Paramount Chief Thomas Marealle katika nyaraka za Rajabu Ibrahim Kirama 1950s

Paramount Chief Thomas Marealle katika nyaraka za Rajabu Ibrahim Kirama 1950s

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
KUMBUKUMBU KIFO CHA MANGI MKUU THOMAS MAREALLE 14 FEBRUARY 2007: PARAMOUNT CHIEF THOMAS MAREALLE KATIKA NYARAKA ZA RAJABU IBRAHIM KIRAMA WA MACHAME NKUU

Mara yangu ya kwanza kusoma historia ya Mangi Mkuu Thomas Marealle ilikuwa ndani ya Nyaraka za Sykes wakati natafiti kitabu cha maisha ya Abdul Sykes.

Kwa bahati mbaya sikuweza kutumia yale niliyosoma katika kitabu nilichokuja kuandika kwa kuwa mengi katika yale niliyosoma yaikuwa mambo binafsi zaidi kuliko historia ya TANU na harakati za kudai uhuru ingawa jina la Nyerere lilikuwa likijitokeza.

Nimekuja kukutana tena na Mangi Mkuu Thomas Marealle baada ya kiasi cha miaka 30 kupita katika Nyaraka za Rajabu Ibrahim Kirama wakati natafiti maisha ya Mzee Rajabu wa Machame Nkuu.

Napenda kama kumbukumbu ya kifo cha Mangi Mkuu nieleze machache katika yale ambayo nimejifunza katika kusoma barua walizokuwa wakiandikiana watu hawa wawili kutoka Kilimanjaro kila mmoja akiwa na nafasi muhimu katika jamii ya kabila la Wachagga.

Thomas Marealle akiwa kwanza Mangi wa Marangu kisha Mangi Mkuu wa Wachagga, Rajabu Kirama yeye akiwa kiongozi wa Waislam na mtu aliyeueneza Uislam Uchaggani akianzia harakati zake kijijini kwake Machame Nkuu katika miaka ya 1930.

Harakati hizi zilileta uadui mkubwa kati yake na Chief Shangali.

Mwishoni wa miaka ya 1800 Wajerumani baada ya kuchoshwa na vita visivyokwisha baina ya Wachagga wenyewe kwa wenyewe waliamua kuwakamata takriban mangi wote isipokuwa Shangali na Marealle.

Jumla ya mangi 19 walinyongwa hadharani isipokuwa Chief Marealle na Chief Shangali.

Haya ndiyo madhila yaliyowakumba Wachagga chini ya utawala wa Wajerumani.

Watoto wa machifu hawa wawili hata hivyo walikuja kupata nguvu kubwa sana katika utawala wa Waingereza.

Katika utawala wa Waingereza na katika hali ya amani na utawala Wachagga waliunda chama - Kilimanjaro Chagga Citizens Union (KCCU) (Umoja wa Raia wa Kilimanjaro).

Petro Njau akiwa kiongozi wa chama hiki alipewa jukumu la kusimamia maslahi ya Wachagga kama taifa.

Katika kanuni za KCCU kanuni hizi zinawataja Wachagga kama watu waliozaliwa huru na wenye haki ya kulinda uhuru wao.

Petro Njau alikinadi chama hiki kuwa ni ‘’chama cha siasa cha kikabila.’’

Nilipokuwa nasoma Nyaraka za Rajabu Ibrahim Kirama nilishangaa sana kusoma kuwa Wachagga kwa asili waliichukulia Kilimanjaro yote kuwa ni nchi.

Nyaraka za KCCU zimejaa maneno ya itikadi ya: ‘’nchi,’’ ‘’taifa,’’ ‘’raia,’’ ‘’uchaguzi,’’ ‘’kura,’’ na ‘’utawala.’’

Petro Njau Rajabu na Ibrahim Kirama walikuwa wanaunganishwa na kukubaliana katika jambo moja kubwa na muhimu sana katika utawala wa Wachagga nalo ni kuwa Mangi walikuwa na nguvu zilizopea wakati raia wao hawakuwa na sauti yoyote.

Kwa ajili hii basi wanastahili kuondolewa wote na awekwe kiongozi mmoja tu atakaetawala Kilimanjaro yote na Wachagga wote.

Petro Njau alikuwa mwandishi wa Mzee Rajabu na pia mwandishi wa Chief Thomas Marealle pale Kilimanjaro ilipokuwa katika siasa za uchaguzi kutafuta Mangi Mkuu atakaekuwa juu ya Mangi wote, yaani Paramount Chief.

Rajabu Kirama alisimama bega kwa bega na Petro Njau katika fikra hii.

Thomas Marealle na Abdiel Shangali ndiyo walikuwa wanagombea nafasi ya Mangi Mkuu na bahati mbaya sana kwa Abdiel Shangali ni kuwa alikuwa na uadui mkubwa na Rajabu Ibrahim Kirama.

Rajabu Kirama akasimama kumsaidia Chief Marealle awe kiongozi wa Wachagga wote.

Hivi ndivyo Thomas Marealle alivyokuja kuchaguliwa kuwa Paramount Chief, yaani Mangi Mkuu.

Picha: Mzee Rajabu Ibrahim Kirama, Mangi Mkuu Thomas Marealle wa Marangu na Chief Abdiel Shangali wa Machame.

Screenshot_20220214-165051_Facebook.jpg
 
Nasaha za bure kama tupo Class vile - Fa.
Ahsante Mzee Saidi
 
we mzee kila kitu ni sykes tuu
Lokonga,
Katika maajabu niliyokutananayo ni hii historia ya Sykes.

Kila utakaemkuta katika historia ya Tanganyika yumo katika nyaraka zao.

Ajabu kubwa sana.
Unadhani nafanya utani?

Nimesoma barua za Chief Thomas Marealle katika nyaraka hizo.
Wanaelezana mambo makubwa ya hali ya baadae ya Tanganyika.

Bahati mbaya siwezi kueleza hayo kwa kuwa yalikuwa mazungumzo binafsi sana.
Unaumia kuwa kuna watu Allah aliwanyanyua kupita wengine.

Tungefahamu vipi historia ya Nyerere kama si nyaraka hizi za Sykes?

Nilialikwa Northwestern University Evanston Chicago kufanya mhadhara juu ya Abdul Sykes.

Hiki chuo ndiyo kinaongoza ulimwenguni katika African History.

Sikutegemea hata kwa mbali kama haya mambo yatakuwa makubwa kiasi hiki.

Yuko publisher aliposoma mswada wa kitabu cha Abdul Sykes aliniambia kuwa mswada wangu ni mgodi wa dhahabu.

Lakini aliogopa kuchapa kitabu changu.
Miaka hiyo mimi kijana kiasi miaka 30.

Samahani sana kama unatabishwa na kalamu yangu.
Kitabu kinakwenda toleo la tano.

Screenshot_20220214-182928_Photos.jpg


Screenshot_20220214-183341_Photos.jpg
 
Lokonga,
Katika maajabu niliyokutananayo ni hii historia ya Sykes.

Kila utakaemkuta katika historia ya Tanganyika yumo katika nyaraka zao.

Ajabu kubwa sana.
Unadhani nafanya utani?

Nimesoma barua za Chief Thomas Marealle katika nyaraka hizo.

Wanaelezana mambo makubwa ya hali ya baadae ya Tanganyika.

Bahati mbaya siwezi kueleza hayo kwa kuwa yalikuwa mazungumzo binafsi sana.

Unaumia kuwa kuna watu Allah aliwanyanyua kupita wengine.

Tungefahamu vipi historia ya Nyerere kama si nyaraka hizi za Sykes?

Nilialikwa Northwestern University Evanston Chicago kufanya mhadhara juu ya Abdul Sykes.

Hiki chuo ndiyo kinaongoza ulimwenguni katika African History.

Sikutegemea hata kwa mbali kama haya mambo yatakuwa makubwa kiasi hiki.

Yuko publisher aliposoma mswada wa kitabu cha Abdul Sykes aliniambia kuwa mswada wangu ni mgodi wa dhahabu.

Lakini aliogopa kuchapa kitabu changu.

Miaka hiyo mimi kijana kiasi miaka 30.

Samahani sana kama unatabishwa na kalamu yangu.

Kitabu kinakwenda toleo la tano.

View attachment 2119388

View attachment 2119390
kuwa serious mzee
 
Huyo chifu mpaka sasa amefanya wakibosho na wamachame hawaivani hata kuoleana,na suo hilo tuu hata nyumba mkibosho akijenga ni marufuku kugeuzia mlango usawa wa machame..
Nje ya mada;niliwahi ambiwa na mzee wangu kuwa huyu mariale haikuwa ukoo wake bali ni neno lilitokana na kupishana kauli baina ya mtu aliekuwa anamuulizia huyu mangi alikuwa amelala sasa akaja mzung kumtembelea sasa yule msaidizi wa chifu akamjibu (mangi nale))yaani kwa kichaga ni mangi kalala)sasa yule jamaa akasindwa kutamka lile neno akasemaa marialeee marialeeee ndio likawa chimbuko la kijiita jina hilo mariale mariale hadi likazoeleka.ila ukoo kabisa aliokuwa akitumia ni (mushi)

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kuwa serious mzee
Lokongo,
Ulianza kwa kuniita, "Wee mzee."
Si adabu.

Lakini nilinyamaza na nikakujibu kistaarabu.

Jibu hilo hapo juu.
Sasa umekuja na "kuwa serious mzee."

Kwangu hiyo ni kebehi na kejeli.
Unataka kujua njoo kwangu na adabu zako kamili tutajadili.

Yale niyajuayo nitakufahamisha na nisiyoyajua nitakueleza kuwa sijui.
Huna sababu ya kutukana.
 
Historia inaendelea
Buji...
Kuna mtu kaghadhibika kwa nini anatajwa Sykes katika historia ya uhuru wa Tanganyika.
Kuna mtu jana na yeye alikuja barzani amechukia kisa ni historia ya Sykes.

Kaiita ''Fake.''

Alitoa ahadi kuwa atarejea barzani.
Namsubiri.

Bado hajarejea.

Kuna mtu alipata kuniuliza kwa nini namtaja Abdul Sykes katika kila niapoizungumza historia ya TANU na harakati za kupigania uhuru?

Jibu zuri zaidi ya nililompa nilikuwanalo lakini niliona ili apate uelewa zaidi na kwa haraka nilijibu swali lake kwa kumuuliza yeye swali.

Nilimuuliza, ''Je unaweza kueleza historia ya Ujamaa Vijijini bila ya kumtaja Julius Nyerere?''

Jibu lake lilikuwa haiwezekani.

''Kwa nini haiwezekani?''
''Haiwezekani kwa sababu Julius Nyerere ndiye aliyeasisi siasa ya Ujamaa Vijijini,'' alijibu.

Nikamwambia kuwa hawa akina Sykes baba yao ni Katibu muasisi wa African Association 1929 iliyokuja kuzaa TANU 1954 na watoto wake wote walikuwa ndani ya TAA na walikuja kuunda TANU pamoja na Mwalimu Nyerere.

Ukiwatoa hawa akina katika historia ya TANU tutakuwa hatuna historia ya kweli kwani Mwalimu atapwaya sana kutajwa peke yake kama muasisi wa harakati za siasa Tanganyika kwa sababu nyingi tu.
 
KUMBUKUMBU KIFO CHA MANGI MKUU THOMAS MAREALLE 14 FEBRUARY 2007: PARAMOUNT CHIEF THOMAS MAREALLE KATIKA NYARAKA ZA RAJABU IBRAHIM KIRAMA WA MACHAME NKUU

Mara yangu ya kwanza kusoma historia ya Mangi Mkuu Thomas Marealle ilikuwa ndani ya Nyaraka za Sykes wakati natafiti kitabu cha maisha ya Abdul Sykes.

Kwa bahati mbaya sikuweza kutumia yale niliyosoma katika kitabu nilichokuja kuandika kwa kuwa mengi katika yale niliyosoma yaikuwa mambo binafsi zaidi kuliko historia ya TANU na harakati za kudai uhuru ingawa jina la Nyerere lilikuwa likijitokeza.

Nimekuja kukutana tena na Mangi Mkuu Thomas Marealle baada ya kiasi cha miaka 30 kupita katika Nyaraka za Rajabu Ibrahim Kirama wakati natafiti maisha ya Mzee Rajabu wa Machame Nkuu.

Napenda kama kumbukumbu ya kifo cha Mangi Mkuu nieleze machache katika yale ambayo nimejifunza katika kusoma barua walizokuwa wakiandikiana watu hawa wawili kutoka Kilimanjaro kila mmoja akiwa na nafasi muhimu katika jamii ya kabila la Wachagga.

Thomas Marealle akiwa kwanza Mangi wa Marangu kisha Mangi Mkuu wa Wachagga, Rajabu Kirama yeye akiwa kiongozi wa Waislam na mtu aliyeueneza Uislam Uchaggani akianzia harakati zake kijijini kwake Machame Nkuu katika miaka ya 1930.

Harakati hizi zilileta uadui mkubwa kati yake na Chief Shangali.

Mwishoni wa miaka ya 1800 Wajerumani baada ya kuchoshwa na vita visivyokwisha baina ya Wachagga wenyewe kwa wenyewe waliamua kuwakamata takriban mangi wote isipokuwa Shangali na Marealle.

Jumla ya mangi 19 walinyongwa hadharani isipokuwa Chief Marealle na Chief Shangali.

Haya ndiyo madhila yaliyowakumba Wachagga chini ya utawala wa Wajerumani.

Watoto wa machifu hawa wawili hata hivyo walikuja kupata nguvu kubwa sana katika utawala wa Waingereza.

Katika utawala wa Waingereza na katika hali ya amani na utawala Wachagga waliunda chama - Kilimanjaro Chagga Citizens Union (KCCU) (Umoja wa Raia wa Kilimanjaro).

Petro Njau akiwa kiongozi wa chama hiki alipewa jukumu la kusimamia maslahi ya Wachagga kama taifa.

Katika kanuni za KCCU kanuni hizi zinawataja Wachagga kama watu waliozaliwa huru na wenye haki ya kulinda uhuru wao.

Petro Njau alikinadi chama hiki kuwa ni ‘’chama cha siasa cha kikabila.’’

Nilipokuwa nasoma Nyaraka za Rajabu Ibrahim Kirama nilishangaa sana kusoma kuwa Wachagga kwa asili waliichukulia Kilimanjaro yote kuwa ni nchi.

Nyaraka za KCCU zimejaa maneno ya itikadi ya: ‘’nchi,’’ ‘’taifa,’’ ‘’raia,’’ ‘’uchaguzi,’’ ‘’kura,’’ na ‘’utawala.’’

Petro Njau Rajabu na Ibrahim Kirama walikuwa wanaunganishwa na kukubaliana katika jambo moja kubwa na muhimu sana katika utawala wa Wachagga nalo ni kuwa Mangi walikuwa na nguvu zilizopea wakati raia wao hawakuwa na sauti yoyote.

Kwa ajili hii basi wanastahili kuondolewa wote na awekwe kiongozi mmoja tu atakaetawala Kilimanjaro yote na Wachagga wote.

Petro Njau alikuwa mwandishi wa Mzee Rajabu na pia mwandishi wa Chief Thomas Marealle pale Kilimanjaro ilipokuwa katika siasa za uchaguzi kutafuta Mangi Mkuu atakaekuwa juu ya Mangi wote, yaani Paramount Chief.

Rajabu Kirama alisimama bega kwa bega na Petro Njau katika fikra hii.

Thomas Marealle na Abdiel Shangali ndiyo walikuwa wanagombea nafasi ya Mangi Mkuu na bahati mbaya sana kwa Abdiel Shangali ni kuwa alikuwa na uadui mkubwa na Rajabu Ibrahim Kirama.

Rajabu Kirama akasimama kumsaidia Chief Marealle awe kiongozi wa Wachagga wote.

Hivi ndivyo Thomas Marealle alivyokuja kuchaguliwa kuwa Paramount Chief, yaani Mangi Mkuu.

Picha: Mzee Rajabu Ibrahim Kirama, Mangi Mkuu Thomas Marealle wa Marangu na Chief Abdiel Shangali wa Machame.

View attachment 2119338
Naungana na wale wasemao kuwa bila kumtaja Sykes na kuwekamo Mwislamu au Uislamu bandiko au andiko lako halikamiliki. Kama mwana htoria, huoni umuhimu wa historia hai kuliko historia ya kutafuta vitabuni au kuelezwa. Kama ulivyoandika Mangi Marealle amefariki 2007 na umdai ulikuwa unataka saana kupata historia ya huko Uchaggani, kwa nini hukumtafuta miaka yote hiyo. Pia, huko Uchaggani kuna wazee wengi ambao wangekupa taarifa hizi za kihistoria, lakini wewe ukaenda North Western University huko Illinois, USA kupata hizo habari. Hizo taarifa ulizosoma au kupata ni second hand (za kuambiwa), nenda ukapate hizo taarifa toka wenyewe. Nimeona umechomekea mzee Mwislamu, lakini kila nikijariba kuangalia sijaona uhusiano zaidi Uislamu wako unakufanya kila kitu lazima kuchomekea Uislamu, Mwislamu, Sykes!!!. Nenda kwa ukoo wa Marreale, wanazo kumbukumbu kedekede kuhusu historia za Uhagani. Achana na historia za kuambiwa peke yake.
 
Naungana na wale wasemao kuwa bila kumtaja Sykes na kuwekamo Mwislamu au Uislamu bandiko au andiko lako halikamiliki. Kama mwana htoria, huoni umuhimu wa historia hai kuliko historia ya kutafuta vitabuni au kuelezwa. Kama ulivyoandika Mangi Marealle amefariki 2007 na umdai ulikuwa unataka saana kupata historia ya huko Uchaggani, kwa nini hukumtafuta miaka yote hiyo. Pia, huko Uchaggani kuna wazee wengi ambao wangekupa taarifa hizi za kihistoria, lakini wewe ukaenda North Western University huko Illinois, USA kupata hizo habari. Hizo taarifa ulizosoma au kupata ni second hand (za kuambiwa), nenda ukapate hizo taarifa toka wenyewe. Nimeona umechomekea mzee Mwislamu, lakini kila nikijariba kuangalia sijaona uhusiano zaidi Uislamu wako unakufanya kila kitu lazima kuchomekea Uislamu, Mwislamu, Sykes!!!. Nenda kwa ukoo wa Marreale, wanazo kumbukumbu kedekede kuhusu historia za Uhagani. Achana na historia za kuambiwa peke yake.
ksk,
Kwani hairuhusiwi kuandikwa historia ya Abdul Sykes?
Nadhani hili tatizo tumeshalimaliza toka 1998 kitabu chake kilipochapwa London.

Kwani hairuhusiwi kuandikwa historia ya Waislam katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika?

Nadhani tatizo hili tulilimaliza toka 1998 nilipoandika kitabu kuhusu''...The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika.''

Unazungumzia historia hai.

Nimekuwekea hapo kitabu cha maisha ya Rajabu Ibrahim Kirama (2020) hicho kitabu ndicho kilichonipeleka Machame Nkuu kufanya utafiti na nikakiandika.

Northwestern University, Chicago nilialikwa mwaka wa 2011 kwa kufanya mahadhara kuhusu historia hii tunayojadili hapa.

Nilialikwa kuzungumza siyo kutafiti.

Baada ya hapo nikaalikwa Zentrum Moderner Orient (ZMO) Berlin kwa ajili ya utafiti wa historia ya Tanzania na nikapewa uhuru wa kuandika nitakacho.

Nilitafiti na kuandika, ''Tanzania: A Nation Without Heroes.''
Kuhusu Rajabu Ibrahim Kirama ''sikuchomeka,'' chembelecho.

Nilikwenda Machame kufanya utafiti wa maisha yake kama mtu aliyeeneza Uislam Uchaggani.

Hakika mimi utafiti wangu umejikita katika historia ya Waislam kwani kama sitafanya hivyo hakuna wa kutafiti na kunusuru historia hii isipotee.

Hebu fikiri historia hii ya Abdul Sykes ilikuwa imefutwa kwa zaidi ya miaka 50 tukawa na historia ya ''ajabu,'' isiyoelezeka wapi ilikotokea na sababu yake nini?

Historia ya Wachagga imeshaandikwa.
Bruno Gutmann ameandika mengi katika historia hii.

Leo mimi nina haja gani ya kuandika historia ya Chief Marealle ambayo tayari imeshaandikwa?

Nimemwandika Rajabu Ibrahim Kirama na baba yake Muro Mboyo ambae licha ya kuwa alimpokea Gutmann Old Moshi na kumpa ardhi ajenge kanisa hakuna popote katika historia ya kanisa Uchagani ametajwa.

Kwa nini iwe ivi?

Huu ndiyo mzigo wangu niliojitwika.
Kuwapa jukwaa na sauti wale ambao historia imewapuuza na kuwasahau.

Unachotakiwa kufanya ni wewe kuacha kunisoma kwani kila ukifungua makala yangu utawasoma Waislam ambao wewe historia yao haikufurahishi.

1644866723817.png

Kulia ni msikiti wa kwanza Machame Nkuu na kushoto shule ya kwanza ya Waislam hapo Nkuu majengo yote yamejengwa na Mzee Rajabu Ibrahim Kirama akishirikiana na Waislam wa Nkuu.

Msikiti ulimalizwa kujengwa tarehe 23 Novemba 1930.
 
Ndugu zanguni,
Kuna mtu hakuniamini nilipomwambia kuwa kila mzalendo aliyehusika katika kupigania uhuru wa Tanganyika nimemsoma katika Nyaraka za Sykes.

Akaniambia, ''Mzee be serious...''
Hakuamini niliyoandika kaona nafanya maskhara.

Nilimpa jibu.
Sikumuonyesha majina ya hawa wazalendo.

Leo asubuhi nimeamka na fikra mpya kuwa kwa faida ya barza niweke kipande hicho hapo chini na vitu vingine kidogo ili yeye na sisi sote tunufaike:

''Ally Sykes alinifahamisha kuwa kumbukumbu hizi zilikuwa ndani ya sefu ambayo haikupatwa kufunguliwa kwa zaidi ya miaka 30.

Nikiyapitia majalada yake nilishangazwa na utaratibu wa Ally Sykes wa kupanga kila kitu na kila kipande cha habari mahali pake hata kingekuwa kidogo namna gani wakati ule wa harakati.

Ally Sykes ana barua ya mwaka 1954 iliyoandikwa kwa penseli toka kwa Zuberi Mtemvu kwenda kwake akimtaarifu juu ya mazungumzo aliyokuwanayo (Mtemvu) na Nyerere kuhusu yeye na TANU.

Stakabadhi ya hundi ya posta toka kwa Ally Sykes kwenda kwa Japhet Kirilo wakati wa Mgogoro wa Ardhi ya Wameru.

Nakala ya barua isiyokuwa na tarehe kutoka TAA kwenda kwa Malkia Elizabeth iliyotiwa saini na viongozi wote wa TAA: Rais Julius Nyerere, Makamu wa Rais Abdulwahid Sykes, Katibu Mkuu Dome Okochi, Naibu Katibu Dossa Aziz, Mweka Hazina John Rupia, Naibu Mweka Hazina Ally Sykes ikimpongeza Malkia kwa kutawazwa.

Barua ya mwaka 1952 toka kwa Rashid Mfaume Kawawa kutoka Bukoba kwenda kwa Ally Sykes ikimfahamisha juu ya hali ya siasa katika Kanda ya Ziwa.

Barua ya mwaka 1963 toka kwa Lady Judith Listowel, Kenneth Kaunda, Julius Nyerere, Kasella Bantu, Chifu Thomas Marealle ...orodha haina mwisho.

Baadaye nilipofanya utafiti kuhusu maisha ya baba yake, Kleist Sykes, nilikuja kufahamu kwamba tabia hii ilirithiwa kutoka kwa baba yake ambae alikuwa akiweka ndani ya jalada kila kipande cha karatasi kilichokuwa na habari iliyostahili kukumbukwa.

Ni jambo la kuhuzunisha kuwa sikuweza kupewa shajara za Abdulwahid ambazo nilielezwa kwamba baadhi ziko katika hati-mkato na hadi leo hazijafasiriwa.

Shajara hizi nimezioana kwa macho yangu lakini kwa kukosa idhini sikuweza kuzifungua na kuzisoma.

Vilevile vsikuweza kupata kumbukumbu halisi za Vita Kuu ya Kwanza zilizoandikwa na Kleist Sykes kwa mkono wake mwenyewe.

Hapana shaka yoyote kwamba nyaraka hizi ni hazina zenye thamani isiyo na mfano wake.

Ni matumaini yangu kwamba siku moja nchi yetu itakubali na kuthamini mchango wa Abdulwahid Kleist Sykes katika taifa la Tanzania na nyaraka hizi kama kielelezo cha harakati dhidi ya ukoloni, zitakubalika na zitawekwa chini ya hifadhi ya Nyaraka za Taifa kwa faida ya vizazi vijavyo.''

(Kutoka ''Maisha na Nyakati za Abdulwahid Sykes...'' (1998).

Picha hizo hapo chini Dome Okochi Budohi Katibu Mkuu TAA 1953 na picha ya Kenneth Kaunda na Julius Nyerere wote hawa nimewasoma katika Nyaraka za Sykes.

''Be serious indeed'' be serious usidhani mimi niko hapa kufanya mchezo.


1644898791002.png


1644899494751.png
 
We mzee wa ajabu sana,historia ya uchagani huko unataka kutwambia Marealle asingekua chief bila huyo ulamaa nani sijui.?
Umada zako nzuri ukichomekea udini unaharibu.
 
We mzee wa ajabu sana,historia ya uchagani huko unataka kutwambia Marealle asingekua chief bila huyo ulamaa nani sijui.?
Umada zako nzuri ukichomekea udini unaharibu.
Babu...
Tusifanye mjadala kwa lugha za hamaki na kuvunjiana adabu, "We Mzee..."

Huwezi kumwita mtu "Wee."

Ungeuliza tu, "Mzee unataka kutwambia..."

Sasa nakujibu.

Hakuna mahali niliposema kuwa Chief Thomas Marealle asingekuwa Mangi Mkuu bila ya msaada wa Mzee Rajabu Ibrahim Kirama.

Nilichosema ni kuwa Mzee Rajabu na watu wake wote Uchaggani walimuunga mkono Chief Thomas Marealle.

''Huyo ulama nani sijui..."
Umeghadhibika.

Maana ya udini ni kutuoa upendeleo kwa watu wa imani yako dhidi ya watu wa imani isiyokuwa yako.

Huu ndiyo udini.

Mimi nimetafiti historia ya Waislam wa Tanganyika, historia ambayo wanahistoria hawakuipa umuhimu.

Ukipenda kuita huu ni udini sikuzuii.
 
The usual, common, boring theme: The main hero in the mostly fictitious plot always turns out to be of Muslim faith, with the Sykes name thrown in here and there for good measure. Such narratives would qualify as bedtime stories for madrassah kids.
 
KUMBUKUMBU KIFO CHA MANGI MKUU THOMAS MAREALLE 14 FEBRUARY 2007: PARAMOUNT CHIEF THOMAS MAREALLE KATIKA NYARAKA ZA RAJABU IBRAHIM KIRAMA WA MACHAME NKUU

Mara yangu ya kwanza kusoma historia ya Mangi Mkuu Thomas Marealle ilikuwa ndani ya Nyaraka za Sykes wakati natafiti kitabu cha maisha ya Abdul Sykes.

Kwa bahati mbaya sikuweza kutumia yale niliyosoma katika kitabu nilichokuja kuandika kwa kuwa mengi katika yale niliyosoma yaikuwa mambo binafsi zaidi kuliko historia ya TANU na harakati za kudai uhuru ingawa jina la Nyerere lilikuwa likijitokeza.

Nimekuja kukutana tena na Mangi Mkuu Thomas Marealle baada ya kiasi cha miaka 30 kupita katika Nyaraka za Rajabu Ibrahim Kirama wakati natafiti maisha ya Mzee Rajabu wa Machame Nkuu.

Napenda kama kumbukumbu ya kifo cha Mangi Mkuu nieleze machache katika yale ambayo nimejifunza katika kusoma barua walizokuwa wakiandikiana watu hawa wawili kutoka Kilimanjaro kila mmoja akiwa na nafasi muhimu katika jamii ya kabila la Wachagga.

Thomas Marealle akiwa kwanza Mangi wa Marangu kisha Mangi Mkuu wa Wachagga, Rajabu Kirama yeye akiwa kiongozi wa Waislam na mtu aliyeueneza Uislam Uchaggani akianzia harakati zake kijijini kwake Machame Nkuu katika miaka ya 1930.

Harakati hizi zilileta uadui mkubwa kati yake na Chief Shangali.

Mwishoni wa miaka ya 1800 Wajerumani baada ya kuchoshwa na vita visivyokwisha baina ya Wachagga wenyewe kwa wenyewe waliamua kuwakamata takriban mangi wote isipokuwa Shangali na Marealle.

Jumla ya mangi 19 walinyongwa hadharani isipokuwa Chief Marealle na Chief Shangali.

Haya ndiyo madhila yaliyowakumba Wachagga chini ya utawala wa Wajerumani.

Watoto wa machifu hawa wawili hata hivyo walikuja kupata nguvu kubwa sana katika utawala wa Waingereza.

Katika utawala wa Waingereza na katika hali ya amani na utawala Wachagga waliunda chama - Kilimanjaro Chagga Citizens Union (KCCU) (Umoja wa Raia wa Kilimanjaro).

Petro Njau akiwa kiongozi wa chama hiki alipewa jukumu la kusimamia maslahi ya Wachagga kama taifa.

Katika kanuni za KCCU kanuni hizi zinawataja Wachagga kama watu waliozaliwa huru na wenye haki ya kulinda uhuru wao.

Petro Njau alikinadi chama hiki kuwa ni ‘’chama cha siasa cha kikabila.’’

Nilipokuwa nasoma Nyaraka za Rajabu Ibrahim Kirama nilishangaa sana kusoma kuwa Wachagga kwa asili waliichukulia Kilimanjaro yote kuwa ni nchi.

Nyaraka za KCCU zimejaa maneno ya itikadi ya: ‘’nchi,’’ ‘’taifa,’’ ‘’raia,’’ ‘’uchaguzi,’’ ‘’kura,’’ na ‘’utawala.’’

Petro Njau Rajabu na Ibrahim Kirama walikuwa wanaunganishwa na kukubaliana katika jambo moja kubwa na muhimu sana katika utawala wa Wachagga nalo ni kuwa Mangi walikuwa na nguvu zilizopea wakati raia wao hawakuwa na sauti yoyote.

Kwa ajili hii basi wanastahili kuondolewa wote na awekwe kiongozi mmoja tu atakaetawala Kilimanjaro yote na Wachagga wote.

Petro Njau alikuwa mwandishi wa Mzee Rajabu na pia mwandishi wa Chief Thomas Marealle pale Kilimanjaro ilipokuwa katika siasa za uchaguzi kutafuta Mangi Mkuu atakaekuwa juu ya Mangi wote, yaani Paramount Chief.

Rajabu Kirama alisimama bega kwa bega na Petro Njau katika fikra hii.

Thomas Marealle na Abdiel Shangali ndiyo walikuwa wanagombea nafasi ya Mangi Mkuu na bahati mbaya sana kwa Abdiel Shangali ni kuwa alikuwa na uadui mkubwa na Rajabu Ibrahim Kirama.

Rajabu Kirama akasimama kumsaidia Chief Marealle awe kiongozi wa Wachagga wote.

Hivi ndivyo Thomas Marealle alivyokuja kuchaguliwa kuwa Paramount Chief, yaani Mangi Mkuu.

Picha: Mzee Rajabu Ibrahim Kirama, Mangi Mkuu Thomas Marealle wa Marangu na Chief Abdiel Shangali wa Machame.

View attachment 2119338
Home-cooked garbage.
 
ksk,
Kwani hairuhusiwi kuandikwa historia ya Abdul Sykes?
Nadhani hili tatizo tumeshalimaliza toka 1998 kitabu chake kilipochapwa London.

Kwani hairuhusiwi kuandikwa historia ya Waislam katika historia ya TANU na uhuru wa Tanganyika?

Nadhani tatizo hili tulilimaliza toka 1998 nilipoandika kitabu kuhusu''...The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism in Tanganyika.''

Unazungumzia historia hai.

Nimekuwekea hapo kitabu cha maisha ya Rajabu Ibrahim Kirama (2020) hicho kitabu ndicho kilichonipeleka Machame Nkuu kufanya utafiti na nikakiandika.

Northwestern University, Chicago nilialikwa mwaka wa 2011 kwa kufanya mahadhara kuhusu historia hii tunayojadili hapa.

Nilialikwa kuzungumza siyo kutafiti.

Baada ya hapo nikaalikwa Zentrum Moderner Orient (ZMO) Berlin kwa ajili ya utafiti wa historia ya Tanzania na nikapewa uhuru wa kuandika nitakacho.

Nilitafiti na kuandika, ''Tanzania: A Nation Without Heroes.''
Kuhusu Rajabu Ibrahim Kirama ''sikuchomeka,'' chembelecho.

Nilikwenda Machame kufanya utafiti wa maisha yake kama mtu aliyeeneza Uislam Uchaggani.

Hakika mimi utafiti wangu umejikita katika historia ya Waislam kwani kama sitafanya hivyo hakuna wa kutafiti na kunusuru historia hii isipotee.

Hebu fikiri historia hii ya Abdul Sykes ilikuwa imefutwa kwa zaidi ya miaka 50 tukawa na historia ya ''ajabu,'' isiyoelezeka wapi ilikotokea na sababu yake nini?

Historia ya Wachagga imeshaandikwa.
Bruno Gutmann ameandika mengi katika historia hii.

Leo mimi nina haja gani ya kuandika historia ya Chief Marealle ambayo tayari imeshaandikwa?

Nimemwandika Rajabu Ibrahim Kirama na baba yake Muro Mboyo ambae licha ya kuwa alimpokea Gutmann Old Moshi na kumpa ardhi ajenge kanisa hakuna popote katika historia ya kanisa Uchagani ametajwa.

Kwa nini iwe ivi?

Huu ndiyo mzigo wangu niliojitwika.
Kuwapa jukwaa na sauti wale ambao historia imewapuuza na kuwasahau.

Unachotakiwa kufanya ni wewe kuacha kunisoma kwani kila ukifungua makala yangu utawasoma Waislam ambao wewe historia yao haikufurahishi.

View attachment 2119625
Kulia ni msikiti wa kwanza Machame Nkuu na kushoto shule ya kwanza ya Waislam hapo Nkuu majengo yote yamejengwa na Mzee Rajabu Ibrahim Kirama akishirikiana na Waislam wa Nkuu.

Msikiti ulimalizwa kujengwa tarehe 23 Novemba 1930.
Unamadini ya kutosha acha wanao chukia wachukie histori ni histori haijalishi itamfurahisha mtu au itamchikiza
 
The usual, common, boring theme: The main hero in the mostly fictitious plot always turns out to be of Muslim faith, with the Sykes name thrown in here and there for good measure. Such narratives would qualify as bedtime stories for madrassah kids.
Schmidt,
Nakuwekea hayo hapo chini usome tuendelee na mjadala:
Hakika kisa cha akina Sykes ni kisa mimi kimenikamata sana.

Utaona kuwa siko peke yangu katika hili.

Mimi hupenda kusema kuwa mtu yeyote ambae angepata bahati ya sema kuokota gunia ndani mna mafaili yenye nyaraka za Sykes angeyasoma yote na kisha angeandika kitabu.

Achilia ule udugu baina yetu lakini siku niliposoma kitabu, ''Modern Tanzanians,'' kitabu alichohariri John Iliffe na kusoma, ''The Townsman: The Life of Kleist Sykes,'' sura iliyoandikwa na mjukuu wa Kleist Sykes, Aisha ''Daisy'' Sykes Buruku historia hii ilikamata fikra zangu.

Ikiwa hujasoma kitabu hiki kitafute ukisome: 'Modern Tanzanians, John Iliffe (ed), East African Publishing House, Nairobi, 1973).

Nakumbuka kama vile jana nilikuwa katika Maktaba ya Taifa, Arusha ndipo nilipokikuta kitabu hiki.

Utafiti wangu wa kutaka kujua mengi ulianza siku ile.
Nikawauliza hawa ndugu zangu juu ya kitabu cha Iliffe.

Wakanifahamisha kuwa babu yao, Kleist Sykes kabla ya kufariki mwaka wa 1949 alikuwa ameandika ''kitabu,'' ambacho alimwachia mwanae Abdul Sykes.

Kwa hakika hakikuwa kitabu bali mswada wa kitabu.

Kleist kwa msaada wa mlezi wake Afande Plantan aliweza kuandika historia ya jeshi lile la Wazulu liliotoka Imhambane kuja Germanostafrika chini ya Hermann von Wissman kupambana na Abushiri bin Salim na Mtwa Mkwawa.

Mwanae Abdu Sykes, Aisha ''Daisy'' Sykes alipoingia Chuo Kikuu cha Afrika ya Mashariki mwaka wa 1967 kusoma Elimu na Historia ndipo alipokutana na Profesa wa Historia John Iliffe na huyu mwalimu wake baada ya kufahamu historia ya akina Sykes na yeye kama mimi akakumbwa na hii ''obsession,'' akataka kujua mengi vipi walifika Tanganyika kutoka Afrika ya Kusini.

Iliffe akampa Daisy ''assignment,'' ya kumkusanyia histori ya ukoo wake.

Hapo ndipo Daisy akawa anachukua nyaraka zilizokuwa katika familia na kumuonyesha Iliffe pamoja na mswada wa kitabu alichoandika babu yake.

Kutokana na nyaraka hizi Iliffe akaandika paper hii: '‘The Role of the African Association in the formation and Realisation of Territorial Conciousness in Tanzania.’ Mimeo, Universityof East Africa Social Sciences Conference,'' 1968.
'
Iliffe akawa kapatwa na homa ya ''obsession,'' ya akina Sykes anataka kujua mengi zaidi kuhusu ukoo huu.

Daisy akipewa ''assignment,'' anakwenda kwa Abdul Sykes baba yake anauliza anapewa maelezo na ushahidi wa nyaraka.

Iliffe kila akielezwa hili ndani linazuka jingine akataka kujua ilikuwaje Abdul Sykes akawa General Secretary wa Dar es Salaam Dockworkers Union mwaka wa 1948.

Iliffe akapewa maelezo na nyaraka akaandika paper, '‘A History of Dockworkers of Dar es Salaam’' TNR, Dar es Salaam, 71, 1970.

Iliffe kama mimi miaka mingi baadae akawa Sykes, Sykes na Sykes.
Historia imemvutia kila siku anagundua jambo jipya.

Sijui kwa nini Iliffe hakuandika historia ya TANU kwa ukamilifu wake wala hakuwa na shauku ya kukutana na Abdul Sykes, baba wa mwanafunzi wake hodari Daisy ambae kamsaidia sana kuijua historia ya African Association na TANU.

Mohamed Said na yeye kwa kumsoma Iliffe gonjwa la Sykes likamkumba.

Mimi nikaamua kufanya kile Iliffe hakufanya nacho ni kuandika maisha ya Abdul Sykes lakini nikaamua pia kuweka mguu wangu pale unyayo wa Iliffe ulipokanyaga.

Hapa sasa ndipo ilipoaanza safari yangu iliyonifikisha hadi Imhambane kijiji kinachoitwa Kwa Likunyi alipotoka Sykes Mbuwane kuelekea Laurenco Marquis akiwa ameongozana na Chief Mohosh na Wazulu wengine kupanda manowari ya Wajerumani kuja Pangani kuanza vita na Abushiri bin Salim na Mtwa Mkwawa mwishoni mwa miaka ya 1880.

Huyu Chief Mohosh ndiye akaja kujulikana kama Affande Plantan Tanganyika akiwa mkuu wa Germany Constabulary.

Prof. Emmanuel Akyeapong wa Harvard na yeye gonjwa la Sykes likamkumba mwaka wa 2008 akaniandikia kuniomba anijumuishe katika mradi wa Dictionary of African Biography (DAB).

Huu uliuwa mradi wa Harvard na Oxford University Press, New York.
Prof. Akyeampong akaniomba niandike mchango wa Kleist Sykes (1894 - 1949) katika historia ya Afrika.

Mradi huu ulijumisha waandishi na watafiti takriban 500 kutoka kila pembe ya dunia.
Mradi ulikamilika bada ya miaka mitatu na Oxford University Press, New York wakachapa volumes sita ya kazi hii.

Mwisho kwa kuhitimisha napenda kukuambia kuwa umekashifu madrasa pasi na sababu kwani madrasa hazina uhusiano wowote hata kwa mbali katika kuandika historia hii ya Abdul Sykes tunayojadili hapa.

1644935757173.png
 
Schmidt,
Nakuwekea hayo hapo chini usome tuendelee na mjadala:
Hakika kisa cha akina Sykes ni kisa mimi kimenikamata sana.

Utaona kuwa siko peke yangu katika hili.

Mimi hupenda kusema kuwa mtu yeyote ambae angepata bahati ya sema kuokota gunia ndani mna mafaili yenye nyaraka za Sykes angeyasoma yote na kisha angeandika kitabu.

Achilia ule udugu baina yetu lakini siku niliposoma kitabu, ''Modern Tanzanians,'' kitabu alichohariri John Iliffe na kusoma, ''The Townsman: The Life of Kleist Sykes,'' sura iliyoandikwa na mjukuu wa Kleist Sykes, Aisha ''Daisy'' Sykes Buruku historia hii ilikamata fikra zangu.

Ikiwa hujasoma kitabu hiki kitafute ukisome: 'Modern Tanzanians, John Iliffe (ed), East African Publishing House, Nairobi, 1973).

Nakumbuka kama vile jana nilikuwa katika Maktaba ya Taifa, Arusha ndipo nilipokikuta kitabu hiki.

Utafiti wangu wa kutaka kujua mengi ulianza siku ile.
Nikawauliza hawa ndugu zangu juu ya kitabu cha Iliffe.

Wakanifahamisha kuwa babu yao, Kleist Sykes kabla ya kufariki mwaka wa 1949 alikuwa ameandika ''kitabu,'' ambacho alimwachia mwanae Abdul Sykes.

Kwa hakika hakikuwa kitabu bali mswada wa kitabu.

Kleist kwa msaada wa mlezi wake Afande Plantan aliweza kuandika historia ya jeshi lile la Wazulu liliotoka Imhambane kuja Germanostafrika chini ya Hermann von Wissman kupambana na Abushiri bin Salim na Mtwa Mkwawa.

Mwanae Abdu Sykes, Aisha ''Daisy'' Sykes alipoingia Chuo Kikuu cha Afrika ya Mashariki mwaka wa 1967 kusoma Elimu na Historia ndipo alipokutana na Profesa wa Historia John Iliffe na huyu mwalimu wake baada ya kufahamu historia ya akina Sykes na yeye kama mimi akakumbwa na hii ''obsession,'' akataka kujua mengi vipi walifika Tanganyika kutoka Afrika ya Kusini.

Iliffe akampa Daisy ''assignment,'' ya kumkusanyia histori ya ukoo wake.

Hapo ndipo Daisy akawa anachukua nyaraka zilizokuwa katika familia na kumuonyesha Iliffe pamoja na mswada wa kitabu alichoandika babu yake.

Kutokana na nyaraka hizi Iliffe akaandika paper hii: '‘The Role of the African Association in the formation and Realisation of Territorial Conciousness in Tanzania.’ Mimeo, Universityof East Africa Social Sciences Conference,'' 1968.
'
Iliffe akawa kapatwa na homa ya ''obsession,'' ya akina Sykes anataka kujua mengi zaidi kuhusu ukoo huu.

Daisy akipewa ''assignment,'' anakwenda kwa Abdul Sykes baba yake anauliza anapewa maelezo na ushahidi wa nyaraka.

Iliffe kila akielezwa hili ndani linazuka jingine akataka kujua ilikuwaje Abdul Sykes akawa General Secretary wa Dar es Salaam Dockworkers Union mwaka wa 1948.

Iliffe akapewa maelezo na nyaraka akaandika paper, '‘A History of Dockworkers of Dar es Salaam’' TNR, Dar es Salaam, 71, 1970.

Iliffe kama mimi miaka mingi baadae akawa Sykes, Sykes na Sykes.
Historia imemvutia kila siku anagundua jambo jipya.

Sijui kwa nini Iliffe hakuandika historia ya TANU kwa ukamilifu wake wala hakuwa na shauku ya kukutana na Abdul Sykes, baba wa mwanafunzi wake hodari Daisy ambae kamsaidia sana kuijua historia ya African Association na TANU.

Mohamed Said na yeye kwa kumsoma Iliffe gonjwa la Sykes likamkumba.

Mimi nikaamua kufanya kile Iliffe hakufanya nacho ni kuandika maisha ya Abdul Sykes lakini nikaamua pia kuweka mguu wangu pale unyayo wa Iliffe ulipokanyaga.

Hapa sasa ndipo ilipoaanza safari yangu iliyonifikisha hadi Imhambane kijiji kinachoitwa Kwa Likunyi alipotoka Sykes Mbuwane kuelekea Laurenco Marquis akiwa ameongozana na Chief Mohosh na Wazulu wengine kupanda manowari ya Wajerumani kuja Pangani kuanza vita na Abushiri bin Salim na Mtwa Mkwawa mwishoni mwa miaka ya 1880.

Huyu Chief Mohosh ndiye akaja kujulikana kama Affande Plantan Tanganyika akiwa mkuu wa Germany Constabulary.

Prof. Emmanuel Akyeapong wa Harvard na yeye gonjwa la Sykes likamkumba mwaka wa 2008 akaniandikia kuniomba anijumuishe katika mradi wa Dictionary of African Biography (DAB).

Huu uliuwa mradi wa Harvard na Oxford University Press, New York.
Prof. Akyeampong akaniomba niandike mchango wa Kleist Sykes (1894 - 1949) katika historia ya Afrika.

Mradi huu ulijumisha waandishi na watafiti takriban 500 kutoka kila pembe ya dunia.
Mradi ulikamilika bada ya miaka mitatu na Oxford University Press, New York wakachapa volumes sita ya kazi hii.

Mwisho kwa kuhitimisha napenda kukuambia kuwa umekashifu madrasa pasi na sababu kwani madrasa hazina uhusiao wowote hata kwa mbali katika kuandika historia hii ya Abdul Sykes tunayojadili hapa.
P
Quit the BS, Mzee MS. Only fools would believe any of your tales , spins and half-truths.
 
Back
Top Bottom