Operesheni maalum ya Putin

Operesheni maalum ya Putin

Mavindozii

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2012
Posts
2,111
Reaction score
2,781
Operesheni maalum" ya Putin haijaenda kulingana na mpango. Kile kilichopaswa kuchukua siku au wiki kadhaa tayari imechukua miezi kadhaa.

Kremlin inaonekana kabisa haikuchukulia upinzani wa Ukraine kwa uzito mkubwa.

Magharibi kuunga mkono Kyiv na wimbi la vikwazo vya kimataifa ambavyo Urusi ingekabiliana nayo. Kaputin ameingia choo cha kike, Achana na Nchi za Magharibi wanachheza na akili za Kaputini. Wana akili sana hao wajamaa.
 
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]

Sawa maria zakharova au peskov !!?
 
Asidharauliwe bado ana nguvu na akianguka Putin kishindo chake kitakuwa kikubwa
Najua ulishawahi kutega ndege na ulimbo ? Kama ulishawahi ni vile umekaa pembeni alafu kuna kile kindege kina mkia mrefu kinakuja kurukaruka juu ya tawi la mti lenye ulimbo alafu kenyewe hakatui, ila kubwa jinga njiwa anakuja analikalia paap tayari hizo mbio za kwenda kumchukua ni kama ndugu yangu Alphonce Simbu yupo Ollimpic 🇯🇵.

Ukweli ni kwamba mpaka sasa Russia anaona kabisaa maji alioyaendea hayanyweki, na tayari yupo kwenye tawi la ulimbo na anaogopa kuruka maana kosa la kuruka ni kutaka na mbawa zinaswe hapo ndipo mtegaji atakuja speed ya gari yako pendwa BMW 5MI ikishika lami ya Mkiwa ikiitafuta Isuna kuelekea Singida mjini.

Russia now inabidi tu ili amchanganye mtegaji ni atulie kwanza hivyo hivyo kavita kidogo huku akiwa makini kujua namna ya kunyanyua mguu kwenye tawi lenye ulimbo ila akikurupuka tu tayari na mbawa zitadakwa na hapo ndio atajua kwanini wimbo wa Taifa letu haujarekodiwa video wakati serikali ina uwezo wa kurusha helicopter kutuonyesha matokeo ya Sensa.
 
True bro alaf hizi taarifa kuwa Putin ajafikia malengo yake kazitoa nani kasema mwenyewe Putin

au wasemaji wake binafsi wa kujitolea
Unaweza kuta anaesema hivyo mpaka Sasa anakula kwa mama yake bira kutoa msaada wowote hapo home, hajayajua malengo ya huyo anaemzungumzia lakin anasema malengo yake hayajatimia ukiimuuliza yapi hayo malengo yake anayoyajua yeye hayataji.
 
Operesheni maalum" ya Putin haijaenda kulingana na mpango. Kile kilichopaswa kuchukua siku au wiki kadhaa tayari imechukua miezi kadhaa. Kremlin inaonekana kabisa haikuchukulia upinzani wa Ukraine kwa uzito mkubwa. Magharibi kuunga mkono Kyiv na wimbi la vikwazo vya kimataifa ambavyo Urusi ingekabiliana nayo. Kaputin ameingia choo cha kike , Achana na Nchi za Magharibi wanachheza na akili za Kaputini . Wana akili sana hao wajamaa .
Unapoweka uzi wenye kualika thinkers jitahidi kuweka hata some sources za taarifa ama findings zako.

Ukiwa unategemea vyanzo vya kutokana na mijadala mitabdaoni utaona kila upande unashinda vita.

Kikubwa let us emphasize on truce
 
Najua ulishawahi kutega ndege na ulimbo ? Kama ulishawahi ni vile umekaa pembeni alafu kuna kile kindege kina mkia mrefu kinakuja kurukaruka juu ya tawi la mti lenye ulimbo alafu kenyewe hakatui, ila kubwa jinga njiwa anakuja analikalia paap tayari hizo mbio za kwenda kumchukua ni kama ndugu yangu Alphonce Simbu yupo Ollimpic [emoji627].

Ukweli ni kwamba mpaka sasa Russia anaona kabisaa maji alioyaendea hayanyweki, na tayari yupo kwenye tawi la ulimbo na anaogopa kuruka maana kosa la kuruka ni kutaka na mbawa zinaswe hapo ndipo mtegaji atakuja speed ya gari yako pendwa BMW 5MI ikishika lami ya Mkiwa ikiitafuta Isuna kuelekea Singida mjini.
Russia now inabidi tu ili amchanganye mtegaji ni atulie kwanza hivyo hivyo kavita kidogo huku akiwa makini kujua namna ya kunyanyua mguu kwenye tawi lenye ulimbo ila akikurupuka tu tayari na mbawa zitadakwa na hapo ndio atajua kwanini wimbo wa Taifa letu haujarekodiwa video wakati serikali ina uwezo wa kurusha helicopter kutuonyesha matokeo ya Sensa.
Wajanja wanamcheck kwenye bainokola[emoji16][emoji16]

Sent from my Infinix X660B using JamiiForums mobile app
 
Screenshot_20221101-171155_Twitter.jpg
 
Asidharauliwe bado ana nguvu na akianguka Putin kishindo chake kitakuwa kikubwa.
Kishindo chake kitakuwa kikubwa ndani ya Urusi kwa sababu ya kukosekana kwa checks and balances katika utawala wa nchi. Taasisi za kiutawala na mihimili yote ya kiserikali iko chini ya udhibiti wa rais ama the Kremlin katika kufanya maamuzi.

Hivyo, suala lolote litakaloleta madhara kwa the Kremlin katika uendeshaji wa nchi na utekelezaji wa maamuzi ya kiutawala, litasababisha madhara kusambaa katika sehemu zote za kiutawala zilizopo chini ya udhibiti wa kimaamuzi wa rais ama the Kremlin.
 
Back
Top Bottom