OilCom inahusika kuchakachua mafuta?

OilCom inahusika kuchakachua mafuta?

Dadake

Member
Joined
Jul 1, 2010
Posts
8
Reaction score
2
Serikali na mamlaka zake inadai inaendelea kupambana na vitendo vya kuchakachua mafuta ya dizeli na petroli, lakini ufuatiliaji niliofanya unaashiria kuwa baadhi ya watendaji ndani ya serikali na mamlaka zinazotarajiwa kudhibiti vitendo hivyo wanafahamu wanaofanya uovu huo na pengine kuwasaidia kwa namna mbalimbali.

Kampuni ya kusafirisha na kuuza aina mbalimbali za mafuta, yaani dizeli, petroli, mafuta ya taa na mafuta ya ndege, Oil Com inasadikiwa kufanya uchakachuaji mafuta kabla haijayaingiza sokoni.

Mei 20, mwaka huu gari la kampuni hiyo Scania Na.T517AJM lenye tela Na. 687ACP lililoendeshwa na S. A. Mkude lilipakiwa lita 35,000 za dizeli katika depot ya kampuni hiyo, Kurasini jijini Dar es Salaam.

Gari hilo likaegeshwa ndani ya Yadi ya kampuni hiyo iliyopo Tabata Relini. Safari ya kupeleka mafuta hayo Ushirombo wilayani Bukombe ilianza Mei 21 mwaka huu, siku ya Ijumaa ambapo yalitakiwa kuwasilishwa kwa Kampuni inayojenga barabara ya Ushirombo mpaka Lunzewe, ambayo imeingia mkataba wa kuuziwa mafuta na Oil Com.

Afisa wa kampuni ya ujenzi, Gasper Msuya, alipelekewa mafuta na nyaraka zinazohusika na mzigo huo na Mkude Jumatatu asubuhi. Baada ya kuchukua sampuli ya mafuta kutoka ndani ya gari hilo na kuondoka nayo, alirejea mchana na kumueleza Mkude kuwa hawezi kupokea mafuta hayo, yamechakachuliwa.

Dereva na gari vikatakiwa kupelekwa polisi Ushirombo. Dereva akaomba polisi ishirikiane na EWURA wachukue sampuli ya mafuta hayo ikafananishwe na yaliyo kwenye matanki ya mafuta yanayomilikiwa na Oil Com yaliyopo Kurasini Dar es Salaam ambapo mafuta hayo yalichukuliwa kwa maelezo kuwa, wakati yakipakiwa hata yeye aliingiwa na shaka kutokana na wepesi wake.

Tofauti na matarajio, wakati dereva huyo akiwa rumande, ofisi ya Oil Com Kahama iliagiza dereva akachukua gari hilo siku hiyo hiyo ya Jumatatu. Inasadikiwa ilipelekwa Kahama. Dereva alishikiliwa na polisi tokea Jumatatu hadi Ijumaa ambapo aliambiwa ajidhamini kwa leseni yake, akae eneo hilo la Ushirombo kwa siku chache, waliomshitaki wasipofika ili apelekwe mahakamani angeachiwa huru arudi Dar. Hakupelekwa mahakamani kwani walompeleka waliingia mitini.

Ufuatiliaji ukafanikisha kupatikana namba ya simu ya kiganjani ya afande aliyeshughulikia sakata hilo na jina lake kwa sasa linahifadhiwa, akaitwa na kuhojiwa:

Swali: Tunazo taarifa kwamba mmekamata mafuta yaliyochakachuliwa na dereva anayetuhumiwa kufanya kosa hilo, suala hilo limefikia wapi?

Jibu: Ni kweli suala hilo lilitokea, lakini siwezi kulizungumzia kwa kina, waulize wakubwa

Swali:
Wakubwa wakina nani? Si ulilishughulikia wewe?

Jibu: Nakushauri umuulize mkuu wa upelelezi.

Ufuatiliaji ukafanikiwa kupata namba ya mkuu wa upelelezi wa wilaya ya Bukombe, Leonard Paul, alipoulizwa baada ya kuelezwa sakata lote lilivyokuwa tokea gari lilivyopakia mzigo hadi lilivyofika mikononi mwa polisi Ushirombo alisema hivi:

"Kwakweli sina taarifa za uhakika za kukueleza kuhusu suala hilo. Kwanza tokea Mei 20 mpaka Mei 30 mwaka huu, sikuwepo wilayani nilikuwa mafunzoni mjini Morogoro. Hata sasa tunavyozungumza nipo vijijini kikazi, nikirudi wilayani nitafuatilia na kutoa ufafanuzi."

Kwa mwendo huu, mchezo huu mchafu utakwisha? Kwa vyovyote hizo lita 35,000 zilisambazwa sokoni baada ya kushtukiwa na kampuni ya ujenzi na kutolewa nje, yalipelekwa wapi? Hilo ni swali linalohitaji kufanyiwa kazi...
 
Haki katika taifa letu, safari bado ni ndefu. Rushwa hupofusha macho ya wenye madaraka wanapokubali kuikumbatia.
 
Haya mambo nadhani kama JK hataki kufuta ushuru wa mafuta ya taa ambayo sasa vijini yanalanguliwa kwa bei kubwa hata kuliko yangekuwa na ushuru basi panahitajika utaalamu wa kina, wapo madereva ambao kweli wamenemeeka na sakata hili, lakini kama amepewa mafuta ambayo tayari jamaa wameishayashughulikia-yeye ana vipimo gani vya kugundua?

Sijajua kwanini JK hataki kutoka ushuru wa mafuta ya taa? Angalau akaokoa hasara ya vifaa vyetu,hasara ya bandari na kampuni zinasomba mafuta kwa ukweli na heshima ya nchi kwa majirani.

Iko kazi!:sick:
 
nenda bp mafuta yao safi, BP wamewanyang'a vituo kibao franchise yao kwa ajili ya kuchanganya mafuta
 
Utaanza kugusa maslahi ya watu. Kama mngelijua jinsi gani oil industry inavyotumiwa kuharibu mambo wala tusingelisema. Na kiboko kinakuja baada ya mnunuzi wa BP ambaye inaaminika ni ....kuingia sokoni
 
wanaochanganya mafuta si madereva wa malori, ila ni wafanyabiashara wanaoagiza hayo mafuta au wanaonunua kutoka depot za mafuta. hawa wanashirikiana na watu wa depot kufanya huu uhalifu. dereva yeye ni kibaru tu na hausiki kwa lolote lile.
 
wanaochanganya mafuta si madereva wa malori, ila ni wafanyabiashara wanaoagiza hayo mafuta au wanaonunua kutoka depot za mafuta. Hawa wanashirikiana na watu wa depot kufanya huu uhalifu. Dereva yeye ni kibaru tu na hausiki kwa lolote lile.

sure....
 
..........na yale malori ya mafuta yaliyochachuliwa toka Tanzania yaliyokamatwa Rwanda yameishia wapi?
 
tutafika tu kwa kuwa tayari tumeshakuwa damping place na shamba la bibi. Uozo Uozo tu.
 
Tamaa itaharibu kila kitu si ajabu hayo mapolisi yamepewa vihela yanaanza kuzungusha mambo...
Wakati dhahama itawakumba na wao...

Afu ma-viongozi yetu nayo hivi hawaskii...hawaoni..au kwakua sisi walipa kodi ndo tunaendesha maisha yao..ndo maana hawajali..

Nyie wenye maamuzi fikieni mahali muone hizo benki na nchi mnazopenda kuweka fedha..na kuishi huko..
Hao jamaa walipenda Nchi zao kuzijenga hazikushushwa.....

Ni upuuzi kama huu wa mafuta waliukataa ndo maana leo mnakimbilia huko..
 
Poor Tanzania. Ukitoa ushuru kwenye mafuta ya taa ndiyo kwanza unawaua Watanzania wenzetu wanyonge. Tunahitaji utawala wa sheria usioangalia personality. Wanasheria wenyewe wako wapi kina Mkono et al? Safari bado ni ndefu kuliko ya kutafuta uhuru. Tunachotakiwa kusema ni ENOUGH IS ENOUGH. YES WE CAN
 
Wana JF,

Haya Yote mie nayapeleka EWURA

Kwa any Administration iliyo vyema katika utendaji wake wa kazi ilipaswa itoe haki bin haki kwa tukio lililotokea Moshi baada ya kituo kimoja kuwa na mafuta yachakachua kwanini naseam hivi.

1: Vituo vyote vya mafuta huwa vyakaguriwa na EWURA huko mikoani na wilayani sasa napenda kujua EWURA wao huwa wamejipanga vipi kwa utaratibu upi wa kukagua vituo vya mafuta??

Iweje hili kosa liende kuwaangukia walio na kituo cha mafuta pale Moshi kwanini hii ni dhahili kuwa EWURA hawawezi kazi yao na wao wachukuliwe hatua especially viongozi wao wa Moshi; hili ni uzembe mkubwa sana nchi nzima.

Kwanini nasema hivyo; inaonekana hizi sheria zitungwazo ni za kufanyika Dar tu basi na sio applicable sehemu nyingine ndani ya nchi hii, jamani viongozi angalieni haya m-yafanyayo katika jamii inayowazunguka na kuwapa dhamana ya kuwaongoza nyie mfanye madudu muhukumu mnaowasimamia; hii si haki mmeivuruga sheria hapo.

2: EWURA inapo toa sheria zake kwa watu wanao husika na taasisi hii je huwa inapewa mamlaka gani katika kujisimamia sheria na utekelezaji wake wa sheria ilizo zitunga??

eg: Kulitolewa tamko kuwa dereva akutwapo akiendesha gari huku anaongea na simu atashikiliwa. Hili sijaliona likitekerezwa kwanini? Ni kuwa mlilirukia hili swala pasipo kulitizama kiundani na kulipangia mikakati makini kwa ajili ya utekelezaji wake na likawashinda. Kwanini mbwatuke kwa kutunga sheria mzisemazo na kushindwa tekeleza?

3: Kwanini kila siku twaimbia serikali yetu haiko makini kila kukicha bla bla zimekuwa nyingi sana? Imefika mahali tuache uzembe na tufuatilie utekelezaji.

4: Hivi wana JF niwaulize kwanini kila kukicha wananchi hasa wafanyabiashara wanakuja na mbinu mpya za ujanja ili kujipatia kipato zaidi na kuwakandamiza watumiaji wakubwa ambao ni watanzania maskini wenye kipato kidogo?

Je hii ni serikali yetu inashindwa kukaa na kudadisi kujua kunani huko na ni mbinu gani zitumike kuepusha hili balaa la watu kuwa creative kwa kuwanyongea kati raia wasio kuwa na uwezo kuumia katika maisha haya? Na wizara zipi husika zahusika Wizara ya UCHUMI, ULINZI (Mambo ya ndani), TRA?

Sielewi kuna mzimu gani katika serikali hii!
 
..kuna mtandao wa matajiri unaojihusisha na biashara ya mafuta machafu nchini.

..hawa naona wamekuwa kama poachers wa miaka ile ya 80.


Hata hivyo, Spika Sitta alisisitiza kuwa, siku zote Bunge litasimama mstari wa mbele kutetea haki za watu na haliwezi kuendelea kubaki kimya kama mambo yakienda tofauti.

Alitolea mfano wa Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji (Ewura) ambayo imefungia baadhi ya wafanyabiashara wa mafuta mkoani Morogoro kutokana na kugundulika kuuza mafuta machafu mkoani humo.

Katikati ya mwaka jana, Ewura ilivisimamisha kutoa huduma vituo kadhaa vya kuuza mafuta kwa tuhuma za kuuza bidhaa hiyo ikiwa chini ya viwango.

Spika Sitta alisema Mahakama moja mkoani Morogoro, ilishirikiana na wafanyabiashara wa mafuta na kuweka pingamizi mahakamani dhidi ya amri hiyo ya Ewura.



Waliokaidi agizo la EWURA watozwa faini mil 10/-

na Happiness Katabazi

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es salaam, imewahukumu kifungo cha miezi sita nje na kulipa faini ya sh milioni 10 wafanyabiashara wawili wa vituo vya mafuta baada ya kupatikana na hatia ya kukaidi amri ya Mamlaka ya Uthibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) ya kufunga vituo vyao vilivyokuwa vikiuza mafuta yaliyochachuka.

Wafanyabiashara hao ni Mohamed Twalib Nahdi na ndugu yake Abdulatif Twalib Nahdi ambao wote ni wakazi wa Morogoro.
Akitoa hukumu hiyo mwishoni mwa wiki, Jaji Thomas Mihayo, alisema amekubaliana na hoja zilizowasilishwa na Wakili wa Ewura, James Kabakama, kwamba amri iliyotolewa na mamlaka hiyo Septemba 19, 2008 inapaswa kuheshimiwa.

Jaji Mihayo alisema yeyote atakayekiuka amri ya mamlaka hiyo atachukuliwa hatua kali za kisheria na kwamba ametoa adhabu nafuu kwa wafanyabiashara hao, ili waweze kujirekebisha.

Kufuatia uamuzi huo, Jaji Mihayo amewataka wafanyabiashara hao kutotenda kosa kama hilo ndani ya miezi sita na akawapa wiki mbili wawe wameshalipa faini ya sh milioni tano kila mmoja. Vituo vya mafuta anavyomiliki Abdulatif Twalib Nahdi ambavyo vimefungiwa ni Kobil Msamvu Petrol Station na Abdulatif Petrol Station.

Aidha, Mohamed Twalib Nahdi naye anamiliki vituo vya Mohamed Twalib Petrol Station, Oilciom Kihenda Petrol Station na Mohamed Twalib Oilcom Petrol Station. Ilidaiwa kuwa EWURA walifanya ukaguzi wa vituo vyote vya mafuta mkoani Morogoro kati ya Septemba 13 na 14 mwaka jana na kubaini vituo vya wafanyabiashara hao kuwa vilikuwa vinauza mafuta yaliyochakachuliwa.

Kutoka na hali hiyo, EWURA, iliwataka wafanyabiashara hao kufunga vituo vyao na kujieleza kwa nini wasichuliwe hatua kwa kuuza mafuta yaliyochakachuliwa. Hata hivyo, wafanyabiashara hao walikiuka amri hiyo na kuendelea na shughuli zao.
 
..kuna mtandao wa matajiri unaojihusisha na biashara ya mafuta machafu nchini.

..hawa naona wamekuwa kama poachers wa miaka ile ya 80.

Dereva ametoa wito kwa EWURA kwamba waende kupima mafuta ya kwenye tanks za oilcom, Ewura hawakuende wala polisi hawakujali. kilicho fuata ni gari kutoweka. mchawi gani tena tunamtafuta? wachawi ni EWURA na OILCOM (Waigizaji). wengine wapo mjini hawajui umuhimu wa mafuta ya taa kwa 80% ya watanzania. Lets call a spade a spade.Ewura na waigizaji wa mafuta wanahusika basi.
 
Wapendwa wanaJF nawashukuru kwa michango yenu kuhusu taarifa za hujuma katika uchumi wa nchi yetu, zinazofanywa na watu wasiyo na uchungu kwa jamii ya Watanzania. Leo nawahabarisha yaliyompata dereva wa Scania lililosafirisha mafuta hayo.

Ufuatiliaji wangu umefanikiwa kumpata dereva huyo na amezungumza kwa kinywa chake mwenyewe, amethibitisha kuwa yote niliyoeleza ni kweli tupu, zaidi ya yote ameongeza baadhi ya taarifa zilizokuwa zimekosekana na ameeleza maswahiba yaliyompata baada ya kurejea kwenye kampuni ya Oil Com ambayo inamiliki kampuni ya usafirishaji mafuta ya Al-hushoom.:crying:
 
Wapendwa wanaJF nawashukuru kwa michango yenu kuhusu taarifa za hujuma katika uchumi wa nchi yetu, zinazofanywa na watu wasiyo na uchungu kwa jamii ya Watanzania. Leo nawahabarisha yaliyompata dereva wa Scania lililosafirisha mafuta hayo.

Ufuatiliaji wangu umefanikiwa kumpata dereva huyo na amezungumza kwa kinywa chake mwenyewe, amethibitisha kuwa yote niliyoeleza ni kweli tupu, zaidi ya yote ameongeza baadhi ya taarifa
zilizokuwa zimekosekana na ameeleza maswahiba yaliyompata baada ya kurejea kwenye kampuni ya Oil Com ambayo inamiliki kampuni ya usafirishaji mafuta ya Al-hushoom.:crying:

Again, we should take interest to know much more about Haruna Masebu, person in charge of EWURA. Naona kama kuna watu hata ndani ya Ewura wananeemeka na hii biashara inayoendelea.

Na tujue pia kampuni kama oil com inamilikiwa kwa asilimia miamoja na wawekezaji wa ndani ambao wananeemeka sana na political cconnection zilizopo. Hawa Oilcom kuna kipindi kulikuwa na tetesi wangelipewa biashara ya kupeleka mafuta ya ndege kwenye viwanja vyetu, ila hizi big airlines zikagoma. Kama sikosei wakaishia kujenga depot yao Mwanza.

Sasa kampuni ambayo mambo ya Safety na environment siyo part ya biashara yao watawezaje kuwa players wa kweli kwenye soko?Tukumbuke pia wanaoperate kwenye nchi kama Malawi as Petroda..that tells alot about how big they are.

Ifike sehemu sasa kila player achunguzwe na watu tujue hili tatizo ni la nani. Tukiacha haya yaendelee, tutakuja jaza maji kwenye ndege maana uovu hauna kiasi.
 
Salaam wanaJF,

Kama umesoma taarifa yenye kichea cha habari "Oil Com inahusika kuchakachua mafuta", tutaelewana vizuri katika taarifa hii ambayo ni muendelezo wake.

Dereva aliyejitambulisha kwa jina la Sulusi Alex Mkude amekiri kuendesha Scania la Oil Com lililopeleka lita 35,000 za dizeli zilizosadikiwa kuwa zilikuwa zimechakachuliwa, na amekiri kuziwasilisha kwa Gasper Msuya, aliyeajiriwa na kampuni inayotengeneza barabara Ushirombo wilayani Bukombe. Amekuwa dereva wa Oil Com kwa miaka 12 na miezi 6.

Amemtaja kwa jina moja askari polisi wa kituo cha Ushirombo, afande Luso, kuwa ndiye aliyekuwa mpelelezi wa shauri hilo. Anamtaja bosi wa Oil Com ofisi ya Kahama kwa jina moja la Ladwa kuwa ndiye aliita dereva ambaye yeye (Mkude) hamfahamu, akaondoa gari kwenye kituo cha polisi Ushirombo na kuipeleka wanakojua.

Alirejea Dar es Salaamaam Juni 5, mwaka huu. Akaugua kwa wiki moja na siku tatu kisha akajirejesha ofisini-yadi ya Oil Com iliyo Tabata relini ambapo alikutana uso kwa uso na Scania lililomwacha kituo cha polisi Ushirombo.

Anasema akamueleza Abdallah Bushilingi ambaye anawajibika kwake, kila kilichompata safarini. Abdallah akamwambia akazungumze na work shop manager anayetajwa kwa jina la Mbaraka. Naye akamwambia akazungumze na Islam ambaye ni meneja wa depot iliyo Kurasini. Hapo anasema hakuonana naye bali sekretari wake baada ya kumweleza uwepo wa Mkude kupitia simu, Islam alitoa maelekezo kwamba akaonane na Norshad ambaye ni msimamizi wa ofisi za Oil Com Tabata relini.

Akaambiwa, "hamna tatizo, rudi kazini lakini gari lako (scania alilosafirishia mafuta likamwacha kituoni Ushirombo) limerudi likiwa bovu, linatengenezwa hivyo lisimamie litengenezwa vizuri." anawataja mafundi waliyolitengeneza kuwa ni Omari na Rama. lilikuwa na ubovu mbalimbali ikiwemo kupasuka busta.

Akaambiwa kwa kuwa gari lake bovu, atakuwa anaendesha tiper linalofanya kazi za ndani ya kampuni hiyo kwa sababu dereva wa gari hilo alifiwa akaenda kwenye msiba Morogoro. aliendesha gari hilo kwa siku tatu. siku mbili alisomba kifusi kutoka kwenye eneo la kusaga mawe linalomilikiwa na kampuni hiyo lililopo Boko kukipeleka kwenye yadi mpya iliyopo Tabata relini jirani na AMI.

Siku ya tatu anasema alisomba udongo uliyochimbwa ndani ya yadi mpya-AMI kuupeleka kwenye yadi mpya nyingine iliyo Malawi cargo, kufukia mashimo. Dereva wa lori hilo aliporudi, akabaki na bila kazi, Juni 28 mwaka huu akapewa Scania T653 ABG aisimamie itengenezwe, ilipokamilika akaambiwa apakie matenki ayapeleke mkoani Mtwara.

Anasema alipoingia ofisini kwa Norshad kuomba nyaraka za kusafirisha mzigo huo, akaambiwa na Norshad, "Wewe sitaki kukuona ofisini kwangu wala ushike gari langu lolote, toka leo kazi basi, njoo kesho uchukue kiinua mgongo chako."

Anasema alipokwenda Ijumaa (juzi) akaambiwa aende kesho yake (leo) alipofika leo amepewa sh. 150,000/- kuwa ndicho kiinua mgongo chake kwa miaka 12 na nusu aliyofanyia kazi kampuni hiyo.

Anasema kwa muda wote huo hakuwahi kuwa na mkataba wa ajira wala kulipiwa mchango wowote katika mfuko wa taifa wa hifadhi ya jamii (NSSF) hivyo alichovuna pekee ni hiyo laki moja na nusu.

Zaidi anasema ameambiwa, asithubutu kushitaki mahala popote kwa sababu hana atakachopata bali atakuwa amejifungia milango ya ajira ya udereva kwa waarabu wote wanaomiliki magari ya kusafirisha mizigo ndani na nje ya nchi.

Pia anasema ameambiwa hivi, akae atulie, ikibidi atafute shughuli nyingine na kwamba ikipita muda kama mwaka mmoja hivi akihitaji kazi kwenye kampuni yao wanaweza kumchukua awafanyie kazi tena.

HAPA inaibuka hoja nyingine ya maslahi ya wafanyakazi katika mashirika ya usafirishaji wa mizigo masafa marefu kwa sababu kumbukumbu zinaonyesha kuwa mfanyakazi mwingine wa kampuni hii anayeitwa George amefungua shitaka kwenye Baraza la Usuluhishi na Upatanishi, kudai malimbikizo ya mapunjo ya mishahara yake na malipo ya kila siku alizokuwa akisafirisha mizigo ya Oil Com, nje ya Nchi.

Shauri hilo litatajwa tena kwenye baraza hilo la Taifa Julai 5, mwaka huu. Mkude anasema wapo madereva wengi, zaidi ya 300 wanaofanya kazi za kampuni hiyo hawana mikataba ya ajira wala hawalipiwi NSSF. Hoja ni kwamba, ina maana hata NSSF wamewekwa 'viganjani' na Oil Com?

Binafsi inanikera sana, nayaandika haya ili mnao husika najua mnayasoma. mtambue kuwa nchi ikiingia kwenye machafuko jeuri yenu haitasaidia na hao mnaodhani ni wenzenu hamtawaona bali mtashuhudia raia wasiyo na hatia wakiangamia.

Hata kama nyinyi mtafanikiwa kuepuka madhara lakini mtaweza kupoteza ndugu, wapendwa na au wana ukoo wenu na hizo mali mnazokumbatia hamtapata raha ya kuwa nazo kwa sababu zitawasuta kila mtakapoziangalia. Jamani, rudisheni moyo wa uzalendo kwa kuacha kukumbatia watu wenye uraia na asili ya Nchi zaidi ya moja ambao wamegeuza Tanzania kuwa sawa na Ubungo Terminal.

Yaani wapo Tanzania kama wasafiri vile, usafiri wao ukifika (vurugu), kila mmoja wao anachukua kilicho chake na kutokomea. siyo wajinga hawa watu wanajua wanalofanya. hawana hasara ya jina la Tanzania kuchafuka kwa sababu si lao, aibu kwenu vibaraka wao.

Kwa sasa niwaache, tukutane wakati mwingine nitakapowaletea yatakayozungumzwa na Haruna Masebu wa EWURA, Waziri/Naibu waziri au Katibu Mkuu Wizara ya Kazi, Ajira na maendeleo ya Vijana, uongozi wa NSSF - Taifa kuhusu suala zima la makato ya wafanyakazi hususani madereva wa Oil Com
 
Back
Top Bottom