Ooh Naingia kama Obamaaa!

Kadingi

Member
Joined
Jun 30, 2013
Posts
14
Reaction score
3
Ndio naingia jamani,nipokeeni kwa hesima na taadhima!Niaje ma Greater Thinker!Mpo!Au mpo mpo kama kina naliu,nani wale wa pale mtaa wa Rais wa kwanza aliye uliwa kule Zaire nani yule...aah!Lete hoja tachagia hoja ukileta vioja tajua umeonja au wale makanjanja!Mnamfulrahia Oboma mmejipanga na majanga ya kuwakaribisha wamarekani au mnathani mtajitoa kwenye umasikini!Fanyeni kazi kwa bidii rasirimali zipo lakini nyie mpo mpo tu!Mmerogwa na nani nyie!Mchina kasaini mikataba kibao hata mmoja haujawekwa wazi na leo hii kama kawaida yetu tumeshasahau,tupo busy na Obama naye atasaini kama kawaida mipicha itapigwa kilichosainiwa ni sirikali baada ya hapo,litatafutwa tukio lingine ili tusahau kama tulivyosahau mambo muhimu Richmond,Meremeta,Jairo,Uliboka,Magamba yaligoma kuvuka,Mwagosi,Kibanda,Mauaji ya Padri,Mabomu ya Arusha,Kauli ya Pinda,Rasimu ya Katiba Mpya,Mahela ya Uswisi,Gesi ya Mtwara yaani yapo mambo mengi tu jamani!Hivi tuna nini sisi watanzania tumekuwa watu wakoongozwa kwa kuletewa matukio ili kututoa kwenye hoja muhimu!Leo gharama za kuja Obama zinaenda kuongeza deni la nchi pamoja na kuchukuliwa rasirimali zetu sisi tupo tu tunakenua meno Obama Obama!Yaani hata nyie ambao mnauelewa na nyie MAGT mpo mpo tu!Mmekaa kishabiki shabiki!Aaaaaaaaaaaaaaaaaah!
 
Dogo karibu, wenzio tunafurahia Obama amecheza ngoma pale airport... punguza hasira.
 
Dogo karibu, wenzio tunafurahia Obama amecheza ngoma pale airport... punguza hasira.

Umejuaje kama mi dogo,wakati hapo juu panajieleza kabisaa!Nina hasira kwa sabubu ya ujinga wetu,kaja Clinton ,Bush na leo Obama hebu nipe tathimini ya hizo ziara mbili mpaka sasa!Au vyandarua!Aaah jamani hata hii inahitaji kuwa na Digrii mbili za uchumi!
 
Karibu mgeni mwenyeji apone. Huyu mgeni mbona matata sana. Mgeni mwenyeji nini huyu, simwelewi elewi.
Mgeni kaamua kuja upya upya kwa new email, wrong phone number.
Mgeni mkwara kibao, wewe mgeni mbona wa ajabu wewe. Mgeni mkwara mwingi kuliko wenyeji.
Haya jichinjie kuku mwenyewe. Karibu ya uwongo uwongo ila mgeni hayo mawe yako, mule mule.
 
Mikwara!Wakina Obama wanasema read between the lines!Kuna uwongo wowote katika mambo niliyoongea kamanda wangu au unanitry!Wakati mwingine maelezo ya mtu yaweza kukujulisha tabia yake,so mimi si mtu wa mikwara kama watz wengi tulivyo maneno mengi kuliko matendo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…