Omari Mwariko nani anamfahamu?

Omari Mwariko nani anamfahamu?

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
OMARI MWARIKO NANI ANAMFAHAMU?

Huyo hapo chini aliyevaa kofia ni Omari Mwariko.

Nimemfahamu Omari Mwariko nakua na nasoma shule ya msingi Moshi katika miaka ya 1960.
Miaka hiyo Omari Mwariko alikuwa mtu maarufu sana.

Omari Mwariko ni msanii bingwa katika kuchonga na kazi zake zimeonyeshwa hapa nchini, Uingereza na Marekani.

Lakini kwa miaka mingi akawa kapotea katika ulimwengu wa usanii akawa haonekani wala hasikiki.

Siku moja miaka 13 iliyopita niko Moshi ghafla nikakutananae barabarani.
Nikamsalimia na nikajitambulisha kwa kumtajia jina la ndugu yake Athmani Upepo.

Hili jina "Upepo," si jina lake ila alipachikwa kwa ajili ya uwezo wake wa kukimbia mbio kwa kasi kubwa.
Nakumbuka utotoni Moshi kila mtu alikuwa na lakabu yake.

Kulikuwa na Ali Maresi.

Hili jina "Maresi," alipewa kwa uhodari wake mpirani kuwa akitanguliziwa pasi mpira akadodoshewa kwa mbele na kuupokea mabeki hawampati na atafunga goli.

Kulikuwa na Athumani Makufuta.

Kisa cha jina hili ni kuwa tukisomeshwa somo la Hand Craft Majengo Middle School na Mwalimu anaitwa Fritz (sina hakika na "spelling").

Huu ulikuwa mwaka wa 1963.

Mwalimu Fritz alichukia sana mwanafunzi kuchora kisha akafuta.
Adhabu yake ni viboko papo kwa papo.

Athumani akafuta na akala mboko sote darasani tunashuhudia.
Athumani Mfinanga toka siku ile akawa Athumani Makufuta.

In Shaa Allah iko siku nitaandika kuhusu haya majina na kuwatafuta wahusika ili tucheke.
Nitaanza na "Toligogo" Omari Matola golikipa hodari amefariki miaka michache iliyopita.

Sote tulikuwa wanafunzi wa Mwalimu Juma darsa yake baina ya Maghrib na Isha Msikiti wa Ijumaa.
Jina hili ukimwita lilikuwa na staili yake maalum.

Unalitamka kama vile unaimba.

Rafiki yangu Allah amrehemu kila nilipokutananae iwe Dar es Salaam au Moshi Mtaa wa Chini akiniadhimisha kwa mapenzi makubwa.

Turudi kwa Omari Mwariko.

Omari Mwariko alinipa muda wake na alipoona namdadisi sana kuhusu kazi zake pale pale akanikaribisha nyumbani kwake Njoro ili anioneshe baadhi ya vinyago alivyokuwa amechonga.

Nilifika nyumbani kwake na akanionyesha kazi zake na akachukua muda kunifungulia maktaba aliyohifadhi picha zake toka ujana wake alipoanza kuchonga.
1612892923285.png
 
kama habari imeishia hewani mkuu,angalia vizuri rafiki yake makufuta.
 
Wote ni waislam tu. Wewe mtu na udini hufai mzee mwenzangu. Kuwa neutral angalau siku moja utaje na budha au mpagani
sijaona ubaya katika hili ko ilitakiwa wawepo na wakristu na wapagani hata kama hawahusiki na kisa kinacho simuliwa
 
Wote ni waislam tu. Wewe mtu na udini hufai mzee mwenzangu. Kuwa neutral angalau siku moja utaje na budha au mpagani.
Kolola,
Mzee mwenzangu.

Nadhani umesoma na kuona kuwa hizo ni kumbukumbu zangu nikiwa mtoto wa miaka 10 hadi 12 kiasi.

Naeleza yale ambayo nimepitia na hawa niliowataja ndiyo walikuwa wenzangu.

Sasa mzee mwenzangu unaniambia mbona sijaweka Mabudha na Wapagani.

Labda nikufahamishe.

Mimi katika umri wangu wote si hapa nyumbani wala si nje ya mipaka yake na nimezunguka sana dunia, sijakutana na mpagani ukimtoa Mzee Ngombale Mwiru.

Kwani wewe unakereka kusoma majina ya Kiislam?

Yanakuudhi huyapendi?
 
Kolola,
Mzee mwenzangu.

Nadhani umesoma na kuona kuwa hizo ni kumbukumbu zangu nikiwa mtoto wa miaka 10 hadi 12 kiasi.

Naeleza yale ambayo nimepitia na hawa niliowataja ndiyo walikuwa wenzangu.

Sasa mzee mwenzangu unaniambia mbona sijaweka Mabudha na Wapagani.

Labda nikufahamishe.

Mimi katika umri wangu wote si hapa nyumbani wala si nje ya mipaka yake na nimezunguka sana dunia, sijakutana na mpagani ukimtoa Mzee Ngombale Mwiru.

Kwani wewe unakereka kusoma majina ya Kiislam?

Yanakuudhi huyapendi?
Haiwezekani mtu mzima mwenzangu kila story hapa JF ni waislam tu. Akina Sykes etc tu.
 
Maalim Mohammed Said

Umewataja watu wote nawafahamu sana.
Kuanzia mwariko
Athumani Upepo
Mwalimu Juma(allah amrehemu akisomesha darsa masjid riadha na kisha kuhamia masjid ijumaa).Tho

Utakuwa unanifahamu fika kwa wazee wangu nikiishi somali street opposite na Masjid Riadha.
Thomas...
Nitakuwa nakujua na wewe ukiniona utanikumbuka.

Nimefurahi kuwa umenishuhudia kuwa hao niliowataja ndiyo walikuwa watoto walioishi hapo Moshi miaka hiyo nami nikiwa mmoja wapo pamoja na wewe.
 
Thomas...
Nitakuwa nakujua na wewe ukiniona utanikumbuka.

Nimefurahi kuwa umenishuhudia kuwa hao niliowataja ndiyo walikuwa watoto walioishi hapo Moshi miaka hiyo nami nikiwa mmoja wapo pamoja na wewe.
Mimi na wewe tukifahamiana vizuri sana kuna wakati nilikuwa na namba yako ya airtel ila niliipoteza.

Kwa umri bila shaka wewe wawafahamu vizuri wazee wangu.
Mimi nimekuja kukufamu nikisoma shule na kusoma vitabu vyako sikuwahi kudhani kuwa uliwahi ishi moshi na kuifahamu vizuri hivi tena na watu wake.

Nilikuja kujua siku ulipowataja baadhi ya jamaa za wazee wangu.
Wakina yusuph olotu(tukiishi mtaa mmoja nyumba ya 3 kutoka kwetu) na Bi Halima Selengi akiitwa shangazi mtaa wa liwali street allah awarehemu.
 
Mimi na wewe tukifahamiana vizuri sana kuna wakati nilikuwa na namba yako ya airtel ila niliipoteza.

Kwa umri bila shaka wewe wawafahamu vizuri wazee wangu.
Mimi nimekuja kukufamu nikisoma shule na kusoma vitabu vyako sikuwahi kudhani kuwa uliwahi ishi moshi na kuifahamu vizuri hivi tena na watu wake.

Nilikuja kujua siku ulipowataja baadhi ya jamaa za wazee wangu.
Wakina yusuph olotu(tukiishi mtaa mmoja nyumba ya 3 kutoka kwetu) na Bi Halima Selengi akiitwa shangazi mtaa wa liwali street allah awarehemu.
Thomas Sankara,
Hakika nitakuwa nawafahamu.
 
Basi wewe ni Mdini. Hakuna Mtanzania ambaye ana miaka zaidi ya 50 hajahusiana na watu was dini tofauti bwashee
Huyu mzee ana hidden agenda ambayo ipo pia ndani ya koran!

Ni kwamba anasimulia masimulizi ya watu weusi wenye majina ya kiarabu katika masuala mengine kabisa na ndani yake lazima ukutane na maneno matatu au zaidi ya imani yake!

Mfano; Msikiti, allah, inshallah, n.k yote hii ni kujaribu kuwafanya watu wasio wa hiyo imani waamini jambo juu ya hiyo imani yake.

Ameeleza kuwa hao ni wenzake! Kiongozi ungeshituka kuanzia hapo Koran inaeleza wazi kabisa kuwa ndugu wa mwisilam ni mwisilam mwenzake, na huyu mzee (mweusi kutoka Tanzania) amechukua itikadi za kiarabu na kiislamu na kuzifanya ni sehemu yake.
 
Huyu mzee ana hidden agenda ambayo ipo pia ndani ya koran!

Ni kwamba anasimulia masimulizi ya watu weusi wenye majina ya kiarabu katika masuala mengine kabisa na ndani yake lazima ukutane na maneno matatu au zaidi ya imani yake!

Mfano; Msikiti, allah, inshallah, n.k yote hii ni kujaribu kuwafanya watu wasio wa hiyo imani waamini jambo juu ya hiyo imani yake.

Ameeleza kuwa hao ni wenzake! Kiongozi ungeshituka kuanzia hapo Koran inaeleza wazi kabisa kuwa ndugu wa mwisilam ni mwisilam mwenzake, na huyu mzee (mweusi kutoka Tanzania) amechukua itikadi za kiarabu na kiislamu na kuzifanya ni sehemu yake.
Loftins,
Huwa nikisoma sentensi inaanza na ''Huyu Mzee,'' uzoefu umenifunza kuwa mwandishi kaghadhibika.
Mimi si mtaalamu wa Qur'an elimu yangu yote ni ya sekula.

Huwa nacheka sana hapa kwa kupewa nembo ambayo si yangu.
Kwa ajili hii siwezi hapa kujadili chochote katika chembelecho, ''hidden aganda.''

Kuwa itikadi ya Kiarabu na Kiislam kuwa ndiyo yangu hili vipi nitakukatalia wakati mimi jina langu ni Mohamed Said Salum Abdallah.

Dini yangu Muislam na kabila yangu ni Mmanyema kabila ambalo ni shida kukuta asiye Muislam ndani yake.
Nimezaliwa Dar es Salaam ya 1950 tena Mtaa wa Kipata Gerezani.

Kabla kuanza darasa la kwanza nimepelekwa madrasa kusoma Qur'an.
Vipi kwa malezi na makuzi haya nitakuwa vinginevyo?

Huyu ndiyo mimi.

Ikiwa wewe unaona hili ni kosa ningekuwa kama wewe na jina la Kizungu na hulka za Kizungu hii ni bahati mbaya sana kwako.

Nimeishi na Wazungu na nimefanyakazi na Wazungu ndani ya Tanzania na nje ya mipaka yake sikuona wao kutaabika na jinsi nilivyo kwa hulka zangu, jina langu na mambo kadha wa kadha.

Nifahamishe nini kinachokukera wewe kuhusu Mohamed Said.
 
Wote ni waislam tu. Wewe mtu na udini hufai mzee mwenzangu. Kuwa neutral angalau siku moja utaje na budha au mpagani.
Hebu ficha upumbavu wako, hakuna unachotaka kukipandikiza hapo
 
Mzee wangu nimemjua mzee mwariko tokea nikiwa mdogo mwaka 84-85 alikua maarufu sana na alishamchongea baba wa taifa kifimbo chake

Mzee mwariko yupona amejaribu mara kadhaa kupata nafasi ya kuwa mbunge wa moshi mjini kupitia ccm ila hakupata nafasi....

ukimtaja unanikumbusha utoto wangu...Mtaa wa Kenyata street, nikienda mtaa wa chini kuzurura na kuchungulia wakicheza ngoma kwa mzee mwariko...


MUNGU AMBARIKI...NA AKUBARIKI
 
Back
Top Bottom