Pablo Franco Kocha Mpya wa Simba SC

demigod

JF-Expert Member
Joined
Jan 2, 2015
Posts
8,292
Reaction score
15,250
Simba imemtangaza Pablo Franco (41) kuwa Kocha Mkuu mpya akichukua nafasi iliyoachwa na Didier Gomes Da Rosa

Kocha huyo alikuwa anainoa Al Quadsia ya Kuwait. Pia amewahi kuzinoa Fuenlabrada, Getafe na amewahi kuwa Kocha Msaidizi Real Madrid.

Swali Je Ana uzoefu upi wa Soka la Kiafrika?

CV yake inaonyesha hajawahi kufundisha barani Afrika. Changamoto za soka la kiafrika anazitambua.

Hapa naona Simba wamejipiga na kitu kizito kingine.

 
Hamna kitu hapa... Polei wana Simba wenzangu.
 
Walisema wanamtaka asie na jina wala CV kubwa aje kuvipatia vyote Simba SC, hii kamari ngoja tuone kama italipa.

Hivi unaweza kuwa na malengo ya kufika mbali kwenye mashindano ya nje na ndani halafu ukamchukua kocha asie na experience ya mashindano husika?

Wanasema wanamtaka asie na jina ili awe na kiu ya mafanikio, kwani mwenye jina ndio anaweza kukubali kuharibu CV yake kizembe kwa kutofikia malengo ya kazi yake?

Hapa naona bora wangetupa sababu nyingine ya kumchukua huyo kocha asiyefahamika, kama ni issue ya mshahara tujue, lakini tusidanganyane na sababu zao walizotoa kwa kumchukua huyo kocha, Simba SC kwa level waliyofiki sio timu ya kuwajaribu makocha, sioni maana ya kumuacha Gomes halafu unaenda kumchukua mwenye CV ndogo zaidi.

#madness.
 
Huo uzoefu unataka awe ameupata wapi?
 
Kuionao Sevilla ama Qadsiya sio sawa na kunoa timu za Africa....... ningewaona wa maana kama mngechukua kocha mwenye profile kubwa kwa Africa hasa kwenye mashindano ya CAFCL&CAFCC
 
Kuionao Sevilla ama Qadsiya sio sawa na kunoa timu za Africa....... ningewaona wa maana kama mngechukua kocha mwenye profile kubwa kwa Africa hasa kwenye mashindano ya CAFCL&CAFCC
Acha kukariri Matola yupo na wazee wa ndumba wapo, soka la Afrika wanacheza wachezaji 30 au mipira inakuwa miwili uwanjani
 
Saivi biriani la Madrid limekuja Msimbazi
Unanikumbusha wale Waspain wa Azam FC.

Waliletwa ili kubadili falsafa ya mpira wa Azam FC.

Mwisho wa siku experience ya soka la kiafrika na tamaduni zake zikawafanya washindwe kazi.
 
Mwana utopolo naona umewahi kuleta uzi kuhusu kocha wetu anyway!! Usichokijua tu ana mfumo wake wa 2-2-6, huo mfumo alishawahi kuingiza wachezaji watatu tu uwanjani na likafa jitu, mtu kashawahi kukaa kwenye benchi la ufundi la timu kubwa kabisa duniani lakini nnavyojua majirani walivyokuwa na nongwa hata hili watalipinga, ukimchek tu sura yake ka Xavi, sasa sikwambii hizo mbinu! Mtugee tu kombe letu mapema kabla ya mwezi wa kumi na mbili!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…