Pambano la mayweather s pacman litaonyeshwa Chanel gani!!?

Varbo

JF-Expert Member
Joined
Aug 14, 2012
Posts
1,121
Reaction score
885
Wadau hili pambano sio la kuhadithiwa au kusubilia uangalie replay! Ni channel ipi itaonyesha!?
 
Niliona TBC walisema wataonyesha ila siwaamini sana! Ila kwa uhakika zaidi fungulia SS2
 
Wadau hili pambano sio la kuhadithiwa au kusubilia uangalie replay! Ni channel ipi itaonyesha!?
kwa tz bwana, ukitaka usiwe na pressure juu ya michezo yote duniani, ni kuwa na DSTV ndani. Unamaliza mchezo lakini haya mengine ni takakata tu, ila uwezo ndio unagoma tutafanyaje! labda wa mikoani kidogo kwa kupitia cables wanaweza kuliona ila uhakika ni supersports. na pambano lenyewe ni saa moja asubuhi siku ya j2 kwa saa za Afrika Mashariki,ndio wanaume wanapanda ulingoni, mapambano ya utangulizi yataanza kwenye saa kumi alfajiri. Kwani kwenye muda hapa mala nyingi huwa ni shedaaa!! mtu anaanza kusubiri tangu saa 4 usiku!! anachoka na kulala ndio game linaanza.
 
Kama ni saa moja asubuhi ya jumapili nitakuwa nimeshaamka nitasachi kila chanel kwenye kebo ila nawasiwasi na tenesko tu
 
Niliona TBC walisema wataonyesha ila siwaamini sana! Ila kwa uhakika zaidi fungulia SS2

Hivi hawa TBC ni watu wa kuamini hata siku moja kwenye events!! bado dk kumi unatangaziwa Tunajiunga na mtangazaji wetu Greisony msigwa toka songea, ambako MZEE WA KUTEMBEA NA MIKASI MIFUKONI, anazidua ghala la nafaka!! utafanya nini, kutegemea tbc, jua ni sawa na kumdhamini mmsai mahakamani/au polisi any tyme utabaki na shuka,. hapo sijaweka mala No signal, mala no service!!!
 
Ss2 kwa dstv itakua saa 10 au saa 9 alfajiri sina uhakika sana
 

Hahahahaha kweli tbc ni shidaaa
 
Tusiyo kuwa na dstv wenye nazo watusitiri
 

Teh..teh..teh..JF raha daah..!!asante kwa kuniongezea siku ya kuishi lol!!
 

Ukweli na UHAKIKA.
 
Hapo ndo tunatofautiana, wengine tbc wengine dstv!
 
Wadau hili pambano sio la kuhadithiwa au kusubilia uangalie replay! Ni channel ipi itaonyesha!?

Ondoa mashaka mkuu ukiamka j2 unachotakiwa usiangalie news yoyote nenda kwenye YouTube angalia pambano itakiwa live kwako kwa wengine recorded
 
Kweli SS2 wataonyesha Ila TBC ni ngumu sana!
 
Ukweli na UHAKIKA.

hawa ni wazee wa fitina tupu, kuna mgari wao wa matangazo ya live, walipewa na wachina, wakalizindua kwa mbwembwe, kuwa kusini wa Afrika ndio gari pekee la aina hiyo, cha ajabu wakionyesha mechi live ni aibu huo uwanja utadhania jua limepatwa!! nusu ni giza nusu mwanga!! halafu hata watangazaji wake wapo kama hawana furaha hivi!! kama vile bora liende, mi huwa napenda kuangalia tv za kenya bwana, mdada tabasamu la kutosha, nguo za kisasa, mtoto mrembo, anatangaza akiwa ame relax, sasa hawa wa tbc utadhani wanajeshi wamepindua nchi sasa ndio wanatoa briefing!!hee kumbe mmama anatangaza news bulletin!!
 

hhahaha kama umepatwa na jua
 

Hhahaha wamasai unawapenda lazima uwataje
 
Supersport ndio wamepewa haki ya kurusha matangazo ya siku hiyo kwa nchi 44 za Afrika.
 
Hhahaha wamasai unawapenda lazima uwataje
kweli nawapenda sana, ila hapo kwenye udhamini ndio shidaaa!! kwani wanavyofanana hata akiharibu kumpata ni inshu!! tena unaweza kuwa unapishana naye, na kumuuliza yelooo ile baba yoyo iko wapi siku hizi? atakwambia ipo monduli imefuata dawa!! kumbe ndio mbaya wako huyo, inakuwa kama ile KESI YA KANGA.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…