Ongezeko la mishahara Vs makato ya miamala, kuna shida mahali

Ongezeko la mishahara Vs makato ya miamala, kuna shida mahali

NEWSINKP

Member
Joined
Sep 26, 2016
Posts
77
Reaction score
92
Watanzania nawasalimu,

Nimejaribu kuwaza ni wapi tunakoelekea nimekosa majibu. Viongozi wetu na watanzania wote ni mashuhuda kuwa tumeambiwa kuwa kuhusu nyongeza ya mishahara tusubiri uchumi uimarike kidogo.

Lakini Leo hii huyu huyu mtu anaeomba kuongezewa mshahara kutokana na kuongezeka kwa garama za maisha Leo hii anatakiwa tena achangie uchumi kupitia miamala anayofanya.

Binafsi nilifikiri mtu anapaswa kuongezewe kipato ili aweze kuchangia uchumi na si kuchangia uchumi akiwa na hali ngumu ya maisha ili aje aongezewe kipato.

Watanzania tunapaswa kujitafakari sana juu ya uongozi tunaoutaka. Nafkiri wawakilishi wetu hawajali chochote kuhusu maisha yetu. Hivi mtu anaekulilia umuongezee mshahara, unamuongezeaje gharama tena na hata hujamuongezea huo mshahara? Huoni kua unamuongezea ugumu wa maisha zaidi?
 
Hivi hawa wanasiasa wao unadhani wanaona uchungu wowote? Mtu ana mishahara zaidi ya miwili bado hajafanya ufisadi, safari kila siku, posho za vikao, nyumba bure, usafiri ma vieite.

Atajua uchungu wako kapuku wa Nadonjuki?
 
Inasemekana tatizo siyo kipato, tatizo ni katiba mpya ambayo wananchi wako tayari hata kuchangia.

Kwahiyo wananchi kwao pesa siyo tatizo.

Nadhani tatizo ni kwamba hawataki tu kuchangia serikali, ila kuchangia wengine huwa wanachanga bila vinyongo. Mzushi Yericko Nyerere alichangiwa milioni 7 ndani ya dakika 5, Mtukanaji Mdude alipewa milioni 10 ndani ya dakika 30🤣

Kwahiyo CHANGIENI maendeleo ya nchi yenu hata kwa LAZIMA maana kwa hiari HAMTAKI.
 
Inasemekana tatizo siyo kipato, tatizo ni katiba mpya ambayo wananchi wako tayari hata kuchangia.

Kwahiyo wananchi kwao pesa siyo tatizo...
Hawa walichangiwa mara 1 tuu, ila hili la miamala unaweza changia hata mara 10 kwa siku kuzingatia na idadi ya miamala utakayofanya kwa siku na ni for the rest of your life labda mpaka mabadiliko yatakapofanyika.
 
Wakati mjuba anawaambia akiongeza mishahara itaripua mfumuko wa bei, mlimwona hayawani aliyevuta bangi.

Malipo ni hapa hapa duniani ndugu zangu.
Kuna vitu ni basic kabisa wala havihitaji usome sana. Mishahara mlima itatoka wapi??
Sent from my INE-LX1r using JamiiForums mobile app
 
Ni kwenda mahakamani kufungua kesi kupinga huu ushenzi ndo njia iliyobaki.
 
Hivi hawa wanasiasa wao unadhani wanaona uchungu wowote? Mtu ana mishahara zaidi ya miwili bado hajafanya ufisadi, safari kila siku, posho za vikao, nyumba bure, usafiri ma vieite.

Atajua uchungu wako kapuku wa Nadonjuki?
Unakuta mtu ni mbunge halafu hapo hapo ni waziri anakunja almost 20M kwa mwezi bado marupurupu 😅😅😅 house allowance, transport pamoja na communication!

Hawazi ada watoto million 8 ya ada yao ni uhakika wengine wanasomesha shule za 18M per year! Mtu huyu kweli hayo makato ya elfu 20 yanamuathiri vipi maana he makes a lot of money more than what he needs to spend!
 
hapo tayari umesha changia mwanao au mtoto wa ndugu yako akapate elimu bora, pia umesaidia ndugu yako popote alipo apate huduma bora hospitalini.
usijutie makato hayo, utafurahia huduma za afya, elimu na barabara.
mjenga nchi ni mwananchi, tujenge nchi yetu.
 
Watanzania nawasalimu,

Nimejaribu kuwaza ni wapi tunakoelekea nimekosa majibu. Viongozi wetu na watanzania wote ni mashuhuda kua tumeambiwa kuwa kuhusu nyongeza ya mishahara tusubiri uchumi uimarike kidogo....
Watunga sera wao wanalipiwa kila kitu mfumo wa hovyo kabisa, hawajui ugumu wa maisha wa watu wengine.
 
hii sasa ndio kampeni mpya ya chadema baada ya kuona katiba mpya imekuwa ndoto za mchana.
ila chadema inazidi kujichafua zaidi kisiasa kwa kuhamasisha mambo ambayo ni kinyume na uzalendo, hakuna anaye shawishika na uhuni huu .
 
Unakuta mtu ni mbunge halafu hapo hapo ni waziri anakunja almost 20M kwa mwezi bado marupurupu 😅😅😅 house allowance, transport pamoja na communication!

Hawazi ada watoto million 8 ya ada yao ni uhakika wengine wanasomesha shule za 18M per year! Mtu huyu kweli hayo makato ya elfu 20 yanamuathiri vipi maana he makes a lot of money more than what he needs to spend!
Hahaha hapo mzee baba umesahau bado hajaiba. 😂😂😂
 
Watanzania nawasalimu,

Nimejaribu kuwaza ni wapi tunakoelekea nimekosa majibu. Viongozi wetu na watanzania wote ni mashuhuda kuwa tumeambiwa kuwa kuhusu nyongeza ya mishahara tusubiri uchumi uimarike kidogo.

Lakini Leo hii huyu huyu mtu anaeomba kuongezewa mshahara kutokana na kuongezeka kwa garama za maisha Leo hii anatakiwa tena achangie uchumi kupitia miamala anayofanya.

Binafsi nilifikiri mtu anapaswa kuongezewe kipato ili aweze kuchangia uchumi na si kuchangia uchumi akiwa na hali ngumu ya maisha ili aje aongezewe kipato.

Watanzania tunapaswa kujitafakari sana juu ya uongozi tunaoutaka. Nafkiri wawakilishi wetu hawajali chochote kuhusu maisha yetu. Hivi mtu anaekulilia umuongezee mshahara, unamuongezeaje gharama tena na hata hujamuongezea huo mshahara? Huoni kua unamuongezea ugumu wa maisha zaidi?
tuendelee kuisoma namba ccm ni ile ile
 
Si nasikia na nauli zimepanda huko. Daaaah
Ukisimama Nshale, Ukikaa Nshale, Ukiinama Nshale.
 
Back
Top Bottom