kesho.
Dogo akitengewa 100kk atachomoa kweli maisha yalivyo magumu hivi?
 
Huyu shabiby nae inatosha ss,wawaachie wengine!

JESUS IS LORD[emoji120]
 
Gairo Ni nyumbani, ccm rushwa Ni kawaida kwao, Ahmed miaka yote anapita kwa mlungula...hao wengine watatulizwa tu. SEMA labda awamu hii itamchomoa maana Jiwe Sina hakika Kama ana uhusiano nzuri na Ahmed(Shabiby). Jina likipita tu Ahmed anarudi bungeni. wakaguru nawaelewa wale watu.Ni Ile jamii ya kumpigia magoti mwenye nacho .
 
Back
Top Bottom