Oysterbay Police-Rushwa imetamalaki

Oysterbay Police-Rushwa imetamalaki

apolycaripto

JF-Expert Member
Joined
Feb 11, 2011
Posts
644
Reaction score
225
Ndugu wanajamvi kweli ule usemi wa ukitaka kujua shida ziko wapi nenda hospitalini(za serikali), mahakama na polisi.Hali iliyopo Oysterbay polisi ni zaidi ya huko kote.

Binafsi nilipata fursa ya kufika hapo baada ya kupata ajali (nikiwa gari yangu imegongwa na mgongaji uwezo mdogo hivyo kuhitaji Bima yake itibu gari yangu).Cha kushangaza nilianza kuombwa rushwa kuanzia Traffic eneo la tukio,vehicle inspector,mfungua file,mpiga chapa na mpelelezi (wote traffic hawa).

Mazee mkono umekuwa mfupi mpaka sasa kesi yangu haieleweki japo hajafa wala kujeruhiwa mtu kwenye ajali hiyo.Kila nikienda file halionekani, nikamtafuta mgongaji wangu (Dreva ambaye hayuko vizuri kimapato) akadai hata yeye anashangaa kwa nini hawajamfikisha mahakamani wakati kila kitu kimezingatiwa.Alidai jamaa walimwambia akitaka mambo yaende haraka ''akunjuke''.

Kuna kichwa kinaitwa Ambwene, du! Yaani utadhani nchi haina mtu, yaani anakwambia kabisa uandae cha kwake kabla hajafanya inspection.Binafsi nimepata mshituko, huyu mtu amedumuje hapo na kujiachia kihivyo.

Kwa ujumla afya zao ni nzuri, vijiti mdomoni na wala hawana wasiwasi.WanaJF ebu nipeni ushauri jinsi ya kutatua hiyo issue yangu.

Tupo pamoja.
 
Rais dhaifu nchi imekuwa tahabani. Dawa ni Lowassa madarakani au CCM kuipisha Chadema. Huyu Baba Mwana Asha hana maana yoyote zaidi ya kucheka cheka na kuwapa marafiki vyeo..... wengine wakina Rais wa Akudo Pedeshee January Makamba badala ya kufanya kazi, wanaenda kupiga picha kwenye ma Bajaj na suruali utazani kijana anayebalehe
 
hakuna sehemu iliyojipanga vzr ktk utumishi wa umma ktk kumhudumia raia, kama hao mapolisi japo katika msafar wa mamba na kenge wapo, cha msingi kile unachokizungumzia si majungu, ktk ofisi za mapolisi kuna ofisi za wakubwa wao gonga lalamika, hukusikilizwa songa mbele hadi kwa mwema wataingi a baridi na suala lako litatatuliwa mara moja. usikate tamaa , rudi na muone mkubwa wao atakusikiliza cha msingi isiwe majungu.
 
Rais dhaifu nchi imekuwa tahabani. Dawa ni Lowassa madarakani au CCM kuipisha Chadema. Huyu Baba Mwana Asha hana maana yoyote zaidi ya kucheka cheka na kuwapa marafiki vyeo..... wengine wakina Rais wa Akudo Pedeshee January Makamba badala ya kufanya kazi, wanaenda kupiga picha kwenye ma Bajaj na suruali utazani kijana anayebalehe

Hapo mkuu ndo umeniacha hoi kabisa
 
Njia ni kuweka utawala mpya hata kama hauna sifa za uongozi. Hao wenye sifa wamefanya nini? Mwambie mwenzio tujiandae kuitoa CCM 2015.
 
Njia ni kuweka utawala mpya hata kama hauna sifa za uongozi. Hao wenye sifa wamefanya nini? Mwambie mwenzio tujiandae kuitoa CCM 2015.

Hii naona ipo sehemu nyingi kweli. Rushwa ya shilingi elfu nane ilipoteza haki ya dungu yangu ya kuibiwa kitu cha thamani ya laki tano kituo kidogo cha polisi Kahama. Takukuru wakitaka kufanya kazi kwa urahisi, basi waanzie hapa. Sasa nao ni kuwapelekea za moto (Za TAKUKURU) tu kwani naona hata aibu hawana siku hizi utafikiri hali ngumu ni kwao tu.
 
mkuu hao jamaa ni noma.ebu fikiria mpaka ss hawajapata mshahara wa mwezi wa kumi kwa nini wadikuombe rushwa pale unapohitaji msaada wao wakati nawao hawatendewi haki???

Kikubwa kama una mawasiliano na Said wa Mwema mtwangie huwa anapokea simu na mueleze mara moja tatizo litaisha na jama wale wa osterbay watapanguliwa tu.

IGP kachoswa na hzo kashfa za watu wake kuwa chanzo cha migogoro kwenye Jamii.
 
Rais dhaifu nchi imekuwa tahabani. Dawa ni Lowassa madarakani au CCM kuipisha Chadema. Huyu Baba Mwana Asha hana maana yoyote zaidi ya kucheka cheka na kuwapa marafiki vyeo..... wengine wakina Rais wa Akudo Pedeshee January Makamba badala ya kufanya kazi, wanaenda kupiga picha kwenye ma Bajaj na suruali utazani kijana anayebalehe

hapo..!.jpg

Mmmh kweli mukubwa si unajionea mwenyewe..............!
 
Ndio maana wameuza kabisa na eneo ili mjue wako kibiashara zaidi...
 
Rais dhaifu nchi imekuwa tahabani. Dawa ni Lowassa madarakani au CCM kuipisha Chadema. Huyu Baba Mwana Asha hana maana yoyote zaidi ya kucheka cheka na kuwapa marafiki vyeo..... wengine wakina Rais wa Akudo Pedeshee January Makamba badala ya kufanya kazi, wanaenda kupiga picha kwenye ma Bajaj na suruali utazani kijana anayebalehe

kweli mzigo mzito apewe punda!
 
Issue hapa ni uwajibikaji. No proper service ondoa CCM weka CDM. Nao wakileta za kuleta weka jeshi maana waTZ tumekuwa sugu kila mtu anavuta kwa kadri ya mahali alipo. Mahakama, elimu, hospitali, TRA, manispaa, ardhi sijui ni idara ipi utaenda upate huduma bila kuzunguka mbuyu. Nitajieni. Hata mortuary bila kidogo huduma huwa ya kulegalega. Mkuu wa nchi anapaa tu anasema uchumi nao unapaa khaa aibu.
 
hongera sana ambwene ongeza bidii ya kula rushwa ili ufikie kama yule cptn komba aliye nikagulia gari yangu@Si nasikia serikali imesema mjilipe mishahara au bro uliye anzisha uzi ujui hilo? Jamaa wanajilipa mshahara kwa kiwango anachoona yeye mwenyewe kuwa kinatosha, na nadhani tutashuhudia mengi ya hayo labda oo vocha imeisha kwa heri.
 
Mi ndio maana nikitembelea vituo vya polisi huwa naimba kwa sauti ya juu ule wimbo wa zamani,

Jamani acheni kulaumu sekta moja tu! mifumo yote imeoza! hata huyo alopata ajali muulizeni hilo gari kanunua kwa hela gani? wizi mtupu! huduma zote sekta zote ni hovyooooo!
 
Tatizo ni kwamba sisi wenyewe ndo tumewazoesha huo upuuzi.......akiomba anapewa, so imekuwa norm of the day.
 
Hawa Polisi walishaapa kushindana na TRA kwenye rushwa.Sasa sijui refa wao ni nani.Tusubiri jeshi la Mangula na Kinana wana nini jipya.
 
Ndugu wanajamvi kweli ule usemi wa ukitaka kujua shida ziko wapi nenda hospitalini(za serikali), mahakama na polisi.Hali iliyopo Oysterbay polisi ni zaidi ya huko kote.

Binafsi nilipata fursa ya kufika hapo baada ya kupata ajali (nikiwa gari yangu imegongwa na mgongaji uwezo mdogo hivyo kuhitaji Bima yake itibu gari yangu).Cha kushangaza nilianza kuombwa rushwa kuanzia Traffic eneo la tukio,vehicle inspector,mfungua file,mpiga chapa na mpelelezi (wote traffic hawa).

Mazee mkono umekuwa mfupi mpaka sasa kesi yangu haieleweki japo hajafa wala kujeruhiwa mtu kwenye ajali hiyo.Kila nikienda file halionekani, nikamtafuta mgongaji wangu (Dreva ambaye hayuko vizuri kimapato) akadai hata yeye anashangaa kwa nini hawajamfikisha mahakamani wakati kila kitu kimezingatiwa.Alidai jamaa walimwambia akitaka mambo yaende haraka ''akunjuke''.

Kuna kichwa kinaitwa Ambwene, du! Yaani utadhani nchi haina mtu, yaani anakwambia kabisa uandae cha kwake kabla hajafanya inspection.Binafsi nimepata mshituko, huyu mtu amedumuje hapo na kujiachia kihivyo.

Kwa ujumla afya zao ni nzuri, vijiti mdomoni na wala hawana wasiwasi.WanaJF ebu nipeni ushauri jinsi ya kutatua hiyo issue yangu.

Tupo pamoja.

Sasa, wewe unataka wafanyeje kama bado hawajalipwa mshahara wa mwezi uliopita?
 
Back
Top Bottom