Ommy Dimpoz taabani akimbizwa Ujerumani

Madimba jr

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2017
Posts
1,577
Reaction score
3,146
Dimpoz anasumbuliwa na koo ambapo katikati ya mwaka huu 2018 alifanyiwa operation katika moja ya hospitali kubwa nchini Afrika ya Kusini,licha ya kuonekana kuimarika kwa afya yake miezi kadhaa iliyopita lakini tatizo hilo limemrudia tena siku chache za hivi karibuni.awali kabla ya kwenda kupatiwa tiba South Afrika, madaktari wa muhimbili walimueleza kuwa ana dalili za kansa ya koo,jambo ambalo hakukubaliana nalo.
Dua za Watanzania zinahitajika kwa kijana wetu Ommy
 
Mungu amponye arejee kwenye majukumu yake!
 
Mungu ni mwingi wa Rehma,, InshaAllah Allah amfanyie wepesi.
 
Sema uzuri wa Hospital Za Bongo mtu Unaambiwa Ukweliii ila ukienda Nje lazima Wakudanganye danganye ili wakupige Hele Foreigner hadi zikiwa zinataka kuisha wanakwambia Una Ca ila Cancer ya Koo TZ rate yake imekuwa Kubwa sana Hasa kwa Vijana Umri wa Ommy ngoja tusubiri na Tuone
 
Sigara
 
Siyo kweli kuwa hospitali za nje zinadanganya wagonjwa mzee wangu; hospitali za nje kama marekani wanakuambia na ile habari usiyotaka kujua. Wanaweza kukuambia wazi kuwa utakufa ndani ya siku tatu, kwa hiyo kama hujaweka wosia kuhusu mali zako sema wakupe wanasheria kukusaidia harak haraka kuweka wosia kabla hujaaga dunia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…