Damaso
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 3,978
- 6,739
Mtanzania ateuliwa kuwa Mkuu wa Shirika la Ujasusi la FBI nchini Marekani. Hii ni hatua ya uundaji wa serikali wa utawala mpya wa Rais Trump.
Kash Patel amezaliwa Marekani lakini Baba yake ni Mganda na Mama yake ni Mtanzania walioamua kuhamia Marekani ambako huko ndiko Kash Patel alikozaliwa. Familia hii ina asili ya Uhindi (Gujarati).
NB: Wahindi ukoo huchukua kwa Mama, kwahiyo Patel ni Mtanzania.
Kama kawaida yetu, kudandia treni kwa mbele, sijui ni nani alitupatia ugonjwa huu wa ujinga kiasi hiki? Wazee wa free rides! Je tunapata faida gani kuhubiria dunia kuwa watu wenye uraia wa nchi zingine waliofanikiwa ni watanzania?
Kijana akicheza Ligi ya Ujerumani basi media zinafukuzana kuandika makala kuwa Yussuf Yurary Poulsen kuwa ni mtanzania? Ukiuliza sababu za kwanini ni Mtanzania utabaki kucheka tu, ukitazama vyema utaona Poulsen hana utanzania wowote.
Malaika Mihambo alivyokiwasha kwenye michezo ya Olympic tukaanza ngonjera zetu, kuwa Malaika Mihambo ni mtanzania ilihali yeye ni Mjerumani. Sasa hivi tumeanza kumzunguza Patel kama kijana wetu mzawa wakati kiuhalisia yeye ni Mhindi, Mgujarati mwenye asili sawa na kina Mahatma Gandhi, Dadabhai Naoroji, Azim Premji, Jamsetji Nusserwanji Tata, Diana Edulji, Sam Pitroda, Ajay Jadeja, Irfan Pathan, pamoja na Ravindra Jadeja.
Tanzania hakuna uraia pacha na wengi wa hawa watu wanaopata mafanikio makubwa wanayapata wakiwa sio raia tena wa Tanzania.
Haina mantiki ya msingi na sio afya njema kuona Mwaisa amekaa Tukuyu akicheza mpira na hakuna ukurasa wa TFF wowote umewahi kumuonesha ila akibadilisha uraia akaenda Australia na kukiwasha haswa, admin wa ukurasa wa TFF kule Facebook utaona anavyosifia kuhusu kiwango chake na kuelezea kuwa ni mtanzania.
Tuache hii tabia, hawa ambao tunawaona wanapata shavu basi tunaanza kutafiti kuhusu maeneo gani Tanzania wazazi wao walipita, sio jambo jema.
Abeba pamoja na mumewe Cherenet wameingia kimagendo Tanzania wakitoka Ethiopia wakitamani kwenda Afrika ya Kusini, kwa bahati nzuri au mbaya wakafanikiwa kufika Mbeya na kukaa kwa muda wa miaka mitano na baadaye kupata nafasi ya kwenda Ufaransa.
Abeba bahati nzuri alikuwa mjamzito hivyo alijifungua mtoto wa kiume na kumpa jina la Dejen ama Daud ksa Kiswahili, Dejen anapenda michezo haswa kikapu na anafanikia kuingia Academy ya Riviera Basketball Academy ambapo anafanya mazoezi kwa bidii kubwa, akiwa na miaka 19 anapata nafasi ya kuonekana na scout wa timu ya Golden State Warriors na kupewa nafasi ya kucheza Pre Season.
Halafu asubuhi unaamka unakutana na wachambuzi njaa wameshiba mihogo wakimzunguza kuwa Dejen ni mtanzania kwa kigezo kuwa aliishi Mbeya, wanasahau kabsa kuwa Abeba pamoja na Cherenet hawana uhusiano wowote na Tanzania, sio kabila bali hata asili yao.
Patel amezaliwa Marekani lakini asili yake ni Mgujarati sio Tanzania hana utanzania wowote, kina Yeriko na wengine acheni kupotosha umma, mtu akipita Tanzania sio kigezo cha yeye kuwa mtanzania, watoto wa mabalozi kutoka nchi nyingine wakizaliwa Tanzania haitoshi wao kuwa watanzania.
Tufikie sehemu tuheshimu jitihada za nchi zao ambazo zimewatengeneza wakafikia hatua hizo. Msilete zile Ngonjera kuwa Obama amekuwa Rais wa Marekani basi Obama ni Mkenya, hakuna hicho kitu.
Kash Patel amezaliwa Marekani lakini Baba yake ni Mganda na Mama yake ni Mtanzania walioamua kuhamia Marekani ambako huko ndiko Kash Patel alikozaliwa. Familia hii ina asili ya Uhindi (Gujarati).
NB: Wahindi ukoo huchukua kwa Mama, kwahiyo Patel ni Mtanzania.
Kama kawaida yetu, kudandia treni kwa mbele, sijui ni nani alitupatia ugonjwa huu wa ujinga kiasi hiki? Wazee wa free rides! Je tunapata faida gani kuhubiria dunia kuwa watu wenye uraia wa nchi zingine waliofanikiwa ni watanzania?
Kijana akicheza Ligi ya Ujerumani basi media zinafukuzana kuandika makala kuwa Yussuf Yurary Poulsen kuwa ni mtanzania? Ukiuliza sababu za kwanini ni Mtanzania utabaki kucheka tu, ukitazama vyema utaona Poulsen hana utanzania wowote.
Malaika Mihambo alivyokiwasha kwenye michezo ya Olympic tukaanza ngonjera zetu, kuwa Malaika Mihambo ni mtanzania ilihali yeye ni Mjerumani. Sasa hivi tumeanza kumzunguza Patel kama kijana wetu mzawa wakati kiuhalisia yeye ni Mhindi, Mgujarati mwenye asili sawa na kina Mahatma Gandhi, Dadabhai Naoroji, Azim Premji, Jamsetji Nusserwanji Tata, Diana Edulji, Sam Pitroda, Ajay Jadeja, Irfan Pathan, pamoja na Ravindra Jadeja.
Tanzania hakuna uraia pacha na wengi wa hawa watu wanaopata mafanikio makubwa wanayapata wakiwa sio raia tena wa Tanzania.
Haina mantiki ya msingi na sio afya njema kuona Mwaisa amekaa Tukuyu akicheza mpira na hakuna ukurasa wa TFF wowote umewahi kumuonesha ila akibadilisha uraia akaenda Australia na kukiwasha haswa, admin wa ukurasa wa TFF kule Facebook utaona anavyosifia kuhusu kiwango chake na kuelezea kuwa ni mtanzania.
Tuache hii tabia, hawa ambao tunawaona wanapata shavu basi tunaanza kutafiti kuhusu maeneo gani Tanzania wazazi wao walipita, sio jambo jema.
Abeba pamoja na mumewe Cherenet wameingia kimagendo Tanzania wakitoka Ethiopia wakitamani kwenda Afrika ya Kusini, kwa bahati nzuri au mbaya wakafanikiwa kufika Mbeya na kukaa kwa muda wa miaka mitano na baadaye kupata nafasi ya kwenda Ufaransa.
Abeba bahati nzuri alikuwa mjamzito hivyo alijifungua mtoto wa kiume na kumpa jina la Dejen ama Daud ksa Kiswahili, Dejen anapenda michezo haswa kikapu na anafanikia kuingia Academy ya Riviera Basketball Academy ambapo anafanya mazoezi kwa bidii kubwa, akiwa na miaka 19 anapata nafasi ya kuonekana na scout wa timu ya Golden State Warriors na kupewa nafasi ya kucheza Pre Season.
Halafu asubuhi unaamka unakutana na wachambuzi njaa wameshiba mihogo wakimzunguza kuwa Dejen ni mtanzania kwa kigezo kuwa aliishi Mbeya, wanasahau kabsa kuwa Abeba pamoja na Cherenet hawana uhusiano wowote na Tanzania, sio kabila bali hata asili yao.
Patel amezaliwa Marekani lakini asili yake ni Mgujarati sio Tanzania hana utanzania wowote, kina Yeriko na wengine acheni kupotosha umma, mtu akipita Tanzania sio kigezo cha yeye kuwa mtanzania, watoto wa mabalozi kutoka nchi nyingine wakizaliwa Tanzania haitoshi wao kuwa watanzania.
Tufikie sehemu tuheshimu jitihada za nchi zao ambazo zimewatengeneza wakafikia hatua hizo. Msilete zile Ngonjera kuwa Obama amekuwa Rais wa Marekani basi Obama ni Mkenya, hakuna hicho kitu.