Paranoia. . . .

Kongosho unauliza kukutwa unatokea guest ni kucheat ? Sio kucheat as well, but unaweza kua commited guilty due ushahidi wa kimazingira ! Nilishakuta violence pahala mwanamke kabambwa anatokea guest. Utetezi wake alidai alikwenda kutafuta chenji ! Inahusu ? Chenji guest ?
 
Ni kweli
Naprefer kuwa paranoid kwa level fulani
Vinginevyo, ntauziwa bata kwenye gunia
Nikiaminishwa ni jogoo :lol:
Kweli dada mkuu,

Katika hii dunia, kila mtu ana level fulani ya ukichaa ila kuna wale ambao wamepitiliza na kuwa machizi kabisa!!

Babu DC
 
Si lazima kweli alikuwa kaenda kucheat
Lakini kwa sababu mwenza wake ni paranoid to a certain level
Ndo maana alianza kuuliza kulikoni.
Paranoia ingekuwa 0% asingeuliza chochote angamini tu kuna sababu ya msingi iliyomfanya huyo mtu kwenda hapo na sio cheating.

 

Vyovyote vile...paranoaic or not, naomba tuwe wakweli,

Huwezi kumkuta mke/mume wako anatoka guest ukabaki bila mstuko...

Tofauti itakuwa kwenye kuchukua hatua na kuelewa/kuamini maelezo utakayopewa!!

Babu DC
 
Kongosho huwezi kuwa paranoid kidogo, either you are or you are not. Kuwa paranoid kunakusanya tabia tofauti pamoja. Unayozungumzia wewe naitambua kama kuwa "makini/alert". Kuwa makini ni tofauti na kuwa paranoid, kwasababu ukiwa makini hukurupuki na kulaumu/shutumu hata sehemu unayoona kabisa hamna tatizo.
 

Babu naomba nikufahamishe kwamba wengi wenye hili tatizo wanapelekeshwa na hisia za kujihisi duni (INFERIOR), na sio kuwa na tabia wanazojaribu kubambikizia wengine. Hawaamini kwamba aliyenaye ameridhika nae, wana wivu uliopitiliza, wana woga wa kugundulika kwa ni "duni" na kuachwa. . . hivyo ndivyo akili zao zinavyofanya kazi.
 
Kwanza za asubuhi, mimi ningekuomba japo unipe hints due early stage diagnosis of that disease !

Kutokua na imani na mtu/watu kwa kiasi kikubwa, kuamini kitu ambacho hakipo, wivu usio na kipimo, woga/hofu/wasiwasi juu ya kitu ambacho hakipo. . . . kwa kifupi ni watu ambao ni very delusional.
 
Hayo ni maradhi ya kimalezi,yanatibika kwa ushauri,tatizo mtu mwenye maradhi haya hajui kama anayo mpaka akutane na mtaalamu wa saikolojia!So ushauri kwa hawa ni kuwakutanisha na madaktari hawa wa saikolojia!

Malezi, genetics, mazingira, kukosa uelewa, kutojiamini vyote vinaweza vikasababisha hilo tatizo.
 

Na mwanamke aishi kama mwanamke sio kama msichana
 
Kutokua na imani na mtu/watu kwa kiasi kikubwa, kuamini kitu ambacho hakipo, wivu usio na kipimo, woga/hofu/wasiwasi juu ya kitu ambacho hakipo. . . . kwa kifupi ni watu ambao ni very delusional.

Kwa hiyo sasa wewe unaongelea wagonjwa!!

Kama mtu anakuwa na dalili zote hizo tena kwa kipimo cha juu kabisa (extremes) basi siyo mzima hata kidogo.

Babu DC!
 
Samahani sana ndugu,

Kwani huo ugonjwa una level moja tu? Hakuna wale ambao hali yao ni mild na wale ambao ni serious?

Zipo aina kadhaa.
. .Paranoid personality disorder (tunayoongelea) inaweza ikamalizwa kwa msaada wa mwanasaikolojia bila dawa.
. . Schizofrenia paranoia hii inahitaji dawa na constant reminder kwamba anachoona hakiexist.

Nadhani kuna nyingine moja ila nimesahau, will look it up.
 
Kwa hiyo sasa wewe unaongelea wagonjwa!!

Kama mtu anakuwa na dalili zote hizo tena kwa kipimo cha juu kabisa (extremes) basi siyo mzima hata kidogo.

Babu DC!
Ni ugonjwa kitaalamu/tabia kimazoea. . ..
 
Ni ugonjwa kitaalamu/tabia kimazoea. . ..


Ahsante Lizzy,

Mie toka mwanzo nilidhani tunaongelea paranoia katika perspectives za watu wa kawaida...

Kumbe ni kitaalamu....Basi hao ni wagonjwa na wenzi wao wawasaidie wakatibiwe.

Ningesema wawapige chini ila kumwacha mwenzi wako katika ugonjwa ni dhambi kubwa sana!!

Babu DC!
 
Paranoia ni kitendo cha mtu kuwa na tabia ya kuwa na wasiwasi,hofu, shaka, na kutoamini mtu mwingine bila sababu ya msingi/ushahidi. Na mara nyingi hua inasukumwa na wivu uliopitiliza kiasi pia kukosa uelewa.

...i doubt hiyo ya kutokuwa na sababu ya msingi,...mfano; nikiwa na lock simu yangu, nikirudi nyumbani straight najifungia bafuni kukoga, naacha tendo la ndoa makusudi, nk, nk....sitakujengea paranoia? weee Lizzy wee...lol
 
Kabisa kabisa without TRUST a relationhip is doomed to fail....Hakuna anaye kataa hapo.

Afadhali afadhali leo umekuja na point nzuri sanai.

But trust comes upon fidelity, honesty, and openness.

Smart people don't just trust blindly. Stupid people do.
 
@Lizzy
Sasa umenipa kazi ya kwenda kusoma kitu hii kinagaubaga
Naona kama siifahamu vizuri hasa baada ya kusema ipo hadi inayotibiwa kwa dawa!!
 
Umeonaee
Hauushurutishi moyo na wala hauishurutishi akili kuamini mtu
Ni mchakato wa muda, hadi utakaporidhika kutokana na vipimo vyako vya kuamini mtu

Kabla ya hapo, kuna paranoia ya kiwango fulani.
But trust comes upon fidelity, honesty, and openness.

Smart people don't just trust blindly. Stupid people do.
 

Hiyo ya utaalam imekuja baada ya watu kutaka ufafanuzi zaidi, hata kuwa overly possesive au hata controling ni TABIA ambazo mtu anaweza akaacha mwenyewe, ila kwasababu zinaweza pia zikaondolewa kwa msaada wa wanasaikolojia basi twaweza kuita ugonjwa.
 

...i doubt hiyo ya kutokuwa na sababu ya msingi,...mfano; nikiwa na lock simu yangu, nikirudi nyumbani straight najifungia bafuni kukoga, naacha tendo la ndoa makusudi, nk, nk....sitakujengea paranoia? weee Lizzy wee...lol

Hapo hautokua umenisababishia paranoia ila umenipa sababu ya kujiuliza kuhusu tabia yako Mbu. Hata kujiuliza mwenzi kwanini amechelewa/alikua wapi muda wote sio kuwa paranoid bali ni kuishi kwenye ulimwengu halisi, huku ukiwa aware of any changes that occurs along the way, REAL changes na sio za kulazimisha.
 
@Lizzy
Sasa umenipa kazi ya kwenda kusoma kitu hii kinagaubaga
Naona kama siifahamu vizuri hasa baada ya kusema ipo hadi inayotibiwa kwa dawa!!

Hahahaha. . . .
Kongosho yapo magonjwa mengi ya kisaikolojia yanayotibika/punguzwa makali kwa dawa (mostly drugs zinazosaidia kubalance neurotranssmiters, hormones ambazo zinahusika sana kwenye namna information zinavyosafirishwa kwenye akili yetu). . . inaitwa biochemical therapy. Ila hii niliyoandika hapa kwamba inatibiwa kwa dawa ni zaidi ya kuwa paranoia, tofauti na Paranoid personality disorder. Anayehitaji dawa ni mtu ambae anakua tayari hawezi kutofautisha nini ni kweli na nini sio kweli (real and unreal) alafu on top of that, anakua fixed on something (paranoid). Anaweza akaamini kuna watu wanapanga kumuua, anaona na kuongea na watu wasiokuwepo (delusional) na vitu kama hivyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…