OSHA yazuia ubomoaji wa Jengo la Zamani la DDC Kariakoo kwa kutofuata utaratibu

OSHA yazuia ubomoaji wa Jengo la Zamani la DDC Kariakoo kwa kutofuata utaratibu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
IMG-20240604-WA0007.jpg
Saa chache tangu Mwanachama wa JamiiForums.com alipolalamikia juu ya mchakato wa ubomoaji wa jengo la zamani la DDC Kariakoo, akidai unafanyika kiholela bila kuzingantia hatua za kiusalama, hatua zimechukuliwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA).

Kuhusu hoja ya memba, soma hapa ~ OSHA mko wapi? Ubomoaji wa jengo la zamani la DDC Kariakoo unafanyika kiholela, ni hatari kwa usalama wa Watu

Meneja-Kanda ya Pwani wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA), George H. Chali amesema:

Tumeona andiko na hayo malalamiko ya Mwananchi jana usiku (Juni 5, 2024) na tukabaini wabomoaji wamekiuka SHERIA YA AFYA NA USALAMA MAHALI PA KAZI NAMBA 5 ya Mwaka 2003 na Kanuni za zake, hawakufuata utaratibu unaotakiwa.

Kwanza kabla ya kufanya ubomoaji kama huo waliokuwa wakiufanya wanatakiwa kufanya tathimini ya nini kitatokea wakati wa mchakato.

Wanatakiwa kusajili mchakato wao huo OSHA lakini wahusika hawakufanya hivyo.

Hivyo, tumezuia mchakato wote wa ubomoaji hadi wahusika watakapofuata taratibu zinazotakiwa labda kama waendelee kufanya hivyo kinyemela.
 
Saa chache tangu Mwanachama wa JamiiForums.com alipolalamikia juu ya mchakato wa ubomoaji wa jengo la zamani la DDC Kariakoo, akidai unafanyika kiholela bila kuzingantia hatua za kiusalama, hatua zimechukuliwa na Wakala wa Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA).

Kuhusu hoja ya memba, soma hapa ~ OSHA mko wapi? Ubomoaji wa jengo la zamani la DDC Kariakoo unafanyika kiholela, ni hatari kwa usalama wa Watu

Meneja-Kanda ya Pwani wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA), George H. Chali amesema:

Tumeona andiko na hayo malalamiko ya Mwananchi jana usiku (Juni 5, 2024) na tukabaini wabomoaji wamekiuka Sheria ya Mwaka 2003 ya Ulinzi na Usalama Sehemu za Kazi, hawakufuata utaratibu unaotakiwa.

Kwanza kabl ya kufanya ubomoaji kama huo waliokuwa wakiufanya wantakiwa kufanya tathimini ya nini kitatokea wakati wa machakato.

Wanatakiwa kusajili mchakato wao huo OSHA lakini wahusika hawakufanya hivyo.

Hivyo, tumezuia mchakato wote wa ubomoaji hadi wahusika watakapofuata taratibu zinazotakiwa labda kama waendelee kufanya hivyo kinyemela.
Osha wanataka kutuambia kuwa ubomoaji hauhitaji kibali na maelezo ya usalama toka kwao! Sisi huku uswazi ukibomoa choo cha paspoti saizi itashangaa dakika mbili wamefika na faini shs. 50,000/=.
 
Back
Top Bottom