mwanakaya
Member
- Mar 17, 2012
- 56
- 183
Wakati anauzwa kwenda kujiunga na Juventus mwaka 2012 wengi walisikitika sana. Walisikitika kumuona kijana mweusi mwenye kipaji kikubwa akiondoka kwa sababu rahisi. Wakati ule Pogba alitoa sababu kwamba anaondoka kwenda kutafuta sehemu atakakopata muda mwingi wa kucheza.
Kijana huyu wa kifaransa alikuwa anaondoka kwenye klabu iliyomlea toka utotoni sababu kubwa ikiwa ni kurudishwa kwa wajina wake Paul Scholes aliyekuwa amestaafu msimu wa nyuma yake. Pogba alijiona hathaminiwi ndio maana mchezaji aliyestaafu anarudishwa kuja kucheza nafasi ya kiungo ambayo yeye pia anacheza.
Kwa upande mwingine kocha wa wakati huo Sir Alex Ferguson alikuwa anamlalamikia wakala wa mchezaji huyo Mino Riola kwamba ndio sababu ya kijana huyo kuondoka. Wengi hatukumuelewa SAF. Tulimpuuza.
Hatimaye Pogba akenda Italia na kucheza kwa mafanikio. Naada ya miaka mitano akarejea kwenye timu yake kwa kuvunja rekodi ya dunia ya uhamisho. Baada ya misimu miwili Pogba ameanza malalamiko. Hana furaha. Hafurahishwi na namna anavyochezeshwa. Hapa ndipo ninapokumbuka maneno ya Ferguson. Shida sio Pogba ni Wakala wake.
Kwangu mimi sababu anazotoa Pogba ni za kitoto. Nijuavyo timu haitakiwi kuingia kwenye mfumo wa mchezaji. Mchezaji anatakiwa aingie kwenye mfumo timu. Kuna mifano mingi, mmoja ni Wayne Rooney. Kiasili Rooney ni mshambuliaji lkn kutokana na kubadilika kwa mifumo tangu kipindi cha Ferg Wazza amechezaji nafasi tofauti. Kuna wakati alichezaji akitokea kushoto, kuna kipindi akacheza CF, kuna kipindi akacheza nyuma ya mshambuliaji hasa kipindi akicheza na washambuliaji tofauti..Berbatov, Tevez, Chicharito, RVP na hata Cadabra. Kuna kipindi alicheza namba nane. Njoo kwa CR7. Amewahi kucheza Winga ya kulia akiwa man u, akacheza kushoto akiwa Madrid, akacheza CF pia.
Pogba akiendelea kuendeshwa na Riola atapotea mapema pamoja na kipaji chake kikubwa. Yatamkuta ya Super Mario Baloteli. Kipaji peke yake bila juhudi na nidhamu ni kitu bure.
Sent using Jamii Forums mobile app
Kijana huyu wa kifaransa alikuwa anaondoka kwenye klabu iliyomlea toka utotoni sababu kubwa ikiwa ni kurudishwa kwa wajina wake Paul Scholes aliyekuwa amestaafu msimu wa nyuma yake. Pogba alijiona hathaminiwi ndio maana mchezaji aliyestaafu anarudishwa kuja kucheza nafasi ya kiungo ambayo yeye pia anacheza.
Kwa upande mwingine kocha wa wakati huo Sir Alex Ferguson alikuwa anamlalamikia wakala wa mchezaji huyo Mino Riola kwamba ndio sababu ya kijana huyo kuondoka. Wengi hatukumuelewa SAF. Tulimpuuza.
Hatimaye Pogba akenda Italia na kucheza kwa mafanikio. Naada ya miaka mitano akarejea kwenye timu yake kwa kuvunja rekodi ya dunia ya uhamisho. Baada ya misimu miwili Pogba ameanza malalamiko. Hana furaha. Hafurahishwi na namna anavyochezeshwa. Hapa ndipo ninapokumbuka maneno ya Ferguson. Shida sio Pogba ni Wakala wake.
Kwangu mimi sababu anazotoa Pogba ni za kitoto. Nijuavyo timu haitakiwi kuingia kwenye mfumo wa mchezaji. Mchezaji anatakiwa aingie kwenye mfumo timu. Kuna mifano mingi, mmoja ni Wayne Rooney. Kiasili Rooney ni mshambuliaji lkn kutokana na kubadilika kwa mifumo tangu kipindi cha Ferg Wazza amechezaji nafasi tofauti. Kuna wakati alichezaji akitokea kushoto, kuna kipindi akacheza CF, kuna kipindi akacheza nyuma ya mshambuliaji hasa kipindi akicheza na washambuliaji tofauti..Berbatov, Tevez, Chicharito, RVP na hata Cadabra. Kuna kipindi alicheza namba nane. Njoo kwa CR7. Amewahi kucheza Winga ya kulia akiwa man u, akacheza kushoto akiwa Madrid, akacheza CF pia.
Pogba akiendelea kuendeshwa na Riola atapotea mapema pamoja na kipaji chake kikubwa. Yatamkuta ya Super Mario Baloteli. Kipaji peke yake bila juhudi na nidhamu ni kitu bure.
Sent using Jamii Forums mobile app