Okwi ana dawa ya msukule

Okwi ana dawa ya msukule

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Simba kwa Okwi ni kama Mbwa kwa chatu. Kutokana na tabia ya chatu ya kumeza wanyama wazimawazima na kuozea tumboni mwake anapomtaka mbwa anatanua tu domo lake na kutoa harufu ya ufundo inayowafutia wanyama wenye uroho wa nyama kama mbwa/Simba SC.

Mbwa huwa anajipeleka mwenyewe mdoni mwa chatu/Okwi kutokana na uroho wake wa kupenda vinono.

Okwi anajulikana sana kwa usumbufu wake na kuzitesa club za Tanzania kila wakati. Anafanya mazoezi ya kufa mtu ili kujiweka fiti/kutoa uvundo na kuzifutia club/mbwa "jinga" za Tanzania zinazopenda vinono.

Anafuta mkwaja wao kisha huyoooo Uganda anaumwa, ana matatizo ya kifamilia, ana hili na lile. Cha ajabu msimu mwingine ukifika Simba ameshasau anaingia mtegoni tena kwa Okwi. Utadhani Okwi amewachukua msukule viongozi wa Simba.
 
Wewe inakuhusu nini au lini uliombwa ukatoe msaada simba kwa niaba ya Okwi
 
Wewe inakuhusu nini au lini uliombwa ukatoe msaada simba kwa niaba ya Okwi
Wewe vepee! Inaniuma kishenzi aisei, hasa kule timu kufungwa na Green Worriers, Azam na kufukuzwa Omog wakati tuna bonge la mchezaji wetu Okwi ambae huenda angesaidia kuepusha yote haya. Utakiona kitakachotokea tena kwa URA na kombe la Mapinduzi!!
 
Wewe vepee! Inaniuma kishenzi aisei, hasa kule timu kufungwa na Green Worriers, Azam na kufukuzwa Omog wakati tuna bonge la mchezaji wetu Okwi ambae huenda angesaidia kuepusha yote haya.
Wapo pia Ngoma na Chirwa, ambao wamepokelewa kishujaa na wapo Zanzibar
 
Wapo pia Ngoma na Chirwa, ambao wamepokelewa kishujaa na wapo Zanzibar
Ni kweli hawapo pia, lakini sababu ya kutokuwepo inafahamika vema "U-KA-TA" ndani ya club kitu ambacho hakipo Simba.
Hata hivyo, Pamoja na kukosekana kwao Yanga iko imara kwa kiasi fulani ukiondoa ile mechi na Mbao FC.
 
Wewe vepee! Inaniuma kishenzi aisei, hasa kule timu kufungwa na Green Worriers, Azam na kufukuzwa Omog wakati tuna bonge la mchezaji wetu Okwi ambae huenda angesaidia kuepusha yote haya. Utakiona kitakachotokea tena kwa URA na kombe la Mapinduzi!!
Umeongea Mkuu.
Okwi mimi ananikera sana kama mpenzi wa timu ya Simba.
Simba inatatizo la mshambuliaji mfungaji, inaamua kusajiri mshambuliaji wa kimataifa Okwi.
Okwi hana muda wa kuichezea Simba, akicheza mechi moja au mbili anatafuta sababu na kuondoka zake anakokujua yeye.
Timu inakosa mgungaji wake mahili na inaishia kufungwa na timu pinzani.
Sasa Simba kama timu inayohitaji ushindi inamchukuliaje huyu mshambuliaji wake wa kimataifa ambaye mda wake mwingi anautumia kuzurula mitaani ?
Simba inahitaji ushindi au inamuhitaji mtalii Okwi ?
Ningekuwa mdau wa usajiri wa timu ya Simba hakika ningemfukuza Okwi, potelea mbali ningekubali ghalama ya kumlipa ili akuze utalii wake anaoupenda.
Simba tunahitaji mshambuliji MWENYE MUDA WA KUICHEZEA TIMU YETU ILI KULETA MATOKEO CHANYA.

Simba hatuhitaji mshambuliaji anayejiona bora kuliko mafanikio ya timu yetu pendwa.
Okwi anazurula huku timu ya Simba ikidhalilika kwa kufungwa na vitimu vidogo kabisa au timu shindani.
Okwi huko aliko anayafurahia haya matokeo mabaya ya timu ya Simba.
Kama asingefurahia matokeo mabovu ya timu yake angefanya bidii kuichezea timu mara nyingi ili kupata matokeo yanayohitajika.
MO mfukuze Okwi kama ulivyomfukuza Amog.
Wapenzi wa Simba hatuna imani naye tena.
Mfukuze Okwi tutafute mshambuliaji mwenye MUDA wa kuichezea timu yetu na kuleta matokeo mazuri.
Okwi baki hukohuko Uganda utatue matatizo yako yote kwa nafasi.
Hatutaki Utapeli wako.
 
Umeongea Mkuu.
Okwi mimi ananikera sana kama mpenzi wa timu ya Simba.
Simba inatatizo la mshambuliaji mfungaji, inaamua kusajiri mshambuliaji wa kimataifa Okwi.
Okwi hana muda wa kuichezea Simba, akicheza mechi moja au mbili anatafuta sababu na kuondoka zake anakokujua yeye.
Timu inakosa mgungaji wake mahili na inaishia kufungwa na timu pinzani.
Sasa Simba kama timu inayohitaji ushindi inamchukuliaje huyu mshambuliaji wake wa kimataifa ambaye mda wake mwingi anautumia kuzurula mitaani ?
Simba inahitaji ushindi au inamuhitaji mtalii Okwi ?
Ningekuwa mdau wa usajiri wa timu ya Simba hakika ningemfukuza Okwi, potelea mbali ningekubali ghalama ya kumlipa ili akuze utalii wake anaoupenda.
Simba tunahitaji mshambuliji MWENYE MUDA WA KUICHEZEA TIMU YETU ILI KULETA MATOKEO CHANYA.

Simba hatuhitaji mshambuliaji anayejiona bora kuliko mafanikio ya timu yetu pendwa.
Okwi anazurula huku timu ya Simba ikidhalilika kwa kufungwa na vitimu vidogo kabisa au timu shindani.
Okwi huko aliko anayafurahia haya matokeo mabaya ya timu ya Simba.
Kama asingefurahia matokeo mabovu ya timu yake angefanya bidii kuichezea timu mara nyingi ili kupata matokeo yanayohitajika.
MO mfukuze Okwi kama ulivyomfukuza Amog.
Wapenzi wa Simba hatuna imani naye tena.
Mfukuze Okwi tutafute mshambuliaji mwenye MUDA wa kuichezea timu yetu na kuleta matokeo mazuri.
Okwi baki hukohuko Uganda utatue matatizo yako yote kwa nafasi.
Hatutaki Utapeli wako.
Hiki ndicho nilichookimaanisha mimi kwenye uzi huu, achana na mawazo ya suSzu36
 
Hiki ndicho nilichookimaanisha mimi kwenye uzi huu, achana na mawazo ya suSzu36
Sisi wadau wa ukweli wa timu ya Simba tumekuelewa.

Anachokifanya mchezaji wa Simba Emanueli Okwi ni Fedheha kwa timu.

Okwi anaidhalilisha timu makusudi kabisa.
Hata sifahamu kwanini viongozi wa Simba wako kimya tu.

Labda kawafanya Misukule kama inavyosemekana.

Mimi sina hamu na hicho kirusi Okwi.
 
Mimi namfananisha jamaa na mpigaji tuu....akishirikiana wapigaji wenzie....Nimeacha kulipia kadi yangu na sina mpango tena wa kuishabikia simba....upuuzi tu......najielekeza kwenye ndondo
 
Nasubiri kauli toka kwa mwenyekiti wetu wa kamati ya usajiri ,kwa kapombe tulishamsikia sasa tu nataka na kwa huyu
 
Alisajiriwa kwa mbwembwe pale msimbazi, lakini wakasahau ugonjwa wa okwi wa usumbufu na kudengua,viongozi wajifunze
 
Wacha ugonjwa üwatafune

Wajanja wachache wanatafuna hela ya ponjoro kiulaini kabisa kisha wanasema kikosì ghalì
 
Sisi wadau wa ukweli wa timu ya Simba tumekuelewa.

Anachokifanya mchezaji wa Simba Emanueli Okwi ni Fedheha kwa timu.

Okwi anaidhalilisha timu makusudi kabisa.
Hata sifahamu kwanini viongozi wa Simba wako kimya tu.

Labda kawafanya Misukule kama inavyosemekana.

Mimi sina hamu na hicho kirusi Okwi.
MCHEZAJI anaeongoza ligi kwa ufungaji wa magoli anapokuwa nje ya uwanja bila sababu za msingi anaiumiza timu na hafai kuchekewa. Hii ni pamoja na Obrey na Ngoma. Hata kama unaidai timu, lakini haimaanishi kuwa usipochezea timu kunapunguza ukubwa wa deni lako, club itakulipa kwa mujibu wa makubaliano na mkataba wako na club hata kama timu itashuka daraja kwasababu yako.
 
Wewe vepee! Inaniuma kishenzi aisei, hasa kule timu kufungwa na Green Worriers, Azam na kufukuzwa Omog wakati tuna bonge la mchezaji wetu Okwi ambae huenda angesaidia kuepusha yote haya. Utakiona kitakachotokea tena kwa URA na kombe la Mapinduzi!!
Ulitabiri
 
Nampa Pole
Emanueli Okwi.
Anaharibu Heshima Yake katika Soka hapa Tanzania.
Ni bora kama ataamua kustaafu Soka la Bongo
Kuliko hali ilivyo sasa.
Emanuel Okwi
Mchezaji Mzuri wa mpira wa Miguu.
 
Ulitabiri
Hahaha, mkuu nilijuwa thimba atatolewa kamasi jembamba na URA kutokana na trend yao iliyopo kwa sasa. Kocha makini anaposema anamtaka mchezaji fulani (Okwi, Chirwa au Ngoma) kwenye kikosi chake ana maana na amemaanisha hivyo, viongozi lazima wafanye kila linalowezekana kumleta huyo mchezaji na kuhakikisha kuwa anapatiwa mazingira mazuri ya kucheza kama kocha atakavyoona inafaa kwa mechi ile. Kwa mfano, kumfukuza Omog bila kutatua tatizo la Okwi kwanza ili aweze kutumiwa na Omog kwenye mechi ni kosa kubwa na sio sawa kwakuwa Omog kumkosa Okwi kwenye mechi ni sawa na Zidane kumkosa Ronaldo kwenye mechi au Barcelona bila Messi, au Man U bila Pogba kwenye mechi. Hapa unaweza kusema Omog ameponzwa na Okwi.
 
Back
Top Bottom