Ongezeko la 2% ya Pensheni kwa wastaafu ni kejeli ya karne

Ongezeko la 2% ya Pensheni kwa wastaafu ni kejeli ya karne

danimutta

JF-Expert Member
Joined
Nov 4, 2011
Posts
273
Reaction score
351
Wastaafu kote nchini tumeshtushwa sana na tangazo la ongezeko ya pensheni kwa asilimia 2% kuanzia 2025 lililotangazwa na Waziri Kikwete (jnr).

Itakumbukwa kwamba ongezeko hili kiduchu kwa rekodi linafanyika baada ya kupita karibu miaka 10 i.e. enzi za Rais Kikwete na Waziri Mkuya walipoongeza pensheni kwa wastani wa asilimia 26% mwaka 2015!

Pengine Waziri Kikwete na Katambi kutokana na umri wao mdogo hawajui changamoto za wastaafu ambao kwa sasa kima cha chini ni laki 1 au hawajishughulishi hata kusoma historical trends za maboresho ya pensheni.

Mathalani miaka ya 2003 na 2009 serikali za wakati huo ziliboresha pensheni (kima cha chini) kwa asilimia 50% na 77% respectively!

Sasa huu uamuzi wa nyongeza ya asilimia 2% katika kipindi cha Rais wetu mpendwa Mama Samia unaingia akilini kweli?

Hakika huu ni uamuzi wa kuhujumu sifa nzuri ya serikali ya sasa. Ina maana mstaafu anayelipwa laki 1 sasa ataambulia tshs. 102,000/=!. Mungu ibariki Tanzania.
 
Nashawishika kuamini kwamba Waziri alitamka vibaya tungemwomba arejee kutamka nyongeza ya pension kwa wastaafu badala ya hiyo 2% vinginevyo ni chukizo kwa wazee walilitumikia Taifa kizalendo.Walioajiriwa kipindi cha Mwalimu;waliohai wako ktk hali mbaya
 
Wastaafu kote nchini tumeshtushwa sana na tangazo la ongezeko ya pensheni kwa asilimia 2% kuanzia 2025 lililotangazwa na Waziri Kikwete (jnr). Itakumbukwa kwamba ongezeko hili kiduchu kwa rekodi linafanyika baada ya kupita karibu miaka 10 i.e. enzi za Rais Kikwete na Waziri Mkuya walipoongeza pensheni kwa wastani wa asilimia 26% mwaka 2015! Pengine Waziri Kikwete na Katambi kutokana na umri wao mdogo hawajui changamoto za wastaafu ambao kwa sasa kima cha chini ni laki 1 au hawajishughulishi hata kusoma historical trends za maboresho ya pensheni. Mathalani miaka ya 2003 na 2009 serikali za wakati huo ziliboresha pensheni (kima cha chini) kwa asilimia 50% na 77% respectively! Sasa huu uamuzi wa nyongeza ya asilimia 2% katika kipindi cha Rais wetu mpendwa Mama Samia unaingia akilini kweli? Hakika huu ni uamuzi wa kuhujumu sifa nzuri ya serikali ya sasa. Ina maana mstaafu anayelipwa laki 1 sasa ataambulia tshs. 102,000/=!. Mungu ibariki Tanzania.
Tangazo lenyewe liko wapi? Labda alimaanisha 20%
 
Wastaafu kote nchini tumeshtushwa sana na tangazo la ongezeko ya pensheni kwa asilimia 2% kuanzia 2025 lililotangazwa na Waziri Kikwete (jnr).

Itakumbukwa kwamba ongezeko hili kiduchu kwa rekodi linafanyika baada ya kupita karibu miaka 10 i.e. enzi za Rais Kikwete na Waziri Mkuya walipoongeza pensheni kwa wastani wa asilimia 26% mwaka 2015!

Pengine Waziri Kikwete na Katambi kutokana na umri wao mdogo hawajui changamoto za wastaafu ambao kwa sasa kima cha chini ni laki 1 au hawajishughulishi hata kusoma historical trends za maboresho ya pensheni.

Mathalani miaka ya 2003 na 2009 serikali za wakati huo ziliboresha pensheni (kima cha chini) kwa asilimia 50% na 77% respectively!

Sasa huu uamuzi wa nyongeza ya asilimia 2% katika kipindi cha Rais wetu mpendwa Mama Samia unaingia akilini kweli?

Hakika huu ni uamuzi wa kuhujumu sifa nzuri ya serikali ya sasa. Ina maana mstaafu anayelipwa laki 1 sasa ataambulia tshs. 102,000/=!. Mungu ibariki Tanzania.
Sasa viongozi ninyi mnaona maslahi yenu na wanasiasa wastaafu ndiyo MAISHA pekee ?. HAYA ! "Eeh MUNGU ingilia hali hii". Amina.
 
Mwenye shibe hamjui mwenye njaa, haswa akiwa na roho ya ulafi.

Yeye mtoto waziri, baba raisi mstaafu, mama mbunge, na bado mama yake akapeleka wazo la wenza wa wastaafu kulipwa sijui 70% ya kile wanacholipwa waume zao. Kifupi familia moja inachota 170%.. Baba analipwa mwanamama analipwa.
Hawajui bei ya mafuta, hawanunui maharage.
Yeye halipi maji, umeme, kodi ya nyumba.. Ye kila kitu ni mseleleko, mara ya mwisho yeye kama yeye kununua sukari dukanj hakumbuki, unategemea nini.
 
Wastaafu wa mfuko wa NSSF hawakulipwa nyongeza ya 2% mwezi January 2025 kama bungee na Serikali walivyotangaza.
 
Waziri Ridhawan Kikwete,tunaomba ufafanuzi kwa nini wastaafu wa sekta binafsi na watumishi wa Serikali wa operational service ambao walikuwa wanachangia mfuko wa NSSF hawakulipwa nyongeza ya 2% ya pension zao kama ulivyolipwa wenzao wa PSSSF.
Michango ya watumishi wa umma na sekta binafsi kwenye mifuko ya hifadhi za jamii ni amana yao na wote walipe bila ubaguzi.
Chama cha Mapinduzi hakipaswi kufumbia macho kwa maanaewatumishi wao wanachangia NSSF.
Serikali ya CCM inawadhulumu vipi watendaji wake.
Mamlaka husika zilipe nyongeza hiyo kwa watumishi wa sekta binafsi, vyama vya siasa na wahudumu wa serikalini ambao ni wanachama wa NSSF
 
Wastaafu kote nchini tumeshtushwa sana na tangazo la ongezeko ya pensheni kwa asilimia 2% kuanzia 2025 lililotangazwa na Waziri Kikwete (jnr).

Itakumbukwa kwamba ongezeko hili kiduchu kwa rekodi linafanyika baada ya kupita karibu miaka 10 i.e. enzi za Rais Kikwete na Waziri Mkuya walipoongeza pensheni kwa wastani wa asilimia 26% mwaka 2015!

Pengine Waziri Kikwete na Katambi kutokana na umri wao mdogo hawajui changamoto za wastaafu ambao kwa sasa kima cha chini ni laki 1 au hawajishughulishi hata kusoma historical trends za maboresho ya pensheni.

Mathalani miaka ya 2003 na 2009 serikali za wakati huo ziliboresha pensheni (kima cha chini) kwa asilimia 50% na 77% respectively!

Sasa huu uamuzi wa nyongeza ya asilimia 2% katika kipindi cha Rais wetu mpendwa Mama Samia unaingia akilini kweli?

Hakika huu ni uamuzi wa kuhujumu sifa nzuri ya serikali ya sasa. Ina maana mstaafu anayelipwa laki 1 sasa ataambulia tshs. 102,000/=!. Mungu ibariki Tanzania.
 

Attachments

  • images (93).jpeg
    images (93).jpeg
    38.2 KB · Views: 4
Back
Top Bottom