Pauline Gekul ahoji uwiano wa adhabu kwa wafanyabiashara kwenye muswada wa marekebisho ya Sheria ya ushindani 2024

Pauline Gekul ahoji uwiano wa adhabu kwa wafanyabiashara kwenye muswada wa marekebisho ya Sheria ya ushindani 2024

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Mbunge wa Babati Mjini, Pauline Gekul amesema kiwango cha adhabu kilichopendekezwa kwenye Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Ushindani wa Mwaka 2024, kwa wafanyabiashara watakaoshindwa kuweka wazi bei za bidhaa wanazouza, kiendane na ukubwa wa biashara husika.

Muswada huo umependekeza kuweka sharti la kila mfanyabiashara nchini kuweka hadharani bei ya kila bidhaa anayouza, na kupendekeza adhabu ya faini kati ya shilingi 10,000 hadi shilingi 1,000,000 kwa atakayeshindwa kufanya hivyo.

Akichangia muswada huo bungeni leo, Gekul amesema licha ya kushushwa kwa adhabu hiyo, bado inapaswa kuzingatia ukubwa wa biashara husika.

 
Kwani kuna ubaya kwenye soko huria kila mtu akijipangia bei atakavyo?.
Naomba msaada ndugu wanazuoni.
 
Mbunge wa Babati Mjini, Pauline Gekul amesema kiwango cha adhabu kilichopendekezwa kwenye Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Ushindani wa Mwaka 2024...
Inaenda kutungwa sheria nyingine ya kuifavor state
 
Huyu alitakiwa awe lupango ananyea debe.

Alichomeka vijana wa watu chupa za makalio.
 
Serikali kutunga Sheria ya sharti kuweka lebo ya bei ya bidhaa au huduma chanzo ITV habari. Nimeipenda hii maana wauzaji wengi wa bidhaa au huduma wamekuwa kama wamachinga. Hapa Serikali inaupiga mwingi kwa kuwajali walaji. Mimi nimeipenda wewe je?
 
Mbunge wa Babati Mjini, Pauline Gekul amesema kiwango cha adhabu kilichopendekezwa kwenye Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Ushindani wa Mwaka 2024...
Ni watu wastaarabu na wenye akili nzuri pekee ndio watakaopenda mambo haya.
 
Back
Top Bottom