Papa Fransis asema walitaka kumuua alipokuwa Iraq 2021

Papa Fransis asema walitaka kumuua alipokuwa Iraq 2021

Suley2019

JF-Expert Member
Joined
Oct 7, 2019
Posts
2,203
Reaction score
5,610
Kiongozi wa Kanisa Katoliki, Papa Francis, amefichua siri kuwa Watu walipanga kumuua wakati akiwa safarini nchini Iraq March 2021 lakini mauaji hayo yalizuiwa baada ya kupata taarifa za kiintelejensia kutoka Nchini Uingereza.

Papa amefichua njama hizo za jaribio la mauaji yake kwenye kitabu cha maisha yake kinachoitwa ‘Hope’ ambacho kinatarajiwa kuchapishwa January 14,2025 ambapo amesema baada ya kutua Baghdad mwezi March 2021, aliambiwa kuhusu tukio hilo ambalo lilipangwa kutekelezwa na Washambuliaji wawili wa kujitoa mhanga ambao wote walikamatwa na kuuawa.

Sehemu ya kilichomo kwenye kitabu chake hicho imechapishwa na gazeti la Italia Corriere della Ser ambapo pamoja na mambo mengine imeeleza kuwa wakati anajiandaa kuifanya ziara yake hiyo ya siku tatu Iraq wakati wa janga la corona, kila Mtu alimshauri asiifanye lakini aliona ni bora aifanye na kusema sababu ya kuambiwa asiende Iraq ni kufuatia Nchi hiyo kukumbwa na ongezeko la ghasia za kimadhehebu na mapigano kati ya Waislamu wa Shia na Sunni pamoja na mateso ya dini ndogo na kupelekea Jumuiya ya Wakristo Nchini humo kupungua kwa kiasi kikubwa wakati huo baada ya kulengwa hasa na kundi la Islamic State na Wafuasi wengine wa itikadi kali za Kisunni.

Amesema njama hiyo ya kutaka kuuawa ilifichuliwa na Majasusi wa Uingereza, ambao walionya Polisi wa Iraq na wao kwa upande wao walimweleza maelezo yake ya usalama mara tu alipowasili “Mwanamke aliyejaa vilipuzi, kijana mlipuaji wa kujitoa mhanga, alikuwa akielekea Mosul kujilipua wakati wa ziara yangu na gari pia lilikuwa limeondoka kwa kasi kubwa kwa nia hiyohiyo.”

Papa amesema alimuuliza Afisa wa Usalama siku iliyofuata nini kimewapata Washambuliaji hao na alijibu kwa unyonge “Hawapo tena, Polisi wa Iraq walikuwa wamewakamata na kuwalipua”
 
Mimi kila siku huwaga nawaza ina maana Pope Francis huwaga haogopi kufa maana unakuta anashikana mkono na kila mtu na anaenda kila sehemu hatalishi
 
Waarab na mauaji ya kujitoa muhanga ni kama jino na fizi. Hao watu wanawaza mauaji from left right to the centre.
 
Mimi kila siku huwaga nawaza ina maana Pope Francis huwaga haogopi kufa maana unakuta anashikana mkono na kila mtu na anaenda kila sehemu hatalishi
Pope ana ulinzi kama tu ilivyo kwa rais wa US kwa mfano. So unapoona pope anashikana mikono na kila mtu (hao akina 'kila mtu' sio kila mtu kama unavyodhani).

Papa ana security detail iliyosheheni yenye wataalamu na vifaa vya kiintelijensia vya kisasa kama tu rais wa US.

So mfano hiyo ziara yake sio kwamba anaamka tu anasema "leo twende Iraq". Hapana kuna maandalizi makubwa sana na hayo ndio yanayopelekea mpaka kupatikana kwa intel kama hizo za makusudio ya mashambulizi na watu wa usalama wanafanya yao.

Kwamfano hapo unaona ni polisi wa Iraq ndio waliwakama hao watu lakini Intel imetoka pengine na kama hao polisi wasinge act haraka kuzuia hilo jaribio basi ngazi ya mbele zaidi ingehusika.

Kuwashirikisha local police ni masuala ya jurisdiction tu ila wangeshindwa haimaanishi papa angeuwawa.
 
Pope ana ulinzi kama tu ilivyo kwa rais wa US kwa mfano. So unapoona pope anashikana mikono na kila mtu (hao akina 'kila mtu' sio kila mtu kama unavyodhani).

Papa ana security detail iliyosheheni yenye wataalamu na vifaa vya kiintelijensia vya kisasa kama tu rais wa US.

So mfano hiyo ziara yake sio kwamba anaamka tu anasema "leo twende Iraq". Hapana kuna maandalizi makubwa sana na hayo ndio yanayopelekea mpaka kupatikana kwa intel kama hizo za makusudio ya mashambulizi na watu wa usalama wanafanya yao.

Kwamfano hapo unaona ni polisi wa Iraq ndio waliwakama hao watu lakini Intel imetoka pengine na kama hao polisi wasinge act haraka kuzuia hilo jaribio basi ngazi ya mbele zaidi ingehusika.

Kuwashirikisha local police ni masuala ya jurisdiction tu ila wangeshindwa haimaanishi papa angeuwawa.
Unamjua rais Samia?

Fuatilia ziara za rais Samia na ziara za pope Francis ujifunze kitu

Kuna unatofauti mkubwa sana
 
"Mwanamke aliyejaa vilipuzi, kijana mlipuaji wa kujitoa mhanga, alikuwa akielekea Mosul kujilipua wakati wa ziara yangu na gari pia lilikuwa limeondoka kwa kasi kubwa kwa nia hiyohiyo.”

Religion of pease
 
"Mwanamke aliyejaa vilipuzi, kijana mlipuaji wa kujitoa mhanga, alikuwa akielekea Mosul kujilipua wakati wa ziara yangu na gari pia lilikuwa limeondoka kwa kasi kubwa kwa nia hiyohiyo.”

Religion of pease
Sio pieces
 
Back
Top Bottom