Kidogo kabla ya yote leo nimeamkia youtube make ni siku sijaangalia mechi za hawa miamba ya PSG..nilichokiona ikabidi niamkie kijiwe maarufu cha kahawa ila ngoja tuanzie mbali kabla ya kwenda penyewe ,Bahati mbaya niliadisiwa sana kuhusu Pele hata na wale ambao hawakuwa wamemshuhudia(raha ya kahawa hii), nikapewa soga nyingi za Almando Maradona kuwahukumu watoto na wajukuu wa Malkia Elizabeth kwa mkono wa Mungu...... Bahati nzuri kwa walioniadisia sikuwa nimeanza kulewa Kahawa na mimi kama sasa.
Zamani kulikuwa na vipaji kuliko sasa, hapa wazamani ndiyo fahari yao kusema hayo(walijinasibu sana juu ya zamani yao). Niliamka nikamkuta George Opong Weah na miguu yake, sikuhadithiwa hata kidogo kuhusu tajiri Del Piero na zile dakika zake, macho yakawa rafiki wa De Lima na uronaldo wake, kipara cha Zidane na mawani ya Edger...... Nikaona siku za Rivaldo zikipishana na tabasamu la Gaucho kila sehemu, nikamuona Michael Owen na kale kaumri kake kwenye lile likiatu la pembeni mwa Allan Shearer.
Yes...! Mbuyu ulianza kama mchicha, hapa wengi tuliamini miguu ya Jack Wilshere itaishia gizani kama shangilia ya Michael Owen akinywa Calasberg na kuongelea Simens kabla ya kutumia AIG......... Yes..! Na ndivyo ilivyotokea tulianza kumuangusha Wilshere kwanza sisi na mawazo yetu fananishi na Owen hata kabla ya mkopo wa Bournmouth na safari ya babu Wenger .
Ndio.....! Kama tunavyoamini mwisho wa Klylian Mbappe ni rafiki na tamati fananishi ya va va vum TH14(Thiery Henry) hapa Henry alishinda kashinda na kushindana. Ni rahisi sana kuwaza namna mawazo yetu yanaumba kama yalivyomuumbia Jack na kipaji chake...... Sina shaka ukiachana na Ronaldo De Assis Moreira(Ronaldinho Gaucho) basi Mfalme wa siri Mbappe yu kwenye mstari wa kukubalika na kupendwa baada ya Ng'olo Kante(ndio maana ile timu ya mtaani kwety U19 kuna Mbappe wanne kwenye kikosi chao).
Leo ya Mbappe imejificha kwenye Magome tu ya miti ikisubiri nguo mpya. Ndio maana yeye si adui wa Cavan wala si shahidi wa Neymar kwa sasa, anajikuta kwenye kibendera na Cavan na anajibeba mabegani mwa Neymar nyuma ya goli....... Siku Mbappe ataacha kutufichia mikono makwapani ndio atakuwa teyari hadharani.
Tunamalizia chaji ya Messi wetu na Ronaldo wetu, huku tukimsubiri Mfalme wa Watoto wetu atoe mikono makwapani karibu na kibendera....... Awali tuliamini Neymar anakwenda kutengeneza ufalme bila ya kujua kilichopo makwapani mwa Kylian