‘Panya Road’ wafikishwa Mahakamani, wasomewa mashitaka nane

‘Panya Road’ wafikishwa Mahakamani, wasomewa mashitaka nane

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374

Kundi la watuhumiwa wa uhalifu ambao wengi wao ni vijana maarufu kwa jina la ''Panya Road'' wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala Kinyerezi Jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za unyang'anyi wa kutumia silaha (mapanga).

Mtuhumiwa wa kwanza Daud Abdallah, 22, Mkazi wa Tungini pamoja na wenzake 16 walifikishwa mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Fadhili Luvinga kusomewa mashtaka nane yanayowakabili.

Waendesha Mashtaka, Mawakili wa Serikali, Michael Ng'hoboko, Avelina Ombock na Nancy Mushumbusi walidai kuwa watuhumiwa kwa pamoja walitenda makosa hayo tarehe 24/04/2022 maeneo ya Chanika Ilala Jijini Dar es Salaam.

Watuhumiwa hao kwa pamoja na wengine ambao bado wanatafutwa walifanya matukio kwa Wananchi mbalimbali kwa kutumia mapanga na kujeruhi kwa lengo la kupora mali.

Waendesha Mashtaka walidai upelelezi wa shauri hilo umekamilika na waliomba tarehe kwa ajili ya kusikiliza hoja za awali.

Watuhumiwa wote walikana mashtaka yao. Kesi hiyo iliahirishwa mpaka tarehe 27/5/2022 na wamepelekwa rumande kwa kuwa makosa waliyoshtakiwa nayo hayana dhamana.
 
Wakae lodge ya serikali mpaka watie akili Kama yule mama Zumarini kule kwa shemeji zangu.
 
Sheria kweli shiiida, yaani mtu anayeua unampeleka mahakamani ili iweje,
Sheria ni sheria kweli
 

Kundi la watuhumiwa wa uhalifu ambao wengi wao ni vijana maarufu kwa jina la ''Panya Road'' wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala Kinyerezi Jijini Dar es Salaam kwa tuhuma za unyang'anyi wa kutumia silaha (mapanga).

Mtuhumiwa wa kwanza Daud Abdallah, 22, Mkazi wa Tungini pamoja na wenzake 16 walifikishwa mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Fadhili Luvinga kusomewa mashtaka nane yanayowakabili.

Waendesha Mashtaka, Mawakili wa Serikali, Michael Ng'hoboko, Avelina Ombock na Nancy Mushumbusi walidai kuwa watuhumiwa kwa pamoja walitenda makosa hayo tarehe 24/04/2022 maeneo ya Chanika Ilala Jijini Dar es Salaam.

Watuhumiwa hao kwa pamoja na wengine ambao bado wanatafutwa walifanya matukio kwa Wananchi mbalimbali kwa kutumia mapanga na kujeruhi kwa lengo la kupora mali.

Waendesha Mashtaka walidai upelelezi wa shauri hilo umekamilika na waliomba tarehe kwa ajili ya kusikiliza hoja za awali.

Watuhumiwa wote walikana mashtaka yao. Kesi hiyo iliahirishwa mpaka tarehe 27/5/2022 na wamepelekwa rumande kwa kuwa makosa waliyoshtakiwa nayo hayana dhamana.
Yaani watoto wamekana mashtaka?? Wamefundishwa na nani??

Tangu Hawa wangese wameanza hii tabia yao walinikumbusha enzi za seven comand,ambao sisi tulikuwa madong hata wakitukuta, wanaomba poo na kuomba sh 50. Nilikuwa nawaza Nina kibisu changu cm7 hiv kikali wembe unasubiri,wakinisogelea nikianza kukata shingo zao, si wataandamana kunitafuta Mimi?
 
Back
Top Bottom