Ombi la Mbolea ya ruzuku kwa wakulima wa mijini (Urban farming)

Ombi la Mbolea ya ruzuku kwa wakulima wa mijini (Urban farming)

lutajangurwa

Senior Member
Joined
Sep 21, 2019
Posts
126
Reaction score
172
Majuzi nilienda kununua mbolea kwenye Kampuni ya mbolea ETG. Nikaambiwa, mbolea zote zimeandikwa RUZUKU. Hakuna nafasi ya kupata mbolea kwa njia nyingine yoyote.

Ikumbukwe kwamba, wapo wakulima wengi wanaolima mijini. Hawa viwango vya mbolea wanavyotumia ni kiasi kidogo tu. Lakini wamesahaulika. Mbaya zaidi, hakuna tena uwezekano wa kupata mbolea kama wewe siyo wa kijijini. TUNAOMBA Waziri alione hili.

Namuomba mheshimiwa Waziri, kama hakuna uwezekano wa wakulima wa mijini kupata mbolea ya ruzuku, basi lifunguliwe dirisha dogo kwa ajili ya bei za kawaida. Hili dirisha kwa sasa limefungwa kabisa. Tutaponea wapi?

Ni muhimu kwa Waziri kujua kwamba, hizi mbogamboga na matunda kwenye masoko mengi ya mjini, vinalimwa mjini au pembezoni mwa miji. Kuna wajasiriamali wa maua, nao pia ni wengi wanaotumia mbolea. Tunaomba tusaidiwe ili huduma hii iendelee.
 
Mijini sio pa kilimo!

Mfano unalimaje mjini, Hilo shamba hata ekari tano lipo wapi huko mjini.

Kilimo tiachie site was huku mikoani...pia msimu wa njaa sijaona mahindi yakigawiwa mjin ni huku huku shamba
 
Majuzi nilienda kununua mbolea kwenye Kampuni ya mbolea ETG. Nikaambiwa, mbolea zote zimeandikwa RUZUKU. Hakuna nafasi ya kupata mbolea kwa njia nyingine yoyote.

Ikumbukwe kwamba, wapo wakulima wengi wanaolima mijini. Hawa viwango vya mbolea wanavyotumia ni kiasi kidogo tu. Lakini wamesahaulika. Mbaya zaidi, hakuna tena uwezekano wa kupata mbolea kama wewe siyo wa kijijini. TUNAOMBA Waziri alione hili.

Namuomba mheshimiwa Waziri, kama hakuna uwezekano wa wakulima wa mijini kupata mbolea ya ruzuku, basi lifunguliwe dirisha dogo kwa ajili ya bei za kawaida. Hili dirisha kwa sasa limefungwa kabisa. Tutaponea wapi?

Ni muhimu kwa Waziri kujua kwamba, hizi mbogamboga na matunda kwenye masoko mengi ya mjini, vinalimwa mjini au pembezoni mwa miji. Kuna wajasiriamali wa maua, nao pia ni wengi wanaotumia mbolea. Tunaomba tusaidiwe ili huduma hii iendelee.
Sijaelewa, yaani mbolea zote zimewekewa RUZUKU? Hata km mtu hutaki mbolea ambayo INA ruzuku huwezi kuuziwa ambayo haina? Au huu mfumo ukoje?
 
Sijaelewa, yaani mbolea zote zimewekewa RUZUKU? Hata km mtu hutaki mbolea ambayo INA ruzuku huwezi kuuziwa ambayo haina? Au huu mfumo ukoje?
Ndo maana ake japo hata hiyo ya ruzuku kuipata ni kasheshe siasa tupu!
 
Back
Top Bottom