Panga la Mfaransa Simba kuwapita mastaa hawa

kbm

JF-Expert Member
Joined
Oct 5, 2012
Posts
5,224
Reaction score
1,677
-Juuko Murshid
-Laudit Mavugo
-Juma Liuzio
-Jamal Mwambeleko
-Mwinyi Kazimoto
-Mohammed Ibrahim, na
-Nicholas Gyan

Chanzo: MWANANCHI

 
Ningekuwa mimi ningeanza kumkata huyo mzungu. Yaani aina yake ya ufundishaji ni sawa na Omog tu. Muda wote anazuia. Kuanzia namba mbili mpaka namba nane anapanga mabeki na viungo wakabaji. Akicheza na Njombe Mji mfumo ni huo akicheza na Yanga mfumo ni huo. Yaani haujui hapa anapambana na ni timu kubwa au ndogo au hapa yupo ugenini au nyumbani.

Raha ya mpira jiachie sio kocha unakuwa mwoga mwoga wa kufungwa kila mechi unazuia hata muasisi wa huo mfumo Mourinho mwenyewe siku hizi kaacha kupaki basi. Watu wanaenda mpirani kuona soka la kitabuni na zaidi sana kushangilia magoli.

Timu kama simba ina kipa mzuri, mabeki wazuri, viungo wakabaji na viungo washambuliaji wazuri na mbele una Boko, Kichuya na Okwi halafu unakutana na timu kama Lipuli unaanza kudefendi unawaleta golini kwako kwani wasikudhuru?

Mbaya zaidi viungo washambuliaji unawaweka benchi unategemea nini. Mo bana kata huyo mtu timu mpe Djuma tushangilie magoli hata Pele alisema mpira ni magoli. Kocha nayeogopa kufungwa huyo sio kocha kabisa.

Acha timu icheze mpira ishambulie ikitokea kufungwa ni bahati mbaya kwani hata Barca, Real, Man U, Man Cityy n.k. mbona wanachezea tu vichapo mara kibao.
 
Ngoja kwanza nipate uhakika wa hizi info. Kama ni kweli kumwacha Gyan ni upuuzi mkubwa sana. Halafu huyo mfaransa mwenyewe kimeo hana hadhi ya kulipwa 40m
 
Bakiza Gyan.. Toa Mseja.
Niyonzima ajipange hiyo nafasi yake tunaweza kuleta hata kifaa zaidi yake
 
Ndio hapo sasa unamuacha Nyonzima unamtoa Gyan,kweli?
Simba watakapofeli ni hapa.Unamuacha vesatile player kama Gyan although si mzuri kihivyo unamuacha Niyonzima ambaye am very sure hatapata nafasi msimu ujao First eleven.Kama ingewezekana kuvunja mkataba wa Niyo kwakweli wangemfungashia Virago.Haina haja ya kua na Foreigner lakini anaanzia nje.Hata huyo Gyan si mzuri kihiiiiivyo.CAF CL Simba wajipange,Wasajili Wanaume na si wavulana.Haya....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…