Online Education Tanzania au Vyuo vya nje

Online Education Tanzania au Vyuo vya nje

newazz

JF-Expert Member
Joined
Mar 28, 2009
Posts
904
Reaction score
907
Ninahitaji kuelekezwa vyuo vinavyotoa online degree hapa Tanzania. Kama hakuna nahitaji vya nje. Niwekee websites nk.

Ninataka kufanya MBA, Logistics/ International Transport au maeneo mengine kadri ninavyoweza kupata options zaidi.

Nahitaji chuo ambao fees zao si kubwa ambazo mtanzania wa kawaida anaweza kumudu, yaani nilipe online education kama ambavyo ningelipa fees kwa kiwango cha pesa, kinachofanana na kama hiyo ingetolewa na chuo cha Tanzania kinachotoa elimu.

Lakini chuo viwe na vigezo vya elimu bora kama" quality of education,the accreditation of the institution etc.

Naomba msaada wa kuelekezwa vyuo hivyo na pengine unipe uzoefu wako wa kusoma online educationa ukiwa hapa Tanzania.
 
www.udsm.ac.tz
wanaatoa kozi za online katika kitengo chao cha Virtual education, japokuwa hajapanuka sana ila nafakili inawezekana kozi unazotaka zikawepo.
 
Asante Wafungo,

Nilikuwa nimewacheki hawa jamaa wa Virtual UD, deadline for application ilikuwa tarehe 05/March.

Sasa nitaenda kuwaona phyically, pale chuo .

Hawa virtual education, wapo eneo gani chuoni UD?
 
virtual education kwa pale UD wapo mkabala na Physics department katika Barabara ya Uvumbuzi.
 
Wafungo,

Nimekusoma, nitaitafuta hiyo barabara ya uvumbuzi.
Asante.

Wadau wengine , je hakuna mwenye jina la chuo , ambaye anasoma/ amesoma online education toka vyuo vya nje???
 
Check pia Liverpool University walikuwa na online MBA content yao ilikuwa nzuri saana.
 
Asante Anfaal,

Nitawacheki na hao.

Nimepata kuona hawa jamaa wa KIU ( Kampala International University)

Na wao wanatoa online MBA, je wadau vipi rating ya chuo hiki na MBA yake , kwa kiwango cha course content, je hii MBA inakubalika katika soko la elimu na ajira? Naomba mchango wenu wadau..
 
Asante Anfaal,

Nitawacheki na hao.

Nimepata kuona hawa jamaa wa KIU ( Kampala International University)

Na wao wanatoa online MBA, je wadau vipi rating ya chuo hiki na MBA yake , kwa kiwango cha course content, je hii MBA inakubalika katika soko la elimu na ajira? Naomba mchango wenu wadau..

Kwani mkuu wewe unaishi wapi?
Maana umepewa option ya UDSM hapo umeendelea kuomba vyuo,sasa unaongelea mambo ya KIU na huna uhakika nacho. Kwanini usiwasiliane na udsm hapo kabla hujaingia kwenye vyuo vinavyoibuka kama uyoga?
To my knowledge, value ya MBA inategemea pia na wapi umeisoma,sio kuwa na MBA ili mradi umepata MBA. KIU ni chuo ambacho baada ya kukosa nafasi za kwenda vyuo vingine vyote Uganda ndio wanaenda hapo. Wengi wanaosoma chuo kile ni watu toka nje ya nchi,hasa waTZ,waKenya,Rwanda na Burundi, na sababu kubwa ni kwamba kabla hawajaenda huko hawakua na information ya kutosha kuhusu chuo hicho. Sina hakika kama kimeshapata accreditation kwa sasa ila mpaka mwaka juzi nilipoenda Kampala ilikua inasemekana chuo hakikua na accreditation hicho mkuu(samahani mliograduate pale kama nawaangusha) ila ni information niliyoipata kule Kampala,mwaka 2008.
 
Back
Top Bottom