PART 2: Haya hapa makundi yanayofurahia ama kuridhishwa na utawala wa awamu ya sita

PART 2: Haya hapa makundi yanayofurahia ama kuridhishwa na utawala wa awamu ya sita

msovero

JF-Expert Member
Joined
Jun 30, 2019
Posts
863
Reaction score
1,534
Baada ya kuangazia makundi ya watu wanaochukia utawala wa Rais Samia sasa ni zamu ya makundi yanayoridhishwa ama kufurahishwa na utawala wake.

1. WAFANYABIASHARA
Katika kipindi cha miaka mitano iliyopita wamepita kwenye dhoruba na sekeseke zito katika biashara zao ikiwemo kubambikiwa kodi, kutishiwa ama kushitakiwa kwa kesi za uhujumu uchumi, kufungiwa biashara zao na hata wengine kutekwa na watu wasiojulikana.

Baada ya ujio wa Rais Samia tumeona ama kushuhudia wafanyabiashara wakipata ahueni katika biashara zao ambapo baadhi kwa waliokuwa wamefunga wameanza kufungua biashara zao, waliokuwa wanaogopa kuwekeza kwenye biashara kwa sasa wameanza kuwekeza, vilio vya wafanyabiashara kuchukuliwa pesa kwenye akaunti zao kinyume na makubaliano kwa sasa havisikiki tena.

Hivyo kiujumla kwa sasa wafanyabiashara ni miongoni mwa watu watakaofurahia utawala wa sasa kulinganisha na uliopita kwani Rais Samia kaanza kuwatengenezea mazingira rafiki ya kufanya biashara zao kwa uhuru licha ya changamoto za hapa na pale ikiwemo ya kuwapanga wafanyabiashara wadogo almaarufu kama 'machinga'.

2. WATUMISHI WA UMMA

Ni miongoni mwa wahanga wa utawala uliopita kwani katika kipindi chote cha miaka mitano mfululizo wamenyimwa haki zao za kiutumishi ikiwemo kupandishwa vyeo na madaraja. Hivyo kwa ujio wa Rais Samia wamekuwa na matumaini mapya kwani haki zao za msingi walizozikosa kwa muda mrefu zimeanza kufanyiwa kazi huku sikio lao wakizidi kulitega kwenye mei mosi ya mwakani ambapo mama Samia anaenda kuwarejeshea furaha yao waliokosa kwa kipindi kirefu.

3. VIJANA WASOMI WASIO NA AJIRA
Huwezi kutaja wahanga wakubwa wa awamu ya tano bila kuwaweka vijana wa kundi hili. Kwani ni katika awamu ya tano ambapo tumeshuhudia vijana hawa wakidharualiwa na kukejeliwa wazi wazi na baadhi ya waliokuwa viongozi wa utawala uliopita ikiwemo kuambiwa kuwa wajiajiri ingali hawana mitaji ya kujiajiri kwa chochote.

Hivyo basi, baada ya mh. Samia kuingia madarakani kundi hili limekuwa na matumaini mapya kwamba huenda 'chief hangaya ' akawafuta machozi kwa kutoa vibali vya ajira tofauti na aliyekuwa mtangulizi wake ambaye yeye 'ajira kwa vijana' hakikuwa kipaumbele chake. Ingawa kundi hili linaweza kubadili uelekeo endapo fursa za ajira zitaendelea kubanwa kama ilivyokuwa katika awamu iliyopita.

4. WAPAMBANAJI NA WACHAKARIKAJI
Hawa wana malengo ya kufika mbali na kufanikiwa kimaisha hivyo wanaamini ndoto zao zitatimia kupitia uwepo wa utawala bora unaojali haki za binadamu chini ya chief Hangaya na sio ubabe na ukatili kama ilivyokuwa katiaka utawala wa mwendazake.

5. WAHANGA WA SIASA ZA DEMOKRASIA NA UTAWALA BORA

Hapa nazungumzia baadhi ya wanasiasa waliokuwa wahanga wa siasa za mwendazake hususani wa kutoka vyama pinzani kwa sasa wana auheni ya kushiriki siasa za kukosoa mwenendo wa serikali licha ya changamoto za hapa na pale ambazo zinaendelea kufanyiwa kazi na kuhakikisha kwamba suala zima la utawala bora na demokrasia vinarejeshwa katika hali yake. Kwa kifupi kundi hili kwa sasa linapumua kulinganisha na mateso na manyanyaso waliopitia katika utawala na siasa za mwendazake.

Hata hivyo makundi ya watu wanaomkubali chief Hangaya ni mengi ila kwa sababu ya muda nimeona niainishe hayo machache yaliyoguswa moja kwa moja na utawala uliopita na hivyo naishia hapa kwa siku ya leo.


Pia soma,

Thread 'PART 1: Hawa hapa watu wanaomchukia na kuchukia utawala wa Rais Samia' PART 1: Hawa hapa watu wanaomchukia na kuchukia utawala wa Rais Samia
 
Hakikisha unasoma maudhui yote kabla ya kukomenti chochote
 
Habari.

Kuna watu waliimba na kuhubiri,

Kusujudu na kurukaruka.

Kunywa bia na kuponda bata la kufa mtu kwamba kwa maisha yao yatakuwa bora mno baada ya Magufuli.

Leo ni miezi 8 bila Magufuli lakini kila wakigeuka huku hakuna umeme, wakigeuka hakuna maji ,wakigeuka huku mbolea lakini moja, wakigeuka huku wanafukuzwa kwenye migodi ,wakigeuka huku wanafukuzwa kwenye mitaa, wakigeuka huku Mungu wao yuko jela kwa ugaidi.

Leo ndiyo wamejua Magufuli alikuwa anafanya kwa ajili yao?
Jinga kabisa na bado mtaendelea kuwa watumwa hivyo hivyo.
Waliowadanganya wamtukane Magufuli wote wamepata mabwana Ulaya wanalishwa bure.

Malipo ni hapa hapa duniani.
 
Bila katiba Imara na yenye kutoa dira na mwelekeo wa Taifa tutabaki tunatabiri kupendwa na kutopendwa kwa viongozi kila uchao.
 
Kwahii orodha yako inaonyesha Raisi anachukiwa na makunxi yote ya jamii.
Kwa mtazamo wako sio?

Kama ndivyo basi sikupingi unless uongezee nyama kwenye hoja yako
 
Watumishi wanafurahi nn mpuuz wewe? Seriakali inajenga madarasa wkt hakuna ofisi za walimu,hakuna ongezeko la mishahara hakuna mifumo Bora ya kwa watumishi hasa walimu yeye anaangalia madarasa tu Sasa watumishi gan wanaomfurahia au wewe na familia yako? Fanyeni tafiti vzri kabla hauja post utumbo au umetumwa na mama kuona presha ya watumishi ktk utawala wake?
 
Watumishi wanafurahi nn mpuuz wewe? Seriakali inajenga madarasa wkt hakuna ofisi za walimu,hakuna ongezeko la mishahara hakuna mifumo Bora ya kwa watumishi hasa walimu yeye anaangalia madarasa tu Sasa watumishi gan wanaomfurahia au wewe na familia yako? Fanyeni tafiti vzri kabla hauja post utumbo au umetumwa na mama kuona presha ya watumishi ktk utawala wake?
Haya ndio madhara ya kusoma heading ukakimbilia kukoment pasipo kuelewa content ya kilichoandikwa lakini right ungesoma na kuelewa usingeandika hiki ulichokiandika hapa
 
Hakikisha unasoma maudhui yote kabla ya kukomenti chochote
Maudhui yote???


Yote na yote serikali iangalie sana utendaji wa mashirika ya umma kama TANESCO, hii ni ishu serious kwakweli, umeme unakatika bila mpangilio maji ndio usiseme!!
Huku niliko kila siku umeme unakatika na HAKUNA taarifa ya tatizo hilo mfano leo tangu asubuhi hakuna umeme.

Haya mambo mh asipoyaangalia kaa upana yatamharibia sana!!


Suala la wafanyabiashara pia bado ni changamoto, nimekushangaa unasema wananufaika sijui unamaanisha nini.

Kwa ufupi suala la machinga limeleta SINTOFAHAMU, mbaya zaidi vibanda vyao vinakumbwa na dhoruba ya kuungua Moto.

tuendelee kuonjoi maisha na Mama Ssmia, kazi iendelee!!
 
Namkubali Samia kwa kuwa anafuata sheria na anamaamuzi magumu. Magu ishu ya tozo na zile kelele angepindua.
Suala la wamachinga na madalali kwa Rais mpenda cheap politics asingeweza kukaza.
Wananchi wafuata mkumbo sahivi inamlaumu kwa umeme na maji, projects zilizopending. Katulia tu maana anajua anazifanyia kazi na zipo kwenye right track.
Uwezo wake wa kuwa mtulivu katika vipindi vigumu unamfanya aweze kutoa maamuzi bora na ya busara.
 
Dah..... Mbona mnahangaika sana na marehemu? JPM hayupo duniani.....na hatagombea.....🤣🤣🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom