Ofisi ya DED Magu mnawaonea Watumishi wa Umma linapofika suala la Malipo, Mamlaka husika fuatilieni suala hili

Ofisi ya DED Magu mnawaonea Watumishi wa Umma linapofika suala la Malipo, Mamlaka husika fuatilieni suala hili

Hagwila

Member
Joined
Apr 18, 2019
Posts
82
Reaction score
99
Umangimeza kwa baadhi ya maofisa wa serikali maofisini, unyanyasaji na upigaji; umerejea kwa kasi baada ya kupigwa stop kwenye awamu ya tano.

Mtumishi mmoja katika ofisi ya DED Magu anayehusika na masuala ya IT, ikiwa ni pamoja kutuma taarifa za malipo yaliyokwisha kuidhinishwa kwenda benki ili wanufaika wapate malipo yao kwa wakati; amekuwa akikalia taarifa hizo kwasababu zake binafsi, matokeo yake malipo kuchelewa.

Mfano hai ni waalimu wamechelewa kupata fedha zao za likizo ya mwisho wa mwaka 2023, licha ya kujaza Vendor Form mapema Novemba 2023; lakini fedha zimewekwa kwenye akaunti zao mwishoni mwa Disemba 2023, hivyo wengi wao hawakwenda likizo maana ilikuwa imebaki wiki moja tu shule kufunguliwa tarehe 08/1/2024.

Mamlaka husika fuatilieni jambo hili.

Mimi Mdau wa Elimu, Magu.
 
IT na maswala ya malipo wapi na wapi ? Wanaohusika na malipo ni wahasibu Idara ya fedha. Unamchafua bure IT hahusiki. Elekeza lawama zako kwa mtu sahihi.
 
Mtu wa IT anahusikaje na OC kushuka?

Mtoa mada naomba elimu kidogo hapo tafadhali.
 
Heri yao hata waMEshalipwa,

HIYO HALMASHAURI WAPO VIZURI.
 
Umangimeza kwa baadhi ya maofisa wa serikali maofisini, unyanyasaji na upigaji; umerejea kwa kasi baada ya kupigwa stop kwenye awamu ya tano.

Mtumishi mmoja katika ofisi ya DED Magu anayehusika na masuala ya IT, ikiwa ni pamoja kutuma taarifa za malipo yaliyokwisha kuidhinishwa kwenda benki ili wanufaika wapate malipo yao kwa wakati; amekuwa akikalia taarifa hizo kwasababu zake binafsi, matokeo yake malipo kuchelewa.

Mfano hai ni waalimu wamechelewa kupata fedha zao za likizo ya mwisho wa mwaka 2023, licha ya kujaza Vendor Form mapema Novemba 2023; lakini fedha zimewekwa kwenye akaunti zao mwishoni mwa Disemba 2023, hivyo wengi wao hawakwenda likizo maana ilikuwa imebaki wiki moja tu shule kufunguliwa tarehe 08/1/2024.

Mamlaka husika fuatilieni jambo hili.

Mimi Mdau wa Elimu, Magu.
Mwamba Hapo Magu DC nadhani hakuna Mtumishi hujawahi kumtaja JF kwa ubaya. Umewaleta Maafisa Elimu, HR, DED leo IT. Jiangalie isije kuwa wewe pia ni tatizo kama woote waliokuzunguka ni wachafu
 
Back
Top Bottom