Siku moja vijana hawa wakitokea Houston waliingia kwenye baa moja pale Dallas ambamo mimi na wenyeji wangu tulikuwa tukijiburudisha na vinywaji; nadhani baa ile ni maarufu sana kwa watanzania. Basi acha watoto hao wa Houston wafanye kufuru kwenye baa hiyo. Niliiuliza vijana hao wanatoa wapi pesa ya kusanganya namna ile, nikawa interested kujua biashara yao. Akili iliyokuwa imeniijia mara moja wakati huo ni kuwa huenda wanashiriki kusambaza madawa ya kulevya kutoka Central/South Amerika. Lakini mmoja wa wenyeji wangu akasema kuwa watanzania wa Houston wana njia nyingi za haramu ikiwa ni pamoja na kuiba cheki za makampuni wanamofanyia kazi, kupitisha madai ya uwongo insurance, na wakati mwingine kuiba bidhaa kutoka kwa waajiri wao na kuziua kama machinga vile. Baada ya miezi minne tu hivi nikasikia wamekamatwa ingawa somebody Lauwo ambaye inasemekana alikuwa smart kuliko hao wengine alifanikiwa kutoroka alipoona upepo unaaza kugeka.
Unfortunately kuna watanzania wengi sana huko Ughaibuni wanajishghulisha na mambo ya wizi wa kujipatia hela ya haraka haraka. Matatizo ya wengi wao wakishazipata wanakuwa watambaji sana wenye matumizi ya kukithiri. Ninafahamu Mkenya mmoja aliyekuwa mwizi pia wa pesa za kodi (IRS) lakini alipokamwata alikuwa ameshakuwa tajiri kweli kweli akiwa na mapartment yake binafsi pamoja na majumba ya kupangisha mengi tu. Sielewi mali zake hizo zilifanyiwa nini lakisi sidhani kama alifilisiwa zote, nadhani alifungwa na kutakiwa kulipa kodi alizoiba pamoja na interest, kwa hiyo mali nyingine zilizobaki akaendelea kuwa nazo.