Orodha ya wachezaji mizigo Yanga

Kwan zalan fc wanatokea mkoa gani hapa bongo? mbn wamepigwa halafu unasema kocha hajawahi kushinda kimataifa. Timu zinazidiana uwezo, lakini pia mpira una matokeo matatu lolote linatokea , timu zote zinatafuta matokeo
Zalan hamna kitu. Wale jamaa hata pesa ya Hotel hawakuwa nayo. Yaani tuliwaleta sisi toka kwao. Unategemea nini?
 
Matola anasubiri tu timu ifungwe hiyo tarehe 23, ili muanze tena kumrushia makopo.
Simba wameshahama huko. Kwa wao sasa kufungwa na Yanga si issue. Nakaaa na wasimba wameshajitoa kwenye usimba na yanga. Wao wanaangalia kimataifa zaidi. Hapa katikati tumewafunga sana huoni hata wakigombana. Wao wanalia na matches za Kimataifa na za ligi kwa ujumla si yanga pekee.... Tutajikuta mwishoni ni sisi tu tunashangilia sana kuwafunga Simba wao wanaona kawaida tu na wanaendelea kujipanga. Utaniambia. Tunabweteka sana kwa kuwafunga Simba.
 
😂 Na bado, Morrison simlimchukua ili kuikomoa Simba heti!!
 
Lawama zote pelekeni kwa uongozi. Wewe unajiandaa na mechi za kimataifa bila kucheza mechi za kirafiki zenye uzito wa kimataifa?

Wachezaji hawana hatia wako vizuri sana shida uongozi wenu uliendelea kupiga kampain hata baada ya uchaguzi.
Na wachambuzi maandazi wa mpira pia wanaiharibu yanga, ndio walikuwa wanaikosoa Simba kwenda nje ya Nchi pre-seson
 
Sijui Yanga akifungwa na SIMBA itakuwaje
Your browser is not able to display this video.
 
Sababu ya yanga kutolewa ni hii:
Kocha wa Alhilal anaijua yanga vizuri zaidi kuliko Nabi anavyoijua Alhilal.

Kocha wa alhilal aliiandaa vyema timu yake kimbinu, dhidi ya ubora na mapungufu ya yanga.

Hata kama utafuta hizo mechi mbili waanze upya bado alhilal atashinda.
 
Morrison Simba walishamwacha. Walishaona hana nidhamu. Ndo maana unaona mwishoni walimtema kiaina. Simba walimwacha jamaa baada ya kuona ana homa ya vipindi. Sisi ambao alishatuaibisha tukamwona ni mali.
Ipo wazi kabxaa...hata jana uliona alivyokuwa hana nidhamu uwanjan hadi wenzake wanammind na kutaka atumie akili na c kufanya utoto uwanjan
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…