Ofisi ya RITA, Missenyi wana matatizo gani?

Ofisi ya RITA, Missenyi wana matatizo gani?

NYENJENKURU

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2011
Posts
1,066
Reaction score
294
Ndugu wanaJamvi kuna jambo limenishangaza kidogo kutoka ofisi ya RITA MISSENYI mkoani Kagera.Kuna mtoto wa shemeji yangu aliomba cheti cha kuzaliwa kwa njia ya mfumo wa RITA ajaza kila kinachotakiwa kuwekwa kwenye mfumo.Baada ya wiki moja kwenye mfumo status ikaonyesha Cerificate Issued,Collect your cerificate at RITA office Messenyi.MAAJABU walipoenda kuchukua cheti wakaambiwa kweli kimetoka na wakawaonyesha ila wakaambiwa kwa utaratibu wao RITA Missenyi ni lazima kwanza uje wakuone na baada ya hapo unapewa siku mbili ndo uje ukichukue . Wameenda leo(23/5/2024) kuchukua wameambiwa warudi Jumatatu(27/5/2024) kweli hii ni HAKI au wanatengeneza mazingira ya kulamba Asali?
 
Nadhani Misenyi ni mpakani.
Kwaiyo wanafanya ufike wajiridhishe kama kweli wewe ni Raia maana Kuna Waganda, wanyankole , wachiga wengi Misenyi.
Fika wakuone kama watakuomba takrima toa ili urahisishe mambo, Dunia hakuna haki
 
Nadhani Misenyi ni mpakani.
Kwaiyo wanafanya ufike wajiridhishe kama kweli wewe ni Raia maana Kuna Waganda, wanyankole , wachiga wengi Misenyi.
Fika wakuone kama watakuomba takrima toa ili urahisishe mambo, Dunia hakuna haki
Hao RITA wana matatizo yao kibao na hapo siyo suala la mpakani wala nini.

Mimi niliomba kupitia makao makuu baada ya kupoteza cha awali. Nikaambatisha kila kitu. Cha ajabu baada ya week tatu nakuta hakuna chochote maombi bado yapo pending. Nikawapigia simu na aliyepokea akashangaa ni kwanini akaomba kuingia kwenye account yangu niliyosajili nikampa na akasema hakuna shida anaona kila kitu kiko sawa na anashindwa kuelewa tatizo ni nini. Alichoniambia ni analifikisha kwa dawati husika. Nilisubiri miezi miwili lakini hakuna kilichofanyika. Mwisho niliwapigia tena simu na alipokea jamaa wa kiume alichonijibu niliamua kuacha kufuatilia tena ili siku nikienda nilipozaliwa nifuatilie huko huko. Hapa nilitambua kwamba hizi ofisi zina watu ambao si sahihi kuwepo katika ofisi hizo.

Baada ya miezi mitatu nililazimika kuomba upya baada ya kukosa muda na kulipa tena hela.. Nikaattach kila kitu na nyaraka zilikuwa zinasomeka vizuri tu. Baada ya siku tano nikajibiwa kwamba mojawapo ya nyaraka haisomeki vizuri. Nikascan na kuattach upya lakini majibu ni yale yale. Nikapiga simu nikaambiwa niattach kama walivoelekeza lakini wapi hakuna lolote.

Nilichokifanya niliamua kujisajili tena upya kwa kutumia email tofautu ila taarifa nilijaza zote sahihi na kuattach nyaraka zile zile. Baada ya siku 4 cheti kilitolewa na nilikipokelea Ruvuma bila kuulizwa chochote zaidi ya kuwasilisha nakala ya nyaraka nilizojaza mtandaoni na viambata vyake na hapo nililipa maombi matatu kwa 21,000 badala ya 7,000 kwa ombi moja tu.

Ajabu maombi yote niliyoyafanya nikiingia kwenye account yangu kwa sasa yanaonekana na status ya mawili ni returned na moja printed.
HAO WANA LAO JAMBO NA INGEKUWA MASUALA YA URAIA WASINGEPRINT HICHO CHETI
 
Hao RITA wana matatizo yao kibao na hapo siyo suala la mpakani wala nini.

Mimi niliomba kupitia makao makuu baada ya kupoteza cha awali. Nikaambatisha kila kitu. Cha ajabu baada ya week tatu nakuta hakuna chochote maombi bado yapo pending. Nikawapigia simu na aliyepokea akashangaa ni kwanini akaomba kuingia kwenye account yangu niliyosajili nikampa na akasema hakuna shida anaona kila kitu kiko sawa na anashindwa kuelewa tatizo ni nini. Alichoniambia ni analifikisha kwa dawati husika. Nilisubiri miezi miwili lakini hakuna kilichofanyika. Mwisho niliwapigia tena simu na alipokea jamaa wa kiume alichonijibu niliamua kuacha kufuatilia tena ili siku nikienda nilipozaliwa nifuatilie huko huko.

Baada ya miezi mitatu nililazimika kuomba upya baada ya kukosa muda na kulipa tena hela.. Nikaattach kila kitu na nyaraka zilikuwa zinasomeka vizuri tu. Baada ya siku tano nikajibiwa kwamba mojawapo ya nyaraka haisomeki vizuri. Nikascan na kuattach upya lakini majibu ni yale yale. Nikapiga simu nikaambiwa niattach kama walivoelekeza lakini wapi hakuna lolote.

Nilichokifanya niliamua kujisajili tena upya kwa kutumia email tofautu ila taarifa nilijaza zote sahihi na kuattach nyaraka zile zile. Baada ya siku 4 cheti kilitolewa na nilikipokelea Ruvuma bila kuulizwa chochote zaidi ya kuwaailisha nakala ya nyaraka nilizojaza mtandaoni na viambata byake.

Ajabu maombi yote niliyoyafanya nikiingia kwenye account yangu kwa sasa yanaonekana na status ya mawili ni returned na moja printed.
HAO WANA LAO JAMBO
Basi labda Kuna mengi machafu siyajui
 
Ndugu wanaJamvi kuna jambo limenishangaza kidogo kutoka ofisi ya RITA MISSENYI mkoani Kagera.Kuna mtoto wa shemeji yangu aliomba cheti cha kuzaliwa kwa njia ya mfumo wa RITA ajaza kila kinachotakiwa kuwekwa kwenye mfumo.Baada ya wiki moja kwenye mfumo status ikaonyesha Cerificate Issued,Collect your cerificate at RITA office Messenyi.MAAJABU walipoenda kuchukua cheti wakaambiwa kweli kimetoka na wakawaonyesha ila wakaambiwa kwa utaratibu wao RITA Missenyi ni lazima kwanza uje wakuone na baada ya hapo unapewa siku mbili ndo uje ukichukue . Wameenda leo(23/5/2024) kuchukua wameambiwa warudi Jumatatu(27/5/2024) kweli hii ni HAKI au wanatengeneza mazingira ya kulamba Asali?
Comment haya Maelezo kwenye page yao ya Instagram, ujumbe utamfikia hadi bosi wao wa juu kabisa na utasaidiwa haraka sana, mie nilishawahi kufanya hivyo na issue yangu ikajadiliwa hadi kwenye magroup yao ya Whatsapp na wazembe wakabainika.
 
Back
Top Bottom