Wasaalam,
Poleni na mihangaiko ya kutafuta unafuu wa maisha wakuu, na kwa wenzangu na mimi tunaofanya kazi kutokea majumbani katika kipindi hiki cha Mlipuko wa corona ni fursa pia ya kufanya mambo mengine binafsi.
Well kama kichwa cha uzi kinavyojitanabaisha, Kila mahali ambapo kuna kuwa na kundi la watu huwa kuna tabia ya kuzuka maneno fulani ambayo watu wa kundi husika tu ndio huweza kujua maana zake, maneno haya kwenye lugha ya kiswahili huitwa "MISIMU" hapa wataalamu wa kiswahili watanielewa zaidi.
Misimu ina sifa ya kukua na kutoweka baada ya muda fulani. Basi nimeona ni vyema nasi wana JF tukaijua msimu yetu ambayo ina trend ama kutumiwa sanaa na wadau kwenye ulimwengu wetu huu wa JF.
Mimi nitaanza na haya maneno ambayo huwa yananifurahisha sanaa nikiyasikia humu JF 😅😅😅.
1. POPOMA
2. PAPUCHI
3. KULA TUNDA KIMASIHARA
4. KUGEGEDA
5. JIWE
6. KUMWAGA POVU ,hili limekuwa likitumika kwenye mazingira mengine nje ya JF pia.
Well kama kuna neno unaliona linatrend au kutumika sanaa humu Jf ama linakufurahisha ukiliona ruksa kutiririka.
Karibuni,
N:B VITA YA CORONA NI YETU SOTE