Ofisa feki wa TAKUKURU akamatwa

Ofisa feki wa TAKUKURU akamatwa

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), mkoa wa Ilala Dar es Salaam, inamshikilia Hussein Hassani (43), kwa kosa la kujifanya Ofisa wa Takukuru na kutapeli wananchi.

Mbali na kujifanya Ofisa wa Takukuru, Hassani ambaye ni mkazi wa Mbagala jijini Dar es Salaam, pia alighushi kitambulisho namba PCCB 1565 chenye jina la Hussein Mhando, cheo cha Ofisa Uchunguzi Mkuu wa Takukuru.

Akizungumza na waandishi Mkuu wa Takukuru Ilala, Christopher Myava, alisema baada ya kughushi kitambulisho Mtuhumiwa alitapeli watu mbalimbali na kujipatia kipato kinyume na sheria.

Myava ameeleza kuwa baada ya kupata taarifa kutoka kwa raia wema kuhusu utapeli huo, waliweka mtego Desemba 12 maeneo ya Pachoto Mwananyamala.

"Tuliweka mtego maeneo hayo lakini kwa bahati mbaya alikimbia na kuacha gari baada ya kuona watu asiowafahamu ambao walikuwa karibu na gari namba T618DMS ambalo alikuwa analitumia," alisema.

Mkuu huyo ameongeza kuwa baada ya mtuhumiwa huyo kukimbia na kuacha gari Takukuru ilifanikiwa kulishikilia na Desemba 16 mtuhumiwa alijisalimisha na kukiri kujifanya Ofisa wa Takukuru na kutapeli wananchi.

Aidha mtuhumiwa huyo alikiri kuchana kitambulisho alichoghushi kwa nia ya kupoteza ushahidi baada ya kuwakimbia maofisa wa Takukuru.

"Wakati tunafanya uchunguzi wa mtuhumiwa huyo kabla ya kumkamata tayari kitambulisho tulikuwa tumeshakitoa kopi," alisema.

1576751595996.png
 
Kwaiyo huyo bwana Hassan ndio huyo aliesimama pembeni kwa mheshimiwa,amevaa open shoes huku ametia mikono mfukon
 
Matapeli wanakera sana, Kuna wakati mwananchi anaweza shindwa kuitikia wito halali kwa sababu ashazoea simu za matapeli

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mmoja walimkamata huko Arusha wakadai ni tiss fake, sasa ni dc!!


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
kuna siku nikiwa mwanza baada ya kupata kilaji niliji tambulisha kwa wanyantuzu makota wa dhahabu kama mtu wa 'usalama' kwa kweli siku hiyo nikula 'shushu' za hatari ila sikuwa na amani kabisa, kulipo pambazuka asubuhi nikaji apiza sitorudia tena huo ujinga!
 
beth,
Mnaweka picha zenu ili iweje, mnajua hasara ya kuweka picha zenu na hasa ninyi watu wa usalama?
 
Kuna mmoja walimkamata huko Arusha wakadai ni tiss fake, sasa ni dc!!


Sent from my iPhone using JamiiForums


Labda huwa wanacheza maigizo kwa lengo la kuuonyesha umma kuwa chombo kinafanya kazi
 
Halafu dume zima na nguvu .

Ingekuwa mijitu kama hii inafiliswa pamoja na viboko 10 live kwenye TV ili dunia iwatambue.

Hovyo sana makima haya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Atakuwa kuna mtu anampatiaga details A,B,C.....wajifanye wanamwachia alafu waendelee kumchunguza uenda kuna kitu behind the carpet.
Haiwezekani mtu from no where kujifanya mtu fulani pasipo kuwa na ukaribu na mmojawapo ya wahusika.
 
Labda huwa wanacheza maigizo kwa lengo la kuuonyesha umma kuwa chombo kinafanya kazi

...jiulize huyo jamaa alijuaje id za takukuru zilivyo, na namna ya uwekaji wa namba n.k!
Kuna sehemu jamaa kakosea/wamekosea hivyo ikabidi lichezwe sebene hapo!
Afuatiliwe then jumapili tusipokutana nae forty forty...


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom