Pamoja na Ushindi wa Yanga na Simba bado kuna shida sehemu, Magoli yamefungwa na wageni

Pamoja na Ushindi wa Yanga na Simba bado kuna shida sehemu, Magoli yamefungwa na wageni

bryan2

JF-Expert Member
Joined
Jun 8, 2016
Posts
3,323
Reaction score
4,679
Hongereni Yanga na Simba kuipeperusha bendera ya nchi vizuri, kwa sasa kila nchi ipo na shauku ya kufahamu kipi special sana kwenye soka letu. Huu moto tuliouanza tuuendeleze kwa timu zote pia mwakani, uhakika timu 4 ni vema zikajipanga zaidi ili kuendelea kupeperusha taifa letu zaidi.

Ila pamoja na ushindi kama taifa bado kuna shida, hapa ndio penye hoja ya msingi ukiangalia gemu ya jana Simba anashinda magoli 7, magoli yote yamefungwa na wachezaji wa kigeni, hakuna Mtanzania hata mmoja, ipo kazi ya kufanya.

Mchezo wa leo Yanga Vs Montasir, Yanga anashinda goli 2, goli zote zinafungwa na wachezaji wa kigeni! Bado kuna shida, Academy zetu za Soka inabidi zifanye kitu kutengeneza washambuliaji jamii ya Mayele ili nasi tuwe tishio kwenye Timu ya Taifa na vilabu vyetu.
 
Km ulitaka kumsifia mayelee ungemsifia tyuuh kivyakee, sio kuokoteza maneno mradi uridhishe nafsi yakoo. Lol

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hata ukipanga team ya taifa washambuliaji watatoka ligi za nje,,, mfano samata, Msuva, kelvin John na Joshua, kongo wenyee wakipanga kikosi Chao mayele humuoni achilia mbali kuitwa,,, Ko punguza makasiriko
 
Hongereni Yanga na Simba kuipeperusha bendera ya nchi vizuri, kwa sasa kila nchi ipo na shauku ya kufahamu kipi special sana kwenye soka letu. Huu moto tuliouanza tuuendeleze kwa timu zote pia mwakani, uhakika timu 4 ni vema zikajipanga zaidi ili kuendelea kupeperusha taifa letu zaidi.

Ila pamoja na ushindi kama taifa bado kuna shida, hapa ndio penye hoja ya msingi ukiangalia gemu ya jana Simba anashinda magoli 7, magoli yote yamefungwa na wachezaji wa kigeni, hakuna Mtanzania hata mmoja, ipo kazi ya kufanya.

Mchezo wa leo Yanga Vs Montasir, Yanga anashinda goli 2, goli zote zinafungwa na wachezaji wa kigeni! Bado kuna shida, Academy zetu za Soka inabidi zifanye kitu kutengeneza washambuliaji jamii ya Mayele ili nasi tuwe tishio kwenye Timu ya Taifa na vilabu vyetu.

Hilo sio ttzo kabisaaa na hoja yako haina mashiko
Mpira ni mchezo wa nafasi hata kwa wenzetu walioendeleea mfano Man City au Madridasta, Chelsea ama Munich na PSG…. Asilimia kubwa wanaofunga magoli sio wazama wakati mwingine ni wageni
 
Back
Top Bottom