Onyo kwa timu ya Simba dhidi ya mechi ya Vita club

MTAZAMO

JF-Expert Member
Joined
Feb 8, 2011
Posts
19,675
Reaction score
33,583
Wakuu,

Kwa ufupi sana kuna kila dalili Vita wanaweza kutushangaza kuliko walivyowashangaza Al Ahly kule Cairo. Wamejiandaa kwa hii mechi kuliko walivyowahi kujipanga kwa muda mrefu kwa mujibu wa media za Kinshasa.

Simba wasahau rekodi zao za kwa Mkapa hatoki mtu, Simba wajiandae na game ngumu ambayo hawajawahi kukutana nayo pale kwa mkapa kwa muongo mmoja uliopita.

Simba watashinda hii game kama spirit za wachezaji zipo juu sana. Mbinu si tatizo bali ari ya wachezaji. Kocha wa Simba ni fundi wa hizi game lakini kesho will have the real test.

Mungu ibariki Simba, Mungu ibariki Tanzania [emoji120]
 
Usiogope, ki professional sawa Simba wawe makini na hao jamaa, ila wasizidishe pressure matokeo yake ikawa balaa pia.

Hao Vita msimu huu nawaona sio wakali kama misimu iliyotangulia, walipigwa na Simba kwao goli moja, wameenda Egypt wakaambulia sare ya 2-2 ambayo kwa mtazamo wangu naona ilitokana zaidi na uzembe wa Al Ahly, kuprove hili lilikuwa right wamepigwa kwao 3-0.

Zaidi naona taarifa hao Vita watawakosa wachezaji wao tegemeo wawili, akiwemo Djuma (beki wa pembeni) alieumia akiwa na timu ya taifa ya Congo, inasemekana anaweza kukaa nje ya uwanja miezi sita. Japo Vita walipigwa kwao hao wachezaji wote wakiwepo uwanjani.

So Simba wajiandae na game wakacheze kwa ari inayotakiwa wataibuka na ushindi.
 
Umetoa usahihi wa mambo yalivyo,wachezaji wangu wa Simba wakijipodoa tu wanapoteza mechi hii.
 
Na kesho MUNGU WAO atakuwa hajafufuka bado maana kashagongwa huku..
 
Kesho Simba watagundua kwamba kumbe pilau lao chini lina mchanga kama sio kokoto
 
Kosa la kiufundi linaloweza kuicost Simba ni kuzembea kumchapa Merreikh kwao wakati walikuwa wana uwezo wa kumfunga Merreikh sasa ona inamlazimu hii mechi akaze misuli kama John Cena ili atoboe maana nina uhakika tukipigwa hapa Vita atavuka kundi hili akiwa wa pili maana uwezo wa kumfunga Aly Ahly kwao ni mdogo sana
 
Nililonga hili sikuvya sare na el merreikh watu wakabisha wee mpaka mishipa ya makalio ikawatoka
 
Utopolo wanatupa karata yao ya mwisho leo!! Semeni Sana muda huu maana baada ya mechi kila utopolo atalazimika kutekeleza uzi wake!! Waulize utopolo wenzio kina Renzo, All-Rounder ambavyo huwa wanatoka nyuzi zao!!
Niwaombe tu leo jikazeni kubaki kwenye uzi hata kama simba itashinda! Utopolo mnatia huruma!!
 
Ndiyo kama ulivyoona mwenyewe kilichotokea kwa Nkapa
 

Mkuu umenichekesha sana hapo mwisho,sina uhakika kama watabaki hapa tena[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…