Pambano la Cheka Na Mserbia

Nawapongeza sana kwa kufatilia mchezo wa masumbwi nchini na support inahitajika sana kuinua vipato vya mabondia na kuinua mchezo kwa ujumla. Mpambano wa jana Fransis Cheka ndio mshindi halali wa mchezo wa jana. Hakuna figisufigisu wala nini. Mchezo wa ngumi una vigezo kwenye kutoa maamuzi. Kwanilivyoshuhudia mtanange ule pale leaders ni wazi Cheka alistahili kushinda bila tatizo. Ukiangalia kumiliki jukwaa, Kujilinda na Kushambulia cheka ndio amefanya zaidi ya Mserbia. Ili upewe round moja kama umeishinda au la unalazimika kupigana round zote 3 kitu ambacho mpinzani wetu hakufanya hivyo. Alitumia muda mwingi kujiziba asishambuliwe (kujigadi) na kurusha makonde machache kila round. Cheka alikua busy muda wote kushambulia japo si makonde yote yaliyo mfikia usoni mserbia ila ni rahisi kumshawishi judge atoe uamuzi kwa upande wako. Nilimshangaa sana mwalimu wa yule jamaa hakumwmabia afanye mashambulizi wakati round zilikua zinayoyoma. Mserbia alikua kwenye nafasi nzuri sana ya kumuondoa cheka kwa knockout lakini hakutumia fursa hiyo kwa uwoga wake. Alionekana mwenye ngumi kali na nzito mfano round ya kwanza alipoweza kumuangusha Cheka chini.Kwa maoni yangu mserbia alishinda round 3 tu na cheka 9. Mserbia alicheza kwa uwoga mwanzo mwisho na anajua Cheka hana nguvu za kumwangusha. Tuendelee kupenda vyetu kwa ushindi wa cheka ni wa halali na hauna mashaka hata kidogo kwakua mserbia hakupigana round 3 zote alijificha dk 2 na kujionyesha dk 1 huwezi kushinda kwa style ile. Tena mimi nilidhani mserbia anamvuta Cheka hadi raound ya 7 ili aanze kushambulia amtoe kwa knockout kabisa lakini haikua hivyo.Hata angekuja judge kutoka ulaya au pambano lingepiganwa nje ya nchi bado cheka angeshinda
Cheka ndio bingwa mpya wa mabara.Hongera Cheka , Hongera Tanzania
 
Mkuu maelezo mengi lakini hoja zako za mwisho ndo zimeonyesha ukweli kua Cheka amepewa ushindi kwasababu wa kwetu walifanyiwa hivyo then Ni sahihi Cheka kupewa ushindi wa Mezani.wewe mwenyewe na Kaseba wanakiri pambano lilishakua zito kwa Cheka Ni uzoefu uliomfikisha round ya 12,
Mimi siwezi kua Mzalendo wa namna hiyo leo hii tunawafundisha nini chipukizi wa ngumi kama ukicheza nyumbani utabebwa na Majaji,tunajijenga au tunajibomoa.
Kweli hii ndo Bongo
 
Jamani tuwaache waamuzi wahukumiwe na uwongo wao kama wamempendelea Cheka lakini tujue ngumi huamuliwa kwa points,knockout au draw sasa inawezekana mzungu alikua anapiga sehemu ambazo hazikuwa na point na Cheka na kupigwa kwake alikua akimgusa au kupiga ilikua ni point.
 
Mkuu kusema kua Cheka kashinda kihalali ni kujidanganya nafsi waziwazi... sio ukweli kabisa alionekana kazidiwa, mwanzo mpaka mwisho kabisaa
 
Mkuu kusema kua Cheka kashinda kihalali ni kujidanganya nafsi waziwazi... sio ukweli kabisa alionekana kazidiwa, mwanzo mpaka mwisho kabisaa
Usihukumu ngumi kwa kutumia mawazo yako au maoni. Jua mchezo na jinsi wanavyotoa point kwa kila round. Mserbia hakupigana round zote tatu. No ring generalship, alitumia muda mwingi ku block ngumi za Cheka na si kupiga zake. Kama tungekua tuna record ngumi zilizorushwa kwa round cheka 50/20 mserbia 16/10 ambayo asingeweza kushinda. Hakushambulia kabisa zaidi ya kushitukiza kwa dk isiyozidi moja. Cheka dk 2 kafanya kazi ya kupiga mserbia dk 1 ndio apewe ushindi?Kivipi? Cheka amemu outbox yule jamaa very big margin
 
Kweli mpira ungekua unaamuliwa mezani na majaji wazawa basi hata sikumoja tungeshuhidia yanga ikiwacharaza vibaya fc barcelona
 
Hapana jamani si kwa kipigo kile,mshindi yuko nyang'anyang'a ( wa kupelekwa hospital) halafu aliyepigwa yu mzima wa afya.
 
Acha urongo Cheka kapigwa bila ubishi.. Na hakuna aliponyang'anywa point.. Cheka hata ngumi moja ya uso hajampiga yule jamaa
 
Cheka kwisha hamna kitu ana rusha ngumi utasema ana cheza kidali hazina uzito wa kuua hata mende, basi tu wanadai mcheza kwao hutuzwa kapewa mkanda hauku mstahili kabisa,kaoga ngumi sana tu kiasi cha kuingia woga,kaisha apumzike ata aibika.
 
Kumbe nyie hamjui ngumi aise.
Hizi ndio sababu why Cheka alishinda bila chenga.
1.Cheka ni CCM damu.
2.Cheka alishaingia jela tena kwa kuonewa kabisa na Bar med.
Ni hivyo tu basi.
3 Nape nnauye mzee wa bao la mkono ndio waziri wa michezo
 
Watanzania kila kitu mnajua.Haya nendeni mkakate rufaa kua cheka kapendelewa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…