Ongeza ukubwa wa storage kwenye Flash yako

Ongeza ukubwa wa storage kwenye Flash yako

Teknolojia ni Yetu sote

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2020
Posts
620
Reaction score
1,240
Hivi unajua unaweza kuongeza nafasi kwenye sd card (memory card) au flash drive kupitia kompyuta ๐Ÿ˜€!! Najua una shangaa relax ๐Ÿ˜

1_20241106_004330_0000.png


Kuna program Moja ukifanikiwa kuwa nayo inakupa Uwezo wa kuongeza nafasi kwenye memory card yako (pendrive) ukubwa unaotaka.

Program iyo inaitwa SData Tools hii ni software itakayokusaidia kuongeza nafasi kwenye memory card yako kwa ukubwa mbalimbali wa flash yako kama ifuatavyo
โ€ข 2Gb kwenda 4Gb
โ€ข 4Gb kwenda 8Gb
โ€ข 8Gb kwenda 16Gb
โ€ข 16Gb kwenda 32Gb nk

2_20241106_004331_0001.png


Program hii inaongeza nafasi kwenye memory bila kuhalibu mfumo wowote uliopo kwenye pendrive yako (Sd card au flash) kwa asilimia ๐Ÿ’ฏ

Unafanyaje Sasa ๐Ÿ˜œ.........๐Ÿƒโ€โ™‚๏ธ
๐Ÿ‘‰ Pakua software inayoitwa SdAta tools kwenye kompyuta yako link hii ๐Ÿ‘‡ SdAta 4.3Mb


3_20241106_004331_0002.png


๐Ÿ‘‰ Ukimaliza sasa utaweza ku extract file lako maana liko kwa mfumo wa Zip Kisha utafungua na ku run file lako sdatatools.exe kupitia run as administrator
๐Ÿ‘‰ Sehemu ya choose data to compress utaweza kuchagua flash yako ni ipi kama Herufi yake ni E,G,H nk
๐Ÿ‘‰ Kwenye data size chagua unataka kuongeza ukubwa gani mfano kama flash yako ni 4Gb weka 8Gb

Ukimaliza bonyeza E compress now utaweza kuongeza ukubwa flash yako. Inafanya kazi kuanzia window 2000 mpaka window 11 โœ…
 
Nimeona ila huu ni uzushi tu may be hiyo software inauwezo wa kucompress file la 4mb to 2mb na kukupa nafasi ya kustore more thing ila haiongezi ukubwa

ingekuwa inawezekana hivyo basi mchina asingetengeneza flash fake angenunu original ya gb4 au 2 akaiextend to 8 au 16 then akauza cheap

Anyway nitafatilia na kuleta majibu
 
Itaonesha tu kwenye computer size kubwa ila haitapokea mafile makubwa kushinda size yake. Kama ni flash ya 2GB umeongeza hadi 4GB ukiweka file la 3GB itakakataa.
Mkuu nimetafuta uzi wako wa vifaa vya intel sijauona.. naomba ufafanuzi juu ya hii pc, vipi processor yake imekaaje? Unaionaje hasa kwa matumizi heavy ya engineering?
 

Attachments

  • Screenshot_20241113_111828_WhatsApp.jpg
    Screenshot_20241113_111828_WhatsApp.jpg
    219.6 KB · Views: 10
acha kudanganya, hiyo program inapunguza ukubwa wa file, kama ilivyo ile program ya Big_Mp3_to_small.
 
Mkuu nimetafuta uzi wako wa vifaa vya intel sijauona.. naomba ufafanuzi juu ya hii pc, vipi processor yake imekaaje? Unaionaje hasa kwa matumizi heavy ya engineering?
Processor nzuri ila inategemea na bei yake, hii processor sio mpya ni rebrand ya same core kuanzia gen ya 12/13 kwa bei chini ya 1.5M sio mbaya ila kama inafika 1.5M kupanda kuna processor nzuri zaidi.
 
Processor nzuri ila inategemea na bei yake, hii processor sio mpya ni rebrand ya same core kuanzia gen ya 12/13 kwa bei chini ya 1.5M sio mbaya ila kama inafika 1.5M kupanda kuna processor nzuri zaidi.
Nakumbuka kuna siku ulisema processor ikiwa na digit 4 ndio nzuri na ukasema ikiwa na letter U sio nzuri. Inanichanganya kidogo
 
Mtoa post kama hujatoka kanda ya ziwa nakulipa ..haya sema...kinehe
 
Nakumbuka kuna siku ulisema processor ikiwa na digit 4 ndio nzuri na ukasema ikiwa na letter U sio nzuri. Inanichanganya kidogo
Zamani mkuu intel gen ya 1 mpaka 13 na processor za Amd ilikua rahisi kabisa kujua generation na uwezo wa processor, gen ya 2 ilikua 2000 series gen ya 8 8000 series gen ya 12 ni 12000 series etc. Kuanzia gen ya 14 ni kama wameambizana wote intel na Amd wame rename processor zao majina yapo shaghala baghala hata mimi nikiona cpu husika hadi ni google kujua exactly ni gen ya ngapi, in short wanafanya makusudi ili average user asijue.

So kwa uhakika zaidi Tumia website ya Notebookcheck Google Jina la cpu ikifuatiwa na neno notebookcheck


Hapo utapata details zote za Cpu husika na uwezo wake.

Ila ndio kama nilivyokwambia juu kwa hio cpu angalia bei, i5 11600H ambayo ni gen ya 11 ina perfomance sawa na hio, na siku hizi gen ya 11 mtumba unapata chini ya 1M na hata mpya hazichezi mbali.
.
 
Back
Top Bottom