Pamoja na Yusuf Kagoma kufanya kazi chafu pale kwenye dimba la katikati, Simba iongeze kiungo no. 6

Pamoja na Yusuf Kagoma kufanya kazi chafu pale kwenye dimba la katikati, Simba iongeze kiungo no. 6

Bando la wiki

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2023
Posts
911
Reaction score
3,017
Uchawi wa mpira now days upo kwenye nguvu ya viungo katikati ya uwanja.

Zamani uchawi wa mpira ulikuwa unaamuliwa na kasi ya mawinga ndio maana mawinga kama akina Ribbery, Arjen Robben, Wright Phillips, Theo Walcott na wengine wengi walitisha sana kwa kasi zao.

Lakini mifumo ya mpira ulipobadilika kazi ya mawinga kuwa na mbio kwa kutanua pembeni sio issue sana ndio maana unakuta winga mashoto badala ya kucheza no. 11 anachezeshwa winga no. 7 ili kwa kasi yake na guu la kushoto afosi kuingia katikati ya uwanja. Sasa mawinga wanapo fosi kuingia katikati means wanataka kuongeza namba ya viungo katikati.

Turudi kwa timu ya Simba, Simba inazidi kuimarika sana kila idara jambo ambapo ni zuri sana lwa timu inayopambania ubingwa wa nchi.
Kama tulivyosema, mpira wa kileo unaamliwa sana na viungo wa katikati (viungo wakabaji na viungo washambuliaji).

Kwenye viungo washambuliaji, Simba haina shida sana kwa sababu ina namba ya kutosha. Changamoto ipo kwa viungo wakabaji: partnership ya YUSUF KAGOMA na FABRICE NGOMA ni babkubwa. Fabrice Ngoma amepunguza sana yale makosa yake ya kuchelewesha mpira kwa kupiga chenga za kuzunguka na kurudisha mipira nyuma kwa mabeki mara kwa mara. Hapo hongera sana kwa Fabrice Ngoma.

Kiungo Yusuf Kagoma, huyo bwana mdogo ni habari nyingine kabisa. Anafika miguuni kwa adui kwa haraka sana na kuchukua mpira. Anainua kichwa kuona mpira aupige kuelekea wapi jambo ambalo huwezi kulipata kwa kiungo Mzamiru Yassin.

Hivyo ili Simba iendelee kuwa mbele ya kila mpinzani anayecheza nae, nashauri viungo wakabaji no. 6 waongezwe kwenye timu ili tuwe na uhakika wa ukabaji hasa unapokutana na mpinzani ambaye anashambulia sana.

Hivyo kwa kuzingatia hilo usajili wa wachezaji hawa mmoja wao kwa nafasi ya kiungo Mkabaji utatufaa sana. Hawa ni viungo wa shoka kweli kweli utopolo wanajua kazi yao. Kiungo wa kwanza ambaye inabidi aje msimbizi ni ADOLPH MTESINGWA BITEGEKO wa Azam FC hanaga kucheka na kima huyo.

Wa pili ni ANDY BIKOKO kutoka Tabora United huyu alizima viungo wote wa utopolo wakala chuma 3 kama wamesimama.

Toa kwa mkopo wachezaji hawa Mzamiru Yassin, Kalabaka, Okajepa, Joshua Mutale, ili uwapate wachezaji hao Andy Bikoko au Bitegeko.
 
Namba ya Fei toto wapo mafundi wengi Jean Ahou, Debora Fernandes, Awesu Awesu, Radack Chasambi. Fei atapata tabu sana
Katika hao walau kidogo anayeweza kumuumiza kichwa Fadlu wakati anapanga kikosi ni Mavambo ambaye naye anaweza kuweka sawa wakacheza wote.
 
Report yangu kwa Uongozi wa simba wafanye Marekebisho ifuatavyo.

1. Beki No 5.
2. Kiungo No 6
3. Kiungo cha Juu 10.

Asanteni kwa kunisikiliza.
 
Ofa ambayo Simba wataipeleka kwa Feitoto wai switch chap ili kumpata ADOLPH BITEGEKO
 
Hawakawii kusajili mawinga[emoji28]
1.Simba Haina Tatizo kwenye Namba
5.Simba Ina mabeki wa kati wanne na wote wazuri Sana.
(A) Hussen Kazi
(B)Che Malone
(C)Hamza
(D) Karaboue
Hapa una taka kusema Kuna shida ya beki wa kati ?

2.Eneo la Namba 6 katika Klabu ya Simba.
(A) Kagoma
(B) Okejedfa
(C) Mzamiru
(D)Ngoma
Hawa viungo wa chini Wana sifa tofauti tofauti.
Ubora wa Kagoma ni kwenye kukaba kwa nguvu na matumizi makubwa ya nguvu kwenye Eneo Hilo.
Okejedfa ni mzuri kwenye kussuport mashambulizi na kukaba kimuunganiko na wenzie.
Mzamiru ni mzuri kukaba kwenye Eneo kubwa la Uwanja.
Ngoma ni mzuri kupokonya mipira kwa kuingikia Mpira na kuchezeshwa timu akiwa chini.
Sasa kocha ana panga Namba 6 kulingana na aina ya mechi aliyo nayo.

3.Eneo la namba 10
Simba Ina wachezaji 4 ambao Wana weza kucheza Eneo Hilo la namba 10
(A) Ahoua
(B) Aweso
(C) Mpanzu
(D) Deborah
Kati ya Hawa wachezaji 4 ni mmoja pekee ndio ana sifa za kutosha kucheza Namba 10.
Ahoua ni mzuri alicheza Eneo Hilo kuliko hao wengine wote yeye ni Creator na sio Play Maker, watu wengi Wana penda wachezaji ambao ni play Maker zaidi.
Aweso ni play maker na sio Creator zaidi,ndio maana ana cheza vizuri akiwa Namba Namba kuliko Namba kumi kwa sababu atengenezi nafasi ila ana chezesha timu.
Mpanzu ni mzuri zaidi alicheza pembeni kuliko Eneo la Namba 10 kwa sababu ana penda kukimbia na mpira zaidi kuliko kucreate chance.
Deborah ni ball dance ana furaisha kumtazama lakini sio mzuri kwenye kutengeneza nafasi za mwisho ni mzuri kwenye kuchezeshwa timu Play Maker.

4.Kulingana na maelezo niliyo kuelezea hapo, Simba Ina pengo kwenye kiungo Cha ushambuliaji Eneo la Namba 10 ndio maana kocha tetesi nyingi zipo kwa Namba 10 kuliko maeneo mengine ambayo hayana mapungufu makubwa.
Lengo la kuongeza nguvu kwenye Eneo la Namba 10 kwa sababu yupo mmoja tu wengine sio Namba 10 halisi.
Kwa kuongezea Simba Ina shida na beki wa pembeni kulia mwingine wa kumsaidia Kapombe, maana Kijili hajaweza kuwa msaada kwa Kapombe.

NB: KARIBU KWA HOJA ZA KITAALAMU KUHUSU SIMBA NA MAPUNGUFU YAKE.
 
Uchawi wa mpira now days upo kwenye nguvu ya viungo katikati ya uwanja.

Zamani uchawi wa mpira ulikuwa unaamuliwa na kasi ya mawinga ndio maana mawinga kama akina Ribbery, Arjen Robben, Wright Phillips, Theo Walcott na wengine wengi walitisha sana kwa kasi zao.

Lakini mifumo ya mpira ulipobadilika kazi ya mawinga kuwa na mbio kwa kutanua pembeni sio issue sana ndio maana unakuta winga mashoto badala ya kucheza no. 11 anachezeshwa winga no. 7 ili kwa kasi yake na guu la kushoto afosi kuingia katikati ya uwanja. Sasa mawinga wanapo fosi kuingia katikati means wanataka kuongeza namba ya viungo katikati.

Turudi kwa timu ya Simba, Simba inazidi kuimarika sana kila idara jambo ambapo ni zuri sana lwa timu inayopambania ubingwa wa nchi.
Kama tulivyosema, mpira wa kileo unaamliwa sana na viungo wa katikati (viungo wakabaji na viungo washambuliaji).

Kwenye viungo washambuliaji, Simba haina shida sana kwa sababu ina namba ya kutosha. Changamoto ipo kwa viungo wakabaji: partnership ya YUSUF KAGOMA na FABRICE NGOMA ni babkubwa. Fabrice Ngoma amepunguza sana yale makosa yake ya kuchelewesha mpira kwa kupiga chenga za kuzunguka na kurudisha mipira nyuma kwa mabeki mara kwa mara. Hapo hongera sana kwa Fabrice Ngoma.

Kiungo Yusuf Kagoma, huyo bwana mdogo ni habari nyingine kabisa. Anafika miguuni kwa adui kwa haraka sana na kuchukua mpira. Anainua kichwa kuona mpira aupige kuelekea wapi jambo ambalo huwezi kulipata kwa kiungo Mzamiru Yassin.

Hivyo ili Simba iendelee kuwa mbele ya kila mpinzani anayecheza nae, nashauri viungo wakabaji no. 6 waongezwe kwenye timu ili tuwe na uhakika wa ukabaji hasa unapokutana na mpinzani ambaye anashambulia sana.

Hivyo kwa kuzingatia hilo usajili wa wachezaji hawa mmoja wao kwa nafasi ya kiungo Mkabaji utatufaa sana. Hawa ni viungo wa shoka kweli kweli utopolo wanajua kazi yao. Kiungo wa kwanza ambaye inabidi aje msimbizi ni ADOLPH MTESINGWA BITEGEKO wa Azam FC hanaga kucheka na kima huyo.

Wa pili ni ANDY BIKOKO kutoka Tabora United huyu alizima viungo wote wa utopolo wakala chuma 3 kama wamesimama.

Toa kwa mkopo wachezaji hawa Mzamiru Yassin, Kalabaka, Okajepa, Joshua Mutale, ili uwapate wachezaji hao Andy Bikoko au Bitegeko.
MAKOLO BANA
 
Back
Top Bottom