Uchaguzi 2020 Pascal Mayalla atangaza nia kugombea Ubunge

idawa

JF-Expert Member
Joined
Jan 20, 2012
Posts
25,284
Reaction score
38,364
Mwandishi nguli na Mchambuzi Mkongwe wa habari Pascal Mayalla ametangaza nia ya kugombea ubunge.

Amesema hivyo baada ya kuona mapungufu mengi kwenye bunge lililopita, amejipima na kuona anatosha kuwania hiyo nafasi.

Hajataja Jimbo, Wala Chama atakachotumia kuwania hiyo nafasi.

Ila amesisitiza ieleweke anaenda bungeni.

Kwa niaba ya Wana JF wote nakutakia safari na mafanikio mema kwenye hiyo safari yako mpya ya utumishi.

Chanzo: Pascal Mayalla . Star tv leo.
===

Pascal Mayalla athibitisha
 
Ni kweli kabisa, nimetangaza nia kugombea ubunge, na sikutangaza ni jimbo gani au kupitia chama gani, ili kuepuka taking undue advantage dhidi ya wagombea wengine ambao hawana access na media.

Wana JF wenzangu, naombeni mniunge mkono katika azma yangu hii.

Paskali Mayalla
 
Kawe kunani? Ulitakiwa uwe na majibu. Kila la kheri!
 
Unaungwaje mkono wakati mchakato umekuwa wa usiri?
Anyway, nakutakia kila la heri!
 
Kawakilishe vyema jimbo letu la JF
 
Tunakuungaje mkono binadamu usiye muwazi,yawezekana unagombea kupitia chama cha kishetani,binadamu aliyekamilika na kujiamni huwa haogopi anaweka wazi ili kufunika minongono,tatizo lako huwa hujui hata kutudanganya ili tusikuone mnafiki wa taifa.
 
Je humu JF kutakua na kituo cha kupigia kura?
Kitawekwa jukwaa lipi.
Tuelekeze basi jinsi ya kukuunga mkono.
 
CCM oyeeee! Kanda pendwa tuu hakuna jingine.

Sent from my TECNO RA7 using JamiiForums mobile app
 
Hongera Sana mkuu kapambane, Sema popote pale ulipo umekuwa Balozi bora kabisa wa JF hujawahi kukosa kuitaja.

Bila shaka utaendelea kuwa mtetezi wa JF hata baada ya kuikwaa hiyo nafasi.

Tofauti na viongozi wengine wanaoitaja JF kiwoga woga ama kuikana kabisa wakati inajulikana ni wadau kindakindaki hapa.
 
Paskali ni wewe huyo au kivuli chako?
Ikiwa kweli niweke kuwa Manager wako wa kampeni!!!!
Na najua huendi mbali na Kawe!!
 
Watu wengi wanakimbilia bungeni kwa lengo la kubadili maisha yao na si ya wananchi.

Kwenye uchaguzi mkuu ingekuwa ni vyema tukachagua nafasi ya urais na udiwani. Sijaona umuhimu na ulazima wa uwepo wa Bunge. Mihimili miwili UTAWALA na Mahakama inajitosheleza kabisa.

Fedha zinazotengwa kuendesha bunge kwa miaka mitano zinaweza kutumika katika maeneo mengine ya maendeleo kwa wananchi.


NB: Nimeandika utani ambao hata mimi binafsi siuelewi[emoji16][emoji16]
 
Pascal Mayalla anashindana na askofu Gwajima kule Kawe!
 
Je humu JF kutakua na kituo cha kupigia kura?
Kitawekwa jukwaa lipi.
Tuelekeze basi jinsi ya kukuunga mkono.
Hawa hawa Wana JF ndio watanzania walioko huko maofisini, Masokoni, Machinga na sehemu mbalimbali hata kwenye Vyombo vya maamuzi...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…