Okwi sasa kutua Dar Kesho Jumamosi kukipiga Msimbazi

kirerenya

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2013
Posts
1,696
Reaction score
2,253

Sasa ni uhakika kwamba Emmanuel Okwi anakuja nchini kumalizana na Simba kwa ajili ya kuanza kuichezea msimu ujao.

Okwi anatarajia kutua nchini kesho Jumamosi na Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe maarufu kama ZHP amethibitisha.

Hans Poppe amewaambia waandishi wa habari leo kwamba Okwi anakuja kumalizana na Simba na kazi itakuwa ni kusaini.

“Anakuja Jumamosi, hapa ni suala la kusaini kwa kuwa suala la mazungumzo tulimaliza Kampala,” alisema Hans Poppe.
 
Yaaani huwa siwaelewi simba huyu jamaa sijui kawaroga au ?,
Wanachompendea ni kuwafungia Yanga tuu,wakiwa na huyo wala hawana haja ya ubingwa maana kwenye mkataba wake kuna kipengele kuwa ahakikishe kuwa anaifunga yanga .
 
Wanachompendea ni kuwafungia Yanga tuu,wakiwa na huyo wala hawana haja ya ubingwa maana kwenye mkataba wake kuna kipengele kuwa ahakikishe kuwa anaifunga yanga .
Hehehehehe basi simba wana mattatizo sana.

Mchezaji wanamsajili anawakimbia halafu wanamsajili tena .

Wanawazimu.
 
Pamoja na ujio wake.

Swali, je,bado yipo fit km miaka yake ya nyuma,au anakuja kwa ajili ya jina lake tu????
 
Dah huyu Okwi nuksi.... Muulizeni kocha Felix Minziro kuhusu balaa la huyu mganda... Naona 5G inanyemelea.
 
Dah huyu Okwi nuksi.... Muulizeni kocha Felix Minziro kuhusu balaa la huyu mganda... Naona 5G inanyemelea.
Msimbazi kuna tatizo sio yaani mkiifunga yanga basi mnaona kama tayari mabingwa?. Hivi kipaumbele cha simba ni kuuifunga yanga tu.
Uhusiano wa Simba na Okwi ni sawa na ule wa Bashite na Mkulu una mambo yaliyofichika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…