Pamoja na mziki wao kuwa tofauti je kati ya Michael Jackson na Bob Marley nani alikubalika zaidi ulimwenguni

Laiti kama Bob angeishi muda mrefu kama Michael basi wangelingana...wengi tushiakuwa watu wazima sana ila tulikuta Bob kashiafariki pamoja na hayo bado nyimbo zake tunazijua...all in all wote wakali sanaaa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi unajua Bob kafa mwaka gani? unafikiri alikua na utajiri kama wa Michael miaka tisini? Bob kafa mwaka 1981 sidhani kama kulikuwa na msanii mweusi mwenye uwezo wa kutoa misaada kama hiyo unayoitaja kipindi hicho...usifikiri wanamuziki wa jamaica wanauwezo kifedha kama wanamuziki wa marekani
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Laiti kama Bob angeishi muda mrefu kama Michael basi wangelingana...wengi tushiakuwa watu wazima sana ila tulikuta Bob kashiafariki pamoja na hayo bado nyimbo zake tunazijua...all in all wote wakali sanaaa

Sent using Jamii Forums mobile app

si kweli kabisa

Tuassume Michael Jackson alikufa 1994 ambapo alikuwa na umri sawa na ule Bob aliofariki akiwa nao...(miaka 36)

Mpaka mwaka 1994 ..Michael Jackson alikuwa ameshatoa album Kama Thriller, Bad, Off the wall, dangerous ...

Kati ya hizo album Hakuna hata moja inayofikiwa na album yeyote ile ya Bob marley kwa mauzo.

Mpaka mwaka 1994 Mj alikuwa ameshaweka rekodi ya kuchukua grammy nyingi zaidi ndani siku moja .........rekodi ambayo aliiweka mwaka 1984.

Mpaka 1994 alikuwa ameshatoa Video ya thriller ..video pekee ya muziki ambayo ipo kwenye maktaba ya taifa USA..

Mpaka 1994 Mj alikuwa ameshafanya Bad tour na Dangerous tour, tour ambazo zilijaza mamilioni ya watu kitu ambacho hakijawahi kufanywa na mwanamuziki yeyote....
 
Bob & the wailers walianzisha aina mpya ya mziki (reggae)...kabla ya hapo walikuwa wanaimba callipso (pop ya jamaica)...sasa utalinganisha reggae na mziki wa Pop uliokuwepo kitambo na kitambo...mziki wa pop obviously unauza na unajulikana kuliko reggae na pia ni wakibiashara zaidi...ndio maana kuna post yako humu humu nimekujibu usiwalinganishe watu hao wawili kifedha...Michael ana hela zaidi ya Bob...Bob hata hiyo miaka 36 hakufikisha kafa mdogo ila kafanya mambo makubwa sana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimesoma michango ya wengi humu. Nimeona wacha Nami niongeze wangu. Yaani kufananisha Hawa wawili ni sawa Na kuwafananisha Mwl Nyerere na Mandela.
Kiuhalisia Nyerere kafanya makubwa Sana Africa kuliko mandela lakini maajabu anatukuzwa mandela kuliko mwalimu.. You know why?
Misimamo ya mwalimu haikuwapendeza mabingwa wa kupamba.. Wenye uwezo WA kumfanya paka aonekane simba so wameamua mpotezea na kumwinua mandela aleyeamua wasamehe wazungu baada ya nchi kupata uhuru (bahati mbaya hatujui makubaliano waliyoingia)
So kiuhalisia mabwana wakubwa hakumpenda Bob wala jumbe za Kwenye nyimbo zake. Walijaribu mbinu zote hadi walipofanikiwa kumyamaxisha milele tatizo wameshindwa nyamazisha utamu na ubora wa nyimbo za huyu nguli..
Si kila ukipatacho google ndio yanakuwa maoni ya wengi jamani.. Ni kwwli ukiingia kwenye site mbali mbali utaona wacko jaco yupo juu Sana ila kiuhalisia Hakuna kiumbe WA ajabu kuwahi kutokea Kama Bob Marley...
Hakuna na hatakuwepo daima

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kasome history ya zimbabwe ndio utajua bob marley ni nani kablahaujaongea fanya research kaka sio kubwabwaja tuu bob alijenga majumba na kugawia maskini ndio maana watotyo wake wanaishi kwa heshima saaana(legacy) aliiacha baba yao wewe kaa na stories zisizokuwa na facts
 
Once he’d found success Marley became extremely generous with this money. Having grown up in a poor family in Jamaica he knew how difficult it was to get by. He decided to put his goodwill into practice by buying houses for friends and supported many of the poor in Jamaica.
 
Hapo umekunya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao ni WATU wawili tofauti,,,ni sawa NA KUMSHINDANISHA ANORD SWEZNIGER na ROWAN ATKINSON(MR BEEN)huyo anaigiza UBABE mwingine VICHEKESHO,,,hivi mpenzi wa MICHAEL JACKSON anayependa mizik ya SOUL...uje umwambiye mambo ya BOB MARLEY anayepiga REGGY mtaelewana kwl?MICHAEL JACKSON NI HATARI kwa music wake na hata mtunzi mzuri pia,, BOB MARLEY nae ni mzuri kwa music wake...lakini MICHAEL JACKSON alibeba DUNIA NZIMA,,,,the WACKO JACKO...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ingawa Bob alifariki mapema lakini hatatokea kama yeye ..MJ ni mfamle wa Pop ..lakini Bob Marley ni God of all kind of music..

Nyimbo za Bob zili/zimeimbwa kwa namna tofauti tofauti sana.(Version tofauti) na huo ndo ubora wa music.

Hakuna kama Bob Nesta Marley..

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…