Ooh rabi, nilidhani karanga, kumbe mavi ya mbuzi

Ooh rabi, nilidhani karanga, kumbe mavi ya mbuzi

Dotto C. Rangimoto

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2012
Posts
1,985
Reaction score
1,286
OOH RABI, NILIDHANI KARANGA, KUMBE MAVI YA MBUZI.

1. Nilidhani ni karanga, kumbe ni mavi ya mbuzi,
Sikudhani ni pakanga, katika wangu mchuzi,
Kuamini mtu janga, jiandae na mauzi.
Kuna mambo ya kuchunga, sifanye tu maamuzi.
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.

2. Nilidhani ni maziwa, kumbe ni tui la nazi,
Ati nimependelewa, na mola wangu Azizi,
Kumbe janga nimepewa, wallahi si kumaizi,
Yale niliyotendewa, mlipaji ni mwenyezi.
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.

3. Nilidhani ni malaika, kumbe adui shetani,
Mimi nilimchunuka, tena nilimuamini,
Kumbe vile anicheka, aniingize mjini,
Akapanga kuchomoka, na sanduku la thamani.
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.

4. Nilidhani muumini, alo na sifa stahiki,
Kumbe najenga imani, kwa kiumbe mnafiki,
Akafanya ushetani, kanirushia mkuki,
Namshukuru Manani, yuko uchi mnafiki,
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.

5. Nilidhani ni kitanda, kumbe tusi la maiti,
Kule kote kunikanda, ni mbinu zake afriti,
Ili apate niponda, aibe zangu tikiti,
Mja alivyonitenda, nusura niwe maiti.
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.

6. Aheri shetani jini, kuliko shetani mtu,
Nani amtuma jini, si kama kiumbe mtu?
Hata ndugu wa ndani, kumwamini sithubutu,
Aweza kuwa shetani, anipige na mtutu.
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.

7. Unapoweka imani, uweke na tahadhari,
Silaha za kibindoni, na dua kwa Qahari
Ujue wafanya nini, inapotokea shari,
Kilio chafaa nini, mtenda hana habari,
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.

8. Yupo fanani bubusa? katika sanaa zake?
Yaani aso yagusa, mambo ya jamii yake?
Au ashindwe papasa, tako la moyo wake?
Kama yupo ni tutusa, ina shida rasi yake,
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.

9. Niliuchonga ujiti, nichore yalo nisibu,
Nikafuata shuruti, pamoja na taratibu,
Wino wa chani kiwiti, ukakinakshi kitabu,
Mwisho ikawa kunuti, nipate chuma thawabu
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.

10. Sijui niweke koma, ama niweke mkato,
Watendwa si hukoma, ama hukwepa kong'oto,
Sitarudia pogoma, kama ng'ombe aso kwato,
Kuwa boya nimekoma, sikiza msaka sato.
Usimwamini yeyote, amini kivuli chako.

Shairi hili lipo hapa kwa hisani ya watu wa Machame.

Njano5.
0784845394
 
Asante Mkuu kwa kuturudisha katika fani ambayo nayo pia inaanza kupotea. Ujumbe Maridhawa kwa wenyekutafakari. Kwa lugha ili ya Kiingereza tunasema,

The only person you can trust is yourself.

I don't trust the society to protect me and my family. I also refuse to live by the rules set by others which condemn me and my family to utter poverty.

Dah! Mkuu kuna mengi ila naelekea TEGETA kwanza nashuka pale IPTL.
 
Asante Mkuu kwa kuturudisha katika fani ambayo nayo pia inaanza kupotea. Ujumbe Maridhawa kwa wenyekutafakari. Kwa lugha ili ya Kiingereza tunasema,

The only person you can trust is yourself.

I don't trust the society to protect me and my family. I also refuse to live by the rules set by others which condemn me and my family to utter poverty.

Dah! Mkuu kuna mengi ila naelekea TEGETA kwanza nashuka pale IPTL.

ASANTE mkuuu,,, nashukuru kwa kujali,,, na kuipenda fani yetu ya ushairi wa kiswahili,,,,

usisaahu LUMBESA,,,,kama kweli waenda IPTL
 
Back
Top Bottom