Ombi la kibali kwa wahitimu wa kozi ya diploma in pipe works oil an gas engineering kuomba nafasi za ajira za ufundi bomba

Ombi la kibali kwa wahitimu wa kozi ya diploma in pipe works oil an gas engineering kuomba nafasi za ajira za ufundi bomba

Joined
Oct 3, 2022
Posts
5
Reaction score
3
Kwa:
Katibu Mkuu,
Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
S.L.P 2483,
Dodoma.

YAH: OMBI LA KIBALI KWA WAHITIMU WA KOZI YA DIPLOMA IN PIPE WORKS OIL AND GAS ENGINEERING KUOMBA NAFASI ZA AJIRA ZA UFUNDI BOMBA

Ndugu Katibu Mkuu,

Kwa heshima na taadhima, mimi ni mwakilishi wa wahitimu wa kozi ya Diploma in Pipe Works Oil and Gas Engineering, ambao tumehitimu mafunzo yetu katika vyuo vya Arusha Technical College na NIT. Kupitia tangazo rasmi la ajira za serikali lililotolewa hivi karibuni, tumebaini kwamba zipo nafasi za ajira za Fundi Bomba ambazo zinaendana moja kwa moja na ujuzi na mafunzo tuliyopata.

Hata hivyo, kwa mujibu wa vigezo vilivyowekwa kwenye tangazo hilo la tarehe 13 desemba 2024 kuna hitaji la kupata kibali kutoka kwa Ofisi yako tukufu ili tuweze kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kuomba nafasi hizo za ajira. Tunatambua umuhimu wa kufuata taratibu zote za ajira za serikali na tuko tayari kushirikiana kikamilifu ili kuhakikisha tunapata nafasi ya kutumia ujuzi wetu kuchangia maendeleo ya taifa.

Kwa msingi huo, tunakuomba kwa heshima ukubali ombi letu na kutoa kibali kinachohitajika ili sisi wahitimu wa kozi hii tuweze kushiriki katika mchakato wa kuomba nafasi za Fundi Bomba kama ilivyotangazwa. Tuna imani kuwa ujuzi wetu katika Pipe Works Oil and Gas Engineering utachangia kwa kiasi kikubwa kufanikisha miradi mbalimbali inayohusiana na sekta ya maji,mafuta na gesi nchini.

Taarifa zote za Kozi hii zinapatikana Chuo cha Ufundi Arusha.
 
Kwa:
Katibu Mkuu,
Ofisi ya Rais,
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora,
S.L.P 2483,
Dodoma.

YAH: OMBI LA KIBALI KWA WAHITIMU WA KOZI YA DIPLOMA IN PIPE WORKS OIL AND GAS ENGINEERING KUOMBA NAFASI ZA AJIRA ZA UFUNDI BOMBA

Ndugu Katibu Mkuu,

Kwa heshima na taadhima, mimi ni mwakilishi wa wahitimu wa kozi ya Diploma in Pipe Works Oil and Gas Engineering, ambao tumehitimu mafunzo yetu katika vyuo vya Arusha Technical College na NIT. Kupitia tangazo rasmi la ajira za serikali lililotolewa hivi karibuni, tumebaini kwamba zipo nafasi za ajira za Fundi Bomba ambazo zinaendana moja kwa moja na ujuzi na mafunzo tuliyopata.

Hata hivyo, kwa mujibu wa vigezo vilivyowekwa kwenye tangazo hilo la tarehe 13 desemba 2024 kuna hitaji la kupata kibali kutoka kwa Ofisi yako tukufu ili tuweze kushiriki kikamilifu katika mchakato wa kuomba nafasi hizo za ajira. Tunatambua umuhimu wa kufuata taratibu zote za ajira za serikali na tuko tayari kushirikiana kikamilifu ili kuhakikisha tunapata nafasi ya kutumia ujuzi wetu kuchangia maendeleo ya taifa.

Kwa msingi huo, tunakuomba kwa heshima ukubali ombi letu na kutoa kibali kinachohitajika ili sisi wahitimu wa kozi hii tuweze kushiriki katika mchakato wa kuomba nafasi za Fundi Bomba kama ilivyotangazwa. Tuna imani kuwa ujuzi wetu katika Pipe Works Oil and Gas Engineering utachangia kwa kiasi kikubwa kufanikisha miradi mbalimbali inayohusiana na sekta ya maji,mafuta na gesi nchini.

Taarifa zote za Kozi hii zinapatikana Chuo cha Ufundi Arusha.
Ni sahihi kabisaa huagaa nashangaaa saana wanahitajii mtu aliyesoma diploma ya civil engineering wakatii waliosoma pipes,oil and gas nilikuaga nawaona pale arushaa tech ndio walikuwa wanachezea pipes kila siku na kufanya mambo yote ya plumbing yaanii kiufupii watu wa pipes,oil and gas wapo very competent kwenye plumbing than aliyesoma civil
 
Ulipokuwa unasoma hiyo course haukuambiwa inakuwa applied wapi???yamkini huko haifiti mkuu!! Mfano mtu aliyesoma mechanical engineering na civil engineering upande wa diploma kwenye michoro mtu wa mechanical yupo vizuri kuliko civil lakini tangazo la kwenda kufundisha veta technical drawing wanamtaka mtu wa Civil! Kwa hiyo ni utaratibu wa serikali nafikiri ombi lako limefika litafanyiwa kazi! Maana ukisema hivyo maanake na mtu aliyesoma chuo cha maji dar es salaam upande wa diploma ndiye yupo vizuri zaidi kuliko nyinyi wote kwenye upande wa plumbing & pipe fitting! Kuna vyitu vinamis kwenye kozi yako ndo maana hawawahitaji kwenye tangazo lao
 
Back
Top Bottom