Ongezeko la wachambuzi wa soka kuliko kina "Samatta"

zandrano

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2017
Posts
7,893
Reaction score
8,816
Hivi karibuni kumekuwapo na ongezeko kubwa la wataalamu wa uchambuzi wa mpira wa miguu, vituo vyote vya luninga na radio stations zina wachambuzi ukiwasikiliza wote ni wanaonyesha weledi wa hali ya juu ktk kuchambua soka la ndani na nje. Kwa maoni yangu hatua hiyo ni jambo zuri tu halina shida, lakini sasa swali ambalo nimekuwa nikijiuliza;

1. Kwa nini sasa hatuzalishi wachezaji bora wenye viwango kama Samatta? Au weledi wetu unaishia mdomoni tu? Nchi nzima tuna football academies zisizozidi 8, je academies hizi zinajikita kufundisha wachambuzi wa soka kuliko wachezaji?

2. Ningetamani sana kuona wataalamu wa vitendo (wachezaji) zaidi kuliko wataalamu wa kuchambua au kuwe na uwiano sawa, yaani wataalamu wa uchambuzi na wachezaji bora.
 
Kwasababu Binadamu hawezi kutaga yai, je inamaanisha hajui / hawezi kuongelea yai bovu?

Pia unadhani kufika alipofika Samatta ni Talent pekee au kuna mengi yanatakiwa, The World is full of talented individuals with unfulfilled potential (attitude pia ina-matter) as well as being at the right place/team.
 
Ipo hivi....kuangalia na kuongea ni rahisi kuliko kucheza.
 
Ajira hakuna. Kila mmoja anajichomeka sehemu yoyote atakayoona atapata tonge kwa urahisi.

Bongo kila mtu mchambuzi, wengine hawana tu platform za kubwekea.

Tanzania Kila baada ya dakika 20 kuna kipindi cha michezo kwenye media. Hapo unategemea nini ??
 
Pia inapendeza mtu anaechambua mpira awe hata amecheza huo mpira unakuta wachambuzi wetu hata hawajawahi kucheza mpira, basi na sentesi za kuunga unga za kiingereza jamaa anajitta mchambuzi utawasikia huku wamebana pua " This Mancity Team is unplayable, fantastic " basi amemaliza uchambuzi. 🙁😡😡
 
Hao si wachambuzi wa soka, hao ni wasimuliaji wa habari za michezo
 
Wachambuzi wa michezo wapewe nafasi na wao ya kufundisha,ili tuone wanaweza.
"Zilongwa mbali zitendwa mbali"
Thiery Henry alikua ni mchambuzi anayelipwa zaidi...akapewa timu huko kwao Ufaransa inaitwa Monaco..kilichomkuta ni kutimuliwa kama si legend wa France yani.
 
Mkuu usihadaike na maneno ya hapo wachambuzi kama.

-- actually..

-- statistics.

-- combination.

-- defensive.

Hawana lolote zaidi ya maneno ya mdomoni,,.

Uchambuzi wa soka haswa kwa asiyekuwa mwanasoka ni mambo yanayotia shaka sn uwezo wao.

Wengi wao ni domo kaya,,lakini hawana weledi wowote wa uchambuzi..
 
Siku hizi wamekamata na neno "consistency" basi shida,mwingine analazimisha kulitumia sehemu unabaki unashangaa tu.
 
Nlivyobahatika kujiunga Form one

Nlitakiwa kuchagua kimoja Kuwa daVinci XV au kuwa kylia Mbappe , Jadon Sancho , Bamidele Ali na wengine wengi

Lakini kwakuwa samatta Ndiye Mchezaji peke wa Tz aliyefanikiwa kujaribu kugusa vilabu vya Ulaya Basi jibu lake mnalo nlichagua nini

Nadhani vijana wengi wa kibongo waliowahi kusakata kabumbu walikuwa na career kama yangu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…