Ofisa mstaafu wa Polisi adai kubambikiwa kesi

Ofisa mstaafu wa Polisi adai kubambikiwa kesi

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Aliyekuwa Mkuu wa Polisi (OCD), wa Wilaya ya Siha, Vicent Lyimo amemwandikia barua Rais Samia Suluhu Hassan, akimuomba aingilie kati suala lake ili Jeshi la Polisi limpatie nakala ya hukumu na mwenendo wa kesi ya kijeshi iliyomshusha cheo.

Lyimo anadai mwaka 2016, alifunguliwa mashtaka katika Mahakama ya kijeshi, akituhumiwa kuwaachia watuhumiwa watatu wa mauaji, mashtaka anayodai kuwa alibambikiwa, kwa sababu waliachiwa na mkuu wa upelelezi (OC-CID).

Kwa mujibu wa ofisa huyo, shauri hilo liliendeshwa kwa miaka minne (2016-2019), na Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Polisi (SACP), Yusuph Ilembo na kutiwa hatiani kwa kosa hilo na kushushwa cheo kutoka Mrakibu wa Polisi (SP) hadi Mkaguzi wa Polisi na kuamriwa kustaafu kwa lazima.

“Niliposhushwa kuwa Inspector (Mkaguzi) nilikuwa na miaka 56, wakadai umri wa kustaafu kwa cheo cha Inspector ni miaka 55. Ila walijichanganya kwa sababu PGO (kanuni za Polisi) zinasema ukikata rufaa hukumu na adhabu zinasitishwa kusubiri maamuzi ya rufaa. Hawakupaswa kuniamuru kustaafu wakati rufaa ilikuwa haijajibiwa. Nafikiri hili kosa ndio maana hawataki kunipa hizo nyaraka.

“Kuninyima nakala halisi za hukumu, mwenendo wa kesi na rufaa ni sawa na kunifunga nyuma mikono nishindwe kufanya chochote mbele ya sheria,” alisisitiza ofisa huyo wa zamani aliyehudumu wilayani Siha mkoani Kilimanjaro alipokuwa akizungumza na Mwananchi jana.

Alisema kama walimshtaki na kumtia hatia kwa haki kwa nini wanasita kumpa nakala hizo? Bila hizo hata nikienda mahakamani au mbele ya chombo kingine chochote cha haki, nitakuwa najisumbua maana huo ndio ushahidi muhimu.

Akijibu swali ni kwa nini anahisi alitengenezewa au kubambikiwa kesi, Lyimo alidai kuwa alikuwa haelewani na mmoja wa viongozi wake na ndiye alitumia madaraka yake kumtengenezea kesi na kunyimwa nyaraka ni mwendelezo huo.

Barua aliyomwandikia Rais

Ofisa huyo alisema alimwandikia Rais barua ya kwanza Desemba 12,2022 na akaandika nyingine ya kukumbushia Januari 13,2023 na sasa ameandika nyingine Februari 9,2023 akimuomba aingilie kati apewe nyaraka.

Katika barua hiyo, amemweleza Rais kuwa; “Hata rufaa yake ilicheleweshwa miaka mitatu tangu mwaka 2019 hadi 2021, bila sababu za msingi na sikupatiwa nakala ya rufaa wala sababu za kukataliwa rufaa yangu kinyume cha sheria na Katiba.”

“Hayo yote ni ishara tosha kwamba nilibambikiwa kesi. Pia nimenyimwa haki yangu ya msingi ya kisheria, kikanuni na kikatiba kubisha hodi mahakamani”alisema.

Akifafanua zaidi kuhusu barua hiyo, Lyimo alidai aliwahi kufungua maombi Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Moshi, lakini yalitupwa kutokana na kukosekana kwa nyaraka halisi ya hukumu na mwenendo wa kesi.

Vigogo wa polisi wafunguka

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa akizungumza na gazeti hili kuhusu suala hilo, alisema kuwa hawezi kulizungumzia badala yake atafutwe msemaji wa jeshi hilo.

Kwa upande wake, msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, David Misime alipoulizwa na Mwananchi jana kama analifahamu jambo hilo, hakukanusha wala kuthibitisha zaidi ya kumtaka ofisa huyo afuate utaratibu wa ndani ya jeshi kudai haki yake.

“Kama anaona alionewa afuate utaratibu zilizopo. Kama kweli alikuwa ni askari aliyeiva na mwenye maadili ya kijeshi,” alisema Misime.

MWANANCHI
 
Kumbe nao wanabambikiana kesi? Hakuna kitu kibaya kama kumbambikia mwengine kesi ni uonevu wa hali ya juu. Nilisikitika siku ile mama akisema baadhi ya polisi wanawawekea watu madawa ya kulevya na kuwabambikia kesi.

Labda na huyu wakati wa utumishi wake alioneaga watu. Na kama ni hivyo Mangi atulie tuu karma ifanye kazi yake.

Polisi muadilifu pekee Tanzania ni Malisa Arusha.

wa kupuliza
 
Ila huyu msemaji wa polisi ana majibu fulani ya kihuni/kiswahili sana, ukitazama ile taarifa yake kwa umma kuhusu kutania polisi aliandika so unprofessional

Leo pia anatoa majibu mkato/ya kiswahili, mwenzie anadai kupitia taratibu za polisi amenyimwa haki,msemaji anajibu shombo
 
Hawa watu wabaya sana,polisi hahitaji huruma ya jamii hata kidogo,ukikutana na polisi anachotaka na kudhani juu yako ni namna ipi atumie ili apate pesa toka kwako.

Huyo apambane na Hali yake,naamini Hadi anafanyiwa haya na yeye kuna watu amewahi kuwaumiza kwa namna yoyote iwayo!!

Kaa kwa kutulia wewe polisi
 
Aliyekuwa Mkuu wa Polisi (OCD), wa Wilaya ya Siha, Vicent Lyimo amemwandikia barua Rais Samia Suluhu Hassan, akimuomba aingilie kati suala lake ili Jeshi la Polisi limpatie nakala ya hukumu na mwenendo wa kesi ya kijeshi iliyomshusha cheo.

Lyimo anadai mwaka 2016, alifunguliwa mashtaka katika Mahakama ya kijeshi, akituhumiwa kuwaachia watuhumiwa watatu wa mauaji, mashtaka anayodai kuwa alibambikiwa, kwa sababu waliachiwa na mkuu wa upelelezi (OC-CID).

Kwa mujibu wa ofisa huyo, shauri hilo liliendeshwa kwa miaka minne (2016-2019), na Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Polisi (SACP), Yusuph Ilembo na kutiwa hatiani kwa kosa hilo na kushushwa cheo kutoka Mrakibu wa Polisi (SP) hadi Mkaguzi wa Polisi na kuamriwa kustaafu kwa lazima.

“Niliposhushwa kuwa Inspector (Mkaguzi) nilikuwa na miaka 56, wakadai umri wa kustaafu kwa cheo cha Inspector ni miaka 55. Ila walijichanganya kwa sababu PGO (kanuni za Polisi) zinasema ukikata rufaa hukumu na adhabu zinasitishwa kusubiri maamuzi ya rufaa. Hawakupaswa kuniamuru kustaafu wakati rufaa ilikuwa haijajibiwa. Nafikiri hili kosa ndio maana hawataki kunipa hizo nyaraka.

“Kuninyima nakala halisi za hukumu, mwenendo wa kesi na rufaa ni sawa na kunifunga nyuma mikono nishindwe kufanya chochote mbele ya sheria,” alisisitiza ofisa huyo wa zamani aliyehudumu wilayani Siha mkoani Kilimanjaro alipokuwa akizungumza na Mwananchi jana.

Alisema kama walimshtaki na kumtia hatia kwa haki kwa nini wanasita kumpa nakala hizo? Bila hizo hata nikienda mahakamani au mbele ya chombo kingine chochote cha haki, nitakuwa najisumbua maana huo ndio ushahidi muhimu.

Akijibu swali ni kwa nini anahisi alitengenezewa au kubambikiwa kesi, Lyimo alidai kuwa alikuwa haelewani na mmoja wa viongozi wake na ndiye alitumia madaraka yake kumtengenezea kesi na kunyimwa nyaraka ni mwendelezo huo.

Barua aliyomwandikia Rais

Ofisa huyo alisema alimwandikia Rais barua ya kwanza Desemba 12,2022 na akaandika nyingine ya kukumbushia Januari 13,2023 na sasa ameandika nyingine Februari 9,2023 akimuomba aingilie kati apewe nyaraka.

Katika barua hiyo, amemweleza Rais kuwa; “Hata rufaa yake ilicheleweshwa miaka mitatu tangu mwaka 2019 hadi 2021, bila sababu za msingi na sikupatiwa nakala ya rufaa wala sababu za kukataliwa rufaa yangu kinyume cha sheria na Katiba.”

“Hayo yote ni ishara tosha kwamba nilibambikiwa kesi. Pia nimenyimwa haki yangu ya msingi ya kisheria, kikanuni na kikatiba kubisha hodi mahakamani”alisema.

Akifafanua zaidi kuhusu barua hiyo, Lyimo alidai aliwahi kufungua maombi Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Moshi, lakini yalitupwa kutokana na kukosekana kwa nyaraka halisi ya hukumu na mwenendo wa kesi.

Vigogo wa polisi wafunguka

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa akizungumza na gazeti hili kuhusu suala hilo, alisema kuwa hawezi kulizungumzia badala yake atafutwe msemaji wa jeshi hilo.

Kwa upande wake, msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, David Misime alipoulizwa na Mwananchi jana kama analifahamu jambo hilo, hakukanusha wala kuthibitisha zaidi ya kumtaka ofisa huyo afuate utaratibu wa ndani ya jeshi kudai haki yake.

“Kama anaona alionewa afuate utaratibu zilizopo. Kama kweli alikuwa ni askari aliyeiva na mwenye maadili ya kijeshi,” alisema Misime.

MWANANCHI
Karma katika ubora wake!
 
Mbona wao ndi mabingwa wa kubambikia wenzao. Ss na wao kwa wao pia imo mpk kieleweke
 
Chura ukimpiga teke unamuongezea mwendo. Badala ya kulia lia hapa, angetumia ujuzi alionao kufungua kampuni ya ulinzi, angekuwa mbali...
 
Aliyekuwa Mkuu wa Polisi (OCD), wa Wilaya ya Siha, Vicent Lyimo amemwandikia barua Rais Samia Suluhu Hassan, akimuomba aingilie kati suala lake ili Jeshi la Polisi limpatie nakala ya hukumu na mwenendo wa kesi ya kijeshi iliyomshusha cheo.

Lyimo anadai mwaka 2016, alifunguliwa mashtaka katika Mahakama ya kijeshi, akituhumiwa kuwaachia watuhumiwa watatu wa mauaji, mashtaka anayodai kuwa alibambikiwa, kwa sababu waliachiwa na mkuu wa upelelezi (OC-CID).

Kwa mujibu wa ofisa huyo, shauri hilo liliendeshwa kwa miaka minne (2016-2019), na Kamishna Mwandamizi Msaidizi wa Polisi (SACP), Yusuph Ilembo na kutiwa hatiani kwa kosa hilo na kushushwa cheo kutoka Mrakibu wa Polisi (SP) hadi Mkaguzi wa Polisi na kuamriwa kustaafu kwa lazima.

“Niliposhushwa kuwa Inspector (Mkaguzi) nilikuwa na miaka 56, wakadai umri wa kustaafu kwa cheo cha Inspector ni miaka 55. Ila walijichanganya kwa sababu PGO (kanuni za Polisi) zinasema ukikata rufaa hukumu na adhabu zinasitishwa kusubiri maamuzi ya rufaa. Hawakupaswa kuniamuru kustaafu wakati rufaa ilikuwa haijajibiwa. Nafikiri hili kosa ndio maana hawataki kunipa hizo nyaraka.

“Kuninyima nakala halisi za hukumu, mwenendo wa kesi na rufaa ni sawa na kunifunga nyuma mikono nishindwe kufanya chochote mbele ya sheria,” alisisitiza ofisa huyo wa zamani aliyehudumu wilayani Siha mkoani Kilimanjaro alipokuwa akizungumza na Mwananchi jana.

Alisema kama walimshtaki na kumtia hatia kwa haki kwa nini wanasita kumpa nakala hizo? Bila hizo hata nikienda mahakamani au mbele ya chombo kingine chochote cha haki, nitakuwa najisumbua maana huo ndio ushahidi muhimu.

Akijibu swali ni kwa nini anahisi alitengenezewa au kubambikiwa kesi, Lyimo alidai kuwa alikuwa haelewani na mmoja wa viongozi wake na ndiye alitumia madaraka yake kumtengenezea kesi na kunyimwa nyaraka ni mwendelezo huo.

Barua aliyomwandikia Rais

Ofisa huyo alisema alimwandikia Rais barua ya kwanza Desemba 12,2022 na akaandika nyingine ya kukumbushia Januari 13,2023 na sasa ameandika nyingine Februari 9,2023 akimuomba aingilie kati apewe nyaraka.

Katika barua hiyo, amemweleza Rais kuwa; “Hata rufaa yake ilicheleweshwa miaka mitatu tangu mwaka 2019 hadi 2021, bila sababu za msingi na sikupatiwa nakala ya rufaa wala sababu za kukataliwa rufaa yangu kinyume cha sheria na Katiba.”

“Hayo yote ni ishara tosha kwamba nilibambikiwa kesi. Pia nimenyimwa haki yangu ya msingi ya kisheria, kikanuni na kikatiba kubisha hodi mahakamani”alisema.

Akifafanua zaidi kuhusu barua hiyo, Lyimo alidai aliwahi kufungua maombi Mahakama Kuu ya Tanzania kanda ya Moshi, lakini yalitupwa kutokana na kukosekana kwa nyaraka halisi ya hukumu na mwenendo wa kesi.

Vigogo wa polisi wafunguka

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa akizungumza na gazeti hili kuhusu suala hilo, alisema kuwa hawezi kulizungumzia badala yake atafutwe msemaji wa jeshi hilo.

Kwa upande wake, msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, David Misime alipoulizwa na Mwananchi jana kama analifahamu jambo hilo, hakukanusha wala kuthibitisha zaidi ya kumtaka ofisa huyo afuate utaratibu wa ndani ya jeshi kudai haki yake.

“Kama anaona alionewa afuate utaratibu zilizopo. Kama kweli alikuwa ni askari aliyeiva na mwenye maadili ya kijeshi,” alisema Misime.

MWANANCHI
wewe umesahau ulivio kuwa unawabambikizia kesi tena ufungwa
 
Ila huyu msemaji wa polisi ana majibu fulani ya kihuni/kiswahili sana, ukitazama ile taarifa yake kwa umma kuhusu kutania polisi aliandika so unprofessional

Leo pia anatoa majibu mkato/ya kiswahili, mwenzie anadai kupitia taratibu za polisi amenyimwa haki,msemaji anajibu shombo
Mara nyingi anakurupuka sana kujibu mambo ya mitaani.

Kama mtu amenyimwa haki yake ni Vema akasikikizwa badala ya kumjibu kirahisi TU.

Mlalamikaji anasema kuwa amefuata taratibu zote kuomba nakala ya hukumu lakini amenyimwa Sasa wanataka afanyeje kama sio kuomba Kwa mh.Rais ambaye ni Amiri Jeshi mkuu.

Jeshi la Polisi linatakiwa lifanyiwe marejehusho makubwa sana. Liondokane na ukoloni mana linahudumia wananchi.
Chombo kikiwa kinaendeshwa Kijeshi Hakiwezi kuwahudumia wananchi Kwa wema mana Kuna wakati kitatumia mabavu kuficha madhaifu ya watendaji wake.

Tatizo la Polisi ni kutumia mabavu kuficha madhaifu yake badala ya kufuata taratibu za kisheria. Mtu ameshastaafu na Sasa ni raia ,Kwa nini anamlazimishwa kufuata taratibu za Kijeshi wakati Kwa Sasa ni Raia na Hana amri Kwa askari hata wanaokaa kwenye ofisi za kutoa hizo nakala?

Yeye ni raia na Kwa cheo chake alichostaafu nacho hawezi kumwamuru askari yeyote kijeshi Sasa hizo taratibu za Kijeshi nazotakiwa ni zipi zaidi ya hizo alizofuata na kunyimwa nakala?
 
Hawa watu wabaya sana,polisi hahitaji huruma ya jamii hata kidogo,ukikutana na polisi anachotaka na kudhani juu yako ni namna ipi atumie ili apate pesa toka kwako.

Huyo apambane na Hali yake,naamini Hadi anafanyiwa haya na yeye kuna watu amewahi kuwaumiza kwa namna yoyote iwayo!!

Kaa kwa kutulia wewe polisi
Umewahi kufuatilia hukumu mahakamani ?
Nchi hii mpaka kutoa maiti mochwari Kuna longolongo !?

Watumishi wa umma wa nchi hii ni shida lakini pia watu wamekuwa wanyama sana sio Polisi sio nani?

Afrika pameingia pepo wabaya wa ubinafsi kila mahali.
Tumeona kwenye mitando Watu wanakaanga karanga za kuuzia binadamu wenzao lakini wanatia sulphuric acid kabla ya kuzikaanga. Sasa jiulize wamewauzia watu wangapi?

Watu wanafanya biashara Kwa kuweka vitu vya ajabu ajabu Kwa Imani za kishirikina. Madereva hawajali maisha ya watu wengine na kuua watu Kwa mamia.
Kwa Sasa ni kama nchi za Kiafrika zimechanganyikiwa mana Sasa watu wanashindana
 
Back
Top Bottom